Mwanzo 36:1-43

  • Wazao wa Esau (1-30)

  • Wafalme na mashehe wa Edomu (31-43)

36  Hii ndiyo historia ya Esau, yaani, Edomu.+  Esau alioa mabinti wa Kanaani: Ada+ binti ya Eloni Mhiti;+ na Oholibama+ binti ya Ana, mjukuu wa Sibeoni Mhivi;  na Basemathi,+ binti ya Ishmaeli, dada ya Nebayothi.+  Na Ada akamzalia Esau mtoto aliyeitwa Elifazi, naye Basemathi akamzaa Reueli,  na Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora.+ Hao ndio wana wa Esau waliozaliwa katika nchi ya Kanaani.  Kisha Esau akawachukua wake zake, wanawe, mabinti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo yake na wanyama wake wote, na mali yote aliyokusanya+ katika nchi ya Kanaani, akahamia nchi nyingine, umbali fulani kutoka kwa Yakobo ndugu yake.+  Alihama kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana wasiweze kuishi pamoja, na nchi walimoishi* haingewatosha kwa sababu walikuwa na mifugo mingi.  Kwa hiyo Esau akahamia eneo lenye milima la Seiri.+ Esau ndiye Edomu.+  Na hii ndiyo historia ya Esau, baba ya Waedomu walioishi katika eneo lenye milima la Seiri.+ 10  Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mke wa Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mke wa Esau.+ 11  Wana wa Elifazi walikuwa Temani,+ Omari, Sefo, Gatamu, na Kenasi.+ 12  Timna akawa suria wa Elifazi, mwana wa Esau. Baada ya muda akamzalia Elifazi mtoto aliyeitwa Amaleki.+ Hao ndio wana wa Ada, mke wa Esau. 13  Hawa ndio wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shamma, na Miza. Hao ndio waliokuwa wana wa Basemathi,+ mke wa Esau. 14  Hawa ndio waliokuwa wana wa Oholibama binti ya Ana, mjukuu wa Sibeoni, mke wa Esau, aliomzalia Esau: Yeushi, Yalamu, na Kora. 15  Hawa ndio mashehe* wa wana wa Esau:+ Wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Shehe Temani, Shehe Omari, Shehe Sefo, Shehe Kenasi,+ 16  Shehe Kora, Shehe Gatamu, na Shehe Amaleki. Hao ndio mashehe wa Elifazi+ katika nchi ya Edomu. Hao ndio wana wa Ada. 17  Hawa ndio wana wa Reueli, mwana wa Esau: Shehe Nahathi, Shehe Zera, Shehe Shamma, na Shehe Miza. Hao ndio mashehe wa Reueli katika nchi ya Edomu.+ Hao ndio wana wa Basemathi, mke wa Esau. 18  Hatimaye hawa ndio wana wa Oholibama, mke wa Esau: Shehe Yeushi, Shehe Yalamu, na Shehe Kora. Hao ndio mashehe wa Oholibama binti ya Ana, mke wa Esau. 19  Hao ndio wana wa Esau, na hao ndio mashehe wao. Esau ndiye Edomu.+ 20  Hawa ndio wana wa Seiri, Mhori, wakaaji wa nchi:+ Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana,+ 21  Dishoni, Ezeri, na Dishani.+ Hao ndio mashehe wa Wahori, wana wa Seiri, katika nchi ya Edomu. 22  Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemamu, naye dada ya Lotani alikuwa Timna.+ 23  Hawa ndio wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu. 24  Hawa ndio wana wa Sibeoni:+ Aya na Ana. Huyu ndiye Ana aliyepata chemchemi za maji ya moto nyikani alipokuwa akiwachunga punda wa Sibeoni baba yake. 25  Hawa ndio watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama binti ya Ana. 26  Hawa ndio wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.+ 27  Hawa ndio wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani. 28  Hawa ndio wana wa Dishani: Usi na Arani.+ 29  Hawa ndio mashehe wa Wahori: Shehe Lotani, Shehe Shobali, Shehe Sibeoni, Shehe Ana, 30  Shehe Dishoni, Shehe Ezeri, na Shehe Dishani.+ Hao ndio mashehe wa Wahori, kila shehe katika nchi ya Seiri. 31  Sasa hawa ndio wafalme waliotawala katika nchi ya Edomu+ kabla mfalme yeyote hajawatawala Waisraeli.*+ 32  Bela mwana wa Beori alitawala Edomu, na jiji lake liliitwa Dinhaba. 33  Bela alipokufa, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akaanza kutawala baada yake. 34  Yobabu alipokufa, Hushamu kutoka katika nchi ya Watemani akaanza kutawala baada yake. 35  Hushamu alipokufa, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani+ katika eneo* la Moabu akaanza kutawala baada yake, na jiji lake liliitwa Avithi. 36  Hadadi alipokufa, Samla kutoka Masreka akaanza kutawala baada yake. 37  Samla alipokufa, Shauli kutoka Rehobothi karibu na ule Mto akaanza kutawala baada yake. 38  Shauli alipokufa, Baal-hanani mwana wa Akbori akaanza kutawala baada yake. 39  Baal-hanani mwana wa Akbori alipokufa, Hadari akaanza kutawala baada yake. Jiji lake liliitwa Pau, na mke wake aliitwa Mehetabeli binti ya Matredi binti ya Mezahabu. 40  Basi haya ndiyo majina ya mashehe wa Esau kulingana na koo zao, kulingana na maeneo yao, kulingana na majina yao: Shehe Timna, Shehe Alva, Shehe Yethethi,+ 41  Shehe Oholibama, Shehe Ela, Shehe Pinoni, 42  Shehe Kenasi, Shehe Temani, Shehe Mibsari, 43  Shehe Magdieli, na Shehe Iramu. Hao ndio mashehe wa Edomu kulingana na sehemu walizoishi katika nchi waliyomiliki.+ Hao ndio wazao wa Esau, baba ya Waedomu.+

Maelezo ya Chini

Au “walimoishi wakiwa wageni.”
Shehe alikuwa mkuu wa kabila.
Tnn., “wana wa Israeli.”
Tnn., “shamba.”