Mwanzo 20:1-18

  • Sara aokolewa kutoka mikononi mwa Abimeleki (1-18)

20  Sasa Abrahamu akaihamisha kambi yake kutoka huko+ na kwenda katika nchi ya Negebu, akaanza kuishi kati ya Kadeshi+ na Shuri.+ Alipokuwa akiishi* Gerari,+  Abrahamu akasema tena kumhusu Sara mke wake: “Huyu ni dada yangu.”+ Kwa hiyo Abimeleki mfalme wa Gerari akaagiza Sara aletwe, naye akamchukua.+  Baadaye, Mungu akamjia Abimeleki katika ndoto usiku na kumwambia: “Wewe ni kama mtu aliyekufa kwa sababu ya mwanamke huyu uliyemchukua,+ kwa maana ameolewa naye ni mke wa mwanamume mwingine.”+  Hata hivyo, Abimeleki hakuwa amemkaribia.* Kwa hiyo akasema: “Yehova, je, utaliua taifa ambalo kwa kweli halina hatia?*  Je, yeye hakuniambia, ‘Huyu ni dada yangu,’ na mwanamke huyu pia hakuniambia, ‘Huyu ni ndugu yangu’? Nilifanya jambo hili kwa moyo mnyoofu na mikono isiyo na hatia.”  Kisha Mungu wa kweli akamwambia katika ndoto: “Ninajua kwamba ulifanya jambo hili kwa moyo mnyoofu, kwa hiyo nilikuzuia usinitendee dhambi. Ndiyo sababu sikukuruhusu umguse.  Sasa mrudishe mke wa mwanamume huyo, kwa maana mwanamume huyo ni nabii,+ atakuombea dua,+ nawe utaendelea kuishi. Lakini usipomrudisha, ujue kwamba kwa hakika utakufa, wewe na watu wako wote.”  Abimeleki akaamka asubuhi na mapema akawaita watumishi wake wote na kuwaambia mambo hayo yote, nao wakaogopa sana.  Kisha Abimeleki akamwita Abrahamu na kumwambia: “Ni jambo gani hili ulilotutendea? Nimekutendea dhambi gani hivi kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi kubwa hivi? Jambo ulilonitendea si sawa.” 10  Na Abimeleki akaendelea kumwambia Abrahamu: “Ulikuwa na nia gani ulipofanya jambo hili?”+ 11  Abrahamu akasema: “Ni kwa sababu nilisema moyoni mwangu, ‘Hakika watu wa mahali hapa hawamwogopi Mungu, nao wataniua kwa sababu ya mke wangu.’+ 12  Na isitoshe, kwa kweli huyu ni dada yangu, binti ya baba yangu lakini si binti ya mama yangu, naye akawa mke wangu.+ 13  Kwa hiyo Mungu aliponifanya nitangetange kutoka katika nyumba ya baba yangu,+ nilimwambia mke wangu: ‘Hivi ndivyo utakavyonionyesha upendo mshikamanifu: Kila mahali tutakapokwenda, sema hivi kunihusu, “Huyu ni ndugu yangu.”’”+ 14  Basi Abimeleki akachukua kondoo na ng’ombe na watumishi wa kiume na wa kike akampa Abrahamu, naye akamrudishia Abrahamu mke wake, Sara. 15  Pia Abimeleki akasema: “Tazama nchi yangu iko wazi mbele yako. Ishi popote unapopenda.” 16  Naye akamwambia Sara: “Tazama ninampa ndugu yako vipande 1,000 vya fedha.+ Ni ishara ya kwamba huna hatia* mbele ya wote walio pamoja nawe na mbele ya watu wote, nawe umeondolewa shutuma.” 17  Na Abrahamu akaanza kumwomba dua Mungu wa kweli, naye Mungu akamponya Abimeleki na mke wake na vijakazi wake, nao wakaanza kuzaa watoto; 18  kwa maana Yehova alikuwa amewafanya wanawake wote wa nyumba ya Abimeleki wawe tasa* kwa sababu ya Sara, mke wa Abrahamu.+

Maelezo ya Chini

Au “akiishi akiwa mgeni.”
Au “ni adilifu.”
Yaani, hakuwa amefanya naye ngono.
Tnn., “Tazama, ni kifuniko cha macho kwako.”
Au “alikuwa amefunga kabisa kila tumbo la uzazi la nyumba ya Abimeleki.”