Mwanzo 42:1-38

  • Ndugu za Yosefu waenda Misri (1-4)

  • Yosefu akutana na ndugu zake na kuwajaribu (5-25)

  • Ndugu zake warudi nyumbani kwa Yakobo (26-38)

42  Yakobo aliposikia kwamba kuna nafaka nchini Misri,+ akawauliza wanawe: “Kwa nini mnatazamana tu?”  Kisha akawaambia: “Nimesikia kwamba kuna nafaka nchini Misri. Shukeni huko mkatununulie nafaka, ili tuendelee kuishi tusije tukafa.”+  Basi ndugu kumi wa Yosefu+ wakashuka Misri kununua nafaka.  Lakini Yakobo hakumruhusu Benjamini,+ ndugu ya Yosefu, aende pamoja na ndugu zake, kwa sababu alisema: “Huenda akapatwa na madhara na kufa.”+  Kwa hiyo wana wa Israeli wakafika Misri pamoja na watu wengine walioenda kununua nafaka, kwa sababu njaa hiyo kali ilikuwa imeenea mpaka katika nchi ya Kanaani.+  Yosefu ndiye aliyekuwa msimamizi nchini Misri,+ na ndiye aliyewauzia nafaka watu wote duniani.+ Kwa hiyo ndugu za Yosefu wakaja na kumwinamia kifudifudi.+  Yosefu alipowaona ndugu zake, aliwatambua mara moja, lakini hakujitambulisha kwao.+ Basi akawauliza kwa ukali: “Mmetoka wapi?” wakamjibu: “Katika nchi ya Kanaani, tumekuja kununua chakula.”+  Basi Yosefu akawatambua ndugu zake, lakini wao hawakumtambua.  Mara moja Yosefu akakumbuka ndoto alizoota kuwahusu,+ akawaambia: “Ninyi ni wapelelezi! Mmekuja kuchunguza udhaifu wa nchi yetu!” 10  Wakamwambia: “Hapana, bwana wetu, sisi watumishi wako tumekuja kununua chakula. 11  Sisi sote ni wana wa mtu mmoja. Nasi ni wanyoofu. Sisi watumishi wako si wapelelezi.” 12  Lakini akawaambia: “Sivyo! Mmekuja kuchunguza udhaifu wa nchi yetu!” 13  Ndipo wakamwambia: “Sisi watumishi wako, ni ndugu 12.+ Sisi ni wana wa mtu mmoja+ anayeishi nchini Kanaani, na ndugu yetu mdogo amebaki na baba yetu,+ lakini mwingine hayupo tena.”+ 14  Hata hivyo, Yosefu akawaambia: “Ni kama tu nilivyowaambia—‘Ninyi ni wapelelezi!’ 15  Hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Kwa hakika kama Farao anavyoishi, hamtatoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo atakapokuja.+ 16  Mtumeni mmoja wenu akamlete ndugu yenu, lakini ninyi wengine mtatiwa kifungoni. Kwa njia hiyo, maneno yenu yatajaribiwa ili ijulikane ikiwa mnasema ukweli. Na kama sivyo, basi, kwa hakika kama Farao anavyoishi, ninyi ni wapelelezi.” 17  Ndipo akawatia kifungoni kwa siku tatu. 18  Siku ya tatu, Yosefu akawaambia: “Fanyeni hili ili mwendelee kuishi, kwa sababu ninamwogopa Mungu. 19  Ikiwa ninyi ni wanyoofu, acheni ndugu yenu mmoja abaki katika nyumba ambamo mmefungiwa, lakini ninyi wengine mnaweza kwenda kuchukua nafaka ili mpunguze makali ya njaa katika nyumba zenu.+ 20  Kisha mleteni kwangu ndugu yenu mdogo, ili maneno yenu yathibitike kuwa ya kweli, nanyi hamtakufa.” Basi wakafanya hivyo. 21  Wakaambiana: “Bila shaka tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu,+ kwa sababu tuliyaona mateso yake alipotusihi tumhurumie, lakini hatukumsikiliza. Ndiyo sababu tunateseka hivi.” 22  Kisha Rubeni akawaambia: “Je, sikuwaambia, ‘Msimdhuru mtoto,’* lakini hamkunisikiliza?+ Sasa kwa hakika tunadaiwa damu yake.”+ 23  Lakini hawakujua kwamba Yosefu alielewa mambo waliyokuwa wakisema, kwa sababu aliongea nao kupitia mkalimani. 24  Basi akaenda mbali nao na kuanza kulia.+ Aliporudi na kuzungumza nao, alimchukua Simeoni+ kutoka kati yao na kumfunga mbele ya macho yao.+ 25  Kisha Yosefu akaamuru mifuko yao ijazwe nafaka, na pesa za kila mmoja wao zirudishwe ndani ya gunia lake na pia wapewe vyakula kwa ajili ya safari. Ndivyo walivyofanyiwa. 26  Basi wakawatwika punda wao nafaka na kuondoka. 27  Walipofika mahali pa kulala, mmoja wao alifungua gunia lake ili amlishe punda wake, akaona pesa kwenye mdomo wa mfuko wake. 28  Akawaambia ndugu zake: “Pesa zangu zimerudishwa, ndizo hizi hapa kwenye mfuko wangu!” Wakashuka moyo, wakaanza kutetemeka na kuulizana: “Ni jambo gani hili ambalo Mungu ametutendea?” 29  Walipofika kwa Yakobo baba yao katika nchi ya Kanaani, wakamwambia mambo yote yaliyowapata, wakisema: 30  “Bwana mkubwa wa nchi hiyo alizungumza nasi kwa ukali+ na kudai kwamba tunaipeleleza nchi yao. 31  Lakini tukamwambia, ‘Sisi ni watu wanyoofu. Sisi si wapelelezi.+ 32  Sisi ni ndugu 12,+ wana wa baba mmoja. Mmoja wetu hayupo,+ na yule mdogo amebaki na baba yetu katika nchi ya Kanaani.’+ 33  Lakini bwana huyo akatuambia, ‘Hivi ndivyo nitakavyojua kwamba ninyi ni wanyoofu: Mwacheni ndugu yenu mmoja abaki nami.+ Kisha chukueni chakula mwende mkapunguze makali ya njaa ya watu wa nyumbani mwenu.+ 34  Mleteni kwangu ndugu yenu mdogo, ili nijue kwamba ninyi si wapelelezi bali ni watu wanyoofu. Kisha nitamrudisha ndugu yenu, nanyi mnaweza kufanya biashara katika nchi hii.’” 35  Walipokuwa wakimwaga nafaka kutoka katika magunia yao, kila mmoja wao alipata mfuko wake wa pesa katika gunia lake. Wote pamoja na baba yao walipoona mifuko yao ya pesa, wakaogopa. 36  Yakobo baba yao akashtuka na kusema: “Mmefanya nifiwe!+ Yosefu hayupo,+ Simeoni naye hayupo,+ na sasa mnataka kumchukua Benjamini! Mambo hayo yote yamenijia mimi!” 37  Lakini Rubeni akamwambia baba yake: “Unaweza kuwaua wanangu wawili nisipomrudisha kwako.+ Mweke chini ya uangalizi wangu, nami nitamrudisha kwako.”+ 38  Lakini Yakobo akasema: “Mwanangu hatashuka huko pamoja nanyi, kwa sababu ndugu yake amekufa, naye amebaki peke yake.+ Akipatwa na madhara na kufia njiani, basi kwa hakika mtazishusha mvi zangu Kaburini*+ kwa huzuni.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Msitende dhambi dhidi ya mtoto huyu.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.