Mwanzo 15:1-21

  • Agano kati ya Mungu na Abramu (1-21)

    • Miaka 400 ya mateso yatabiriwa (13)

    • Mungu arudia ahadi aliyompa Abramu (18-21)

15  Baada ya hayo neno la Yehova likamjia Abramu katika maono, likisema: “Usiogope,+ Abramu. Mimi ni ngao yako.+ Thawabu yako itakuwa kubwa sana.”+  Abramu akasema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, utanipa nini, kwa sababu mpaka sasa sina mtoto na yule atakayerithi nyumba yangu ni Eliezeri,+ mtu wa Damasko?”  Abramu akaendelea kusema: “Hujanipa uzao wowote,*+ na mtu* wa nyumba yangu atakuwa mrithi wangu.”  Lakini tazama! Yehova akamjibu hivi: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, lakini mwana wako mwenyewe* atakuwa mrithi wako.”+  Ndipo akamtoa nje na kumwambia: “Tafadhali, tazama juu mbinguni uzihesabu nyota, ikiwa unaweza kuzihesabu.” Kisha akamwambia: “Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”*+  Naye akawa na imani katika Yehova,+ Naye akamhesabu kuwa mwadilifu.*+  Pia akasema hivi: “Mimi ni Yehova, niliyekutoa katika jiji la Uru la Wakaldayo ili nikupe nchi hii iwe miliki yako.”+  Ndipo Abramu akauliza: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, nitajuaje kwamba nitaimiliki?”  Mungu akamjibu: “Chukua kwa ajili yangu ndama jike wa miaka mitatu, mbuzi jike wa miaka mitatu, kondoo dume wa miaka mitatu, njiwa tetere, na njiwa mchanga.” 10  Basi akawachukua wote hao na kuwakata vipande viwili na kuweka kila kipande kando ya kipande cha pili,* lakini hakuwakata ndege. 11  Kisha ndege wawindaji wakaanza kushuka juu ya mizoga hiyo, lakini Abramu akawa akiwafukuza. 12  Jua lilipokaribia kutua, usingizi mzito ukamshika Abramu na giza zito lenye kuogopesha likamfunika. 13  Kisha Mungu akamwambia Abramu: “Ujue kwa hakika kwamba wazao* wako watakuwa wageni katika nchi ambayo si yao na kwamba watu wa nchi hiyo watawafanya kuwa watumwa na kuwatesa kwa miaka 400.+ 14  Lakini mimi nitalihukumu taifa watakalolitumikia,+ na baada ya hapo watatoka huko na mali nyingi.+ 15  Lakini wewe, utaenda kwa mababu zako kwa amani; utazikwa baada ya kuishi maisha marefu.+ 16  Lakini wazao wako watarudi hapa+ katika kizazi cha nne, kwa sababu uovu wa Waamori bado haujafikia kipimo chake kamili.”+ 17  Jua lilipotua na giza zito kuingia, tanuru linalofuka moshi lilitokea, na mwenge wa moto ukapita katikati ya vile vipande vya nyama. 18  Siku hiyo Yehova alifanya agano+ pamoja na Abramu, akisema: “Nitaupa uzao wako* nchi hii,+ kuanzia mto wa Misri mpaka kwenye ule mto mkubwa, mto Efrati:+ 19  nchi ya Wakeni,+ Wakenizi, Wakadmoni, 20  Wahiti,+ Waperizi,+ Warefaimu,+ 21  Waamori, Wakanaani, Wagirgashi, na Wayebusi.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mbegu yoyote.”
Tnn., “mwana.”
Tnn., “yule anayetoka katika sehemu zako za ndani.”
Tnn., “itakavyokuwa mbegu yako.”
Au “akamhesabia uadilifu.”
Au “na kuweka kila kipande ili kilingane na cha pili.”
Tnn., “mbegu.”
Tnn., “Nitaipa mbegu yako.”