Mwanzo 8:1-22

  • Maji ya Gharika yapungua (1-14)

    • Njiwa atumwa (8-12)

  • Kutoka ndani ya safina (15-19)

  • Ahadi ya Mungu kuhusu dunia (20-22)

8  Lakini Mungu akamwelekezea uangalifu* Noa na wanyama wote wa mwituni na wanyama wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya safina,+ na Mungu akavumisha upepo duniani, maji yakaanza kupungua.  Chemchemi za kilindi cha maji na malango ya mbinguni ya mafuriko yakafungwa, kwa hiyo mvua kutoka mbinguni ikaacha kunyesha.*+  Kisha maji yakaanza kupungua hatua kwa hatua duniani. Kufikia mwishoni mwa siku 150, maji yalikuwa yamepungua sana.  Katika mwezi wa saba, siku ya 17 ya mwezi huo, safina ikatua kwenye milima ya Ararati.  Na maji yakazidi kupungua hatua kwa hatua mpaka mwezi wa kumi. Katika mwezi wa kumi, siku ya kwanza ya mwezi huo, vilele vya milima vikaonekana.+  Basi mwishoni mwa siku 40, Noa akafungua dirisha+ la safina alilokuwa ametengeneza  na kumtuma nje kunguru; kunguru alikuwa akienda na kurudi, mpaka maji yalipokauka duniani.  Baadaye akamtuma njiwa ili aone ikiwa maji yalikuwa yamepungua ardhini.  Njiwa huyo hakupata mahali pa kutua,* kwa hiyo akarudi kwa Noa ndani ya safina kwa sababu maji yalikuwa bado yameifunika dunia yote.+ Kwa hiyo akaunyoosha mkono wake nje na kumwingiza ndani ya safina. 10  Noa akangojea siku saba zaidi, akamtuma tena njiwa nje ya safina. 11  Njiwa huyo alipomrudia Noa ikielekea jioni, aliona kwamba alikuwa na jani bichi la mzeituni mdomoni mwake! Basi Noa akajua kwamba maji yalikuwa yamepungua duniani.+ 12  Akangojea tena siku nyingine saba. Kisha akamtuma nje njiwa huyo, lakini hakurudi tena. 13  Sasa katika mwaka wa 601,+ mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, maji yalikuwa yamepungua duniani; Noa akaondoa kifuniko cha safina na kuona kwamba ardhi ilikuwa ikikauka. 14  Katika mwezi wa pili, siku ya 27 ya mwezi huo, dunia ilikuwa imekauka. 15  Sasa Mungu akamwambia Noa: 16  “Toka ndani ya safina, wewe, mke wako, wanao, na wake zao.+ 17  Toka pamoja na viumbe wote walio hai wa kila aina,+ viumbe wanaoruka, wanyama, na wanyama wote wanaotambaa, ili wazaane* duniani na kuongezeka na kuwa wengi duniani.”+ 18  Basi Noa akatoka nje, pamoja na wanawe,+ mke wake, na wake wa wanawe. 19  Kila kiumbe aliye hai, kila mnyama anayetambaa na kila kiumbe anayeruka, kila kiumbe anayetembea duniani, akatoka ndani ya safina kulingana na familia yake.+ 20  Kisha Noa akamjengea Yehova madhabahu,+ akachukua baadhi ya wanyama walio safi na baadhi ya viumbe wanaoruka walio safi,+ akawatoa kuwa dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu+ hiyo. 21  Na Yehova akaanza kusikia harufu ya kupendeza.* Kwa hiyo Yehova akasema moyoni mwake: “Sitailaani ardhi+ tena kwa sababu ya mwanadamu, kwa maana mwelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mbaya tangu wakati wa ujana;+ nami sitamwangamiza tena kamwe kila kiumbe aliye hai kama nilivyofanya.+ 22  Kuanzia sasa na kuendelea, dunia haitakosa kamwe kuwa na majira ya kupanda mbegu na kuvuna, baridi na joto, kiangazi na masika, na mchana na usiku.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “akamkumbuka.”
Au “ikazuiliwa.”
Au “mahali pa kutua kwa ajili ya wayo wa mguu wake.”
Au “wajae.”
Au “inayotuliza.”