Mwanzo 48:1-22

  • Yakobo awabariki wana wawili wa Yosefu (1-12)

  • Efraimu apata baraka kubwa zaidi (13-22)

48  Baada ya hayo, Yosefu akaambiwa: “Tazama, baba yako anadhoofika.” Basi akawachukua wanawe wawili, Manase na Efraimu, na kwenda nao.+  Ndipo Yakobo akaambiwa: “Tazama, mwana wako Yosefu amekuja kukuona.” Basi Israeli akajikakamua na kuketi kitandani.  Yakobo akamwambia Yosefu: “Mungu Mweza-Yote alinitokea kule Luzi katika nchi ya Kanaani na kunibariki.+  Naye akaniambia, ‘Ninakufanya uzae, nami nitakufanya uwe na watoto wengi, nami nitakufanya uwe kusanyiko la mataifa,+ nami nitaupa uzao wako* baada yako nchi hii iwe miliki yao ya kudumu.’+  Sasa wana wako wawili uliowazaa katika nchi ya Misri kabla sijaja kwako nchini Misri ni wangu.+ Efraimu na Manase watakuwa wangu kama Rubeni na Simeoni walivyo wangu.+  Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Wataitwa kwa jina la ndugu zao katika urithi wao.+  Nilipokuwa nikitoka Padani, Raheli alikufa+ kando yangu katika nchi ya Kanaani, na bado tulikuwa na safari ndefu kabla ya kufika Efrathi.+ Kwa hiyo nikamzika huko nikiwa njiani kuelekea Efrathi, yaani, Bethlehemu.”+  Kisha Israeli akawaona wana wa Yosefu na kuuliza: “Ni nani hawa?”  Yosefu akamwambia baba yake: “Hawa ni wanangu ambao Mungu amenipa mahali hapa.”+ Yakobo akasema: “Tafadhali walete karibu nami ili niwabariki.”+ 10  Sasa macho ya Israeli yalikuwa yamedhoofika kwa sababu ya uzee, naye hangeweza kuona. Basi Yosefu akawaleta karibu naye, Yakobo akawabusu na kuwakumbatia. 11  Israeli akamwambia Yosefu: “Sikuwazia kamwe kwamba nitauona uso wako,+ lakini sasa Mungu ameniruhusu pia kuona uzao wako.”* 12  Kisha Yosefu akawaondoa kwenye magoti ya Israeli, naye akainama kifudifudi. 13  Halafu Yosefu akawachukua wote wawili na kuwaleta karibu na Yakobo; alimchukua Efraimu+ kwa mkono wake wa kulia na kumweka upande wa kushoto wa Israeli, na Manase+ kwa mkono wake wa kushoto na kumweka upande wa kulia wa Israeli. 14  Lakini Israeli akaunyoosha mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa ndiye aliyekuwa mdogo, halafu akauweka mkono wake wa kushoto juu ya kichwa cha Manase. Aliweka mikono yake hivyo kimakusudi kwa sababu Manase alikuwa mzaliwa wa kwanza.+ 15  Kisha akambariki Yosefu na kusema:+ “Mungu wa kweli ambaye baba zangu Isaka na Abrahamu walitembea mbele zake,+Mungu wa kweli ambaye amekuwa akinichunga maisha yangu yote mpaka leo,+ 16  Malaika ambaye amekuwa akiniponya katika misiba yote,+ awabariki wavulana hawa.+ Na waitwe kwa jina langu na jina la baba zangu, Abrahamu na Isaka,Acha waongezeke na kuwa umati mkubwa duniani.”+ 17  Yosefu hakufurahi alipoona baba yake ameuweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efraimu, basi akashika mkono wa baba yake na kujaribu kuuondoa juu ya kichwa cha Efraimu ili auweke juu ya kichwa cha Manase. 18  Yosefu akamwambia baba yake: “Sivyo baba yangu, kwa kuwa huyu ndiye mzaliwa wa kwanza.+ Weka mkono wako wa kulia juu ya kichwa chake.” 19  Lakini baba yake akazidi kukataa na kusema: “Najua, mwanangu, najua. Yeye pia atakuwa taifa, yeye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye,+ na uzao wake utalingana* kabisa na mataifa.”+ 20  Basi akaendelea kuwabariki siku hiyo,+ akisema: “Waisraeli na walitaje jina lenu wanapotangaza baraka, wakisema,‘Mungu na awafanye muwe kama Efraimu na kama Manase.’” Hivyo akaendelea kumtanguliza Efraimu mbele ya Manase. 21  Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Tazama, ninakufa, + lakini kwa hakika Mungu ataendelea kuwa pamoja nanyi na kuwarudisha katika nchi ya mababu zenu.+ 22  Mimi ninakupa sehemu moja zaidi ya nchi* kuliko ndugu zako, ambayo nilichukua kutoka mikononi mwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “nitaipa mbegu yako.”
Tnn., “mbegu yako.”
Tnn., “mbegu yake italingana.”
Au “mteremko mmoja zaidi wa nchi.” Tnn., “bega moja zaidi.”