Nahumu 1:1-15

  • Mungu awalipiza kisasi maadui wake (1-7)

    • Mungu anataka watu wamwabudu yeye peke yake (2)

    • Yehova huwajali wanaomkimbilia (7)

  • Ninawi kuangamizwa (8-14)

    • Taabu haitatokea mara ya pili (9)

  • Taifa la Yuda latangaziwa habari njema (15)

1  Tangazo dhidi ya Ninawi:+ Kitabu cha maono ya Nahumu* Mwelkoshi:   Yehova ni Mungu anayetaka watu wamwabudu yeye peke yake+ naye hulipiza kisasi;Yehova hulipiza kisasi naye yuko tayari kuonyesha ghadhabu yake.+ Yehova hulipiza kisasi dhidi ya maadui wake,Naye hukusanya ghadhabu kwa ajili ya maadui wake.   Yehova si mwepesi wa hasira,+ naye ana nguvu nyingi,+Lakini Yehova hatasita kamwe kutoa adhabu inayostahiliwa.+ Kijia chake kimo katika upepo unaosababisha uharibifu na katika dhoruba,Na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.+   Hukemea bahari,+ naye huikausha;Naye huifanya mito yote ikauke.+ Bashani na Karmeli hunyauka,+Na maua ya Lebanoni hunyauka.   Milima hutetemeka kwa sababu yake,Na vilima huyeyuka.+ Dunia itasukasuka kwa sababu ya uso wake,Pamoja na nchi na wote wanaoishi humo.+   Ni nani anayeweza kusimama mbele ya hasira yake kali?+ Na ni nani anayeweza kustahimili joto la hasira yake?+ Ghadhabu yake itamwagwa kama moto,Na miamba itavunjika-vunjika kwa sababu yake.   Yehova ni mwema,+ ni ngome katika siku ya taabu.+ Anawakazia fikira* wale wanaotafuta kimbilio kwake.+   Kwa mafuriko makubwa atapaangamiza kabisa mahali pake,*Na giza litawafuatia maadui wake.   Mtapanga njama gani dhidi ya Yehova? Anasababisha maangamizi kamili. Taabu haitatokea tena mara ya pili.+ 10  Kwa maana wamesokotana kama miiba,Nao ni kama watu waliolewa pombe;*Lakini watateketezwa kabisa kama nyasi kavu. 11  Kutoka kwako atatoka yule anayepanga njama ya uovu dhidi ya Yehova,Akitoa ushauri usiofaa. 12  Yehova anasema hivi: “Ingawa walikuwa na nguvu nyingi na walikuwa wengi,Hata hivyo, wataangamizwa na kutoweka.* Nimekutesa wewe,* lakini sitakutesa tena. 13  Na sasa nitavunja nira yake na kuiondoa juu yako,+Nami nitazikata pingu zako vipande viwili. 14  Yehova ameamuru hivi kukuhusu,*‘Jina lako halitaendelezwa tena. Nitaziharibu sanamu zako za kuchongwa na sanamu za chuma* kutoka katika nyumba ya* miungu yako. Nitakuchimbia kaburi, kwa sababu unachukiza.’ 15  “Tazama! Miguu ya yule anayeleta habari njema iko milimani,Yule anayetangaza amani.+ Fanya sherehe zako,+ Ee Yuda, timiza nadhiri zako,Kwa maana mtu asiyefaa hatapita tena kati yako. Ataangamizwa kabisa.”

Maelezo ya Chini

Maana yake “Mfariji.”
Au “Anawatunza.” Tnn., “Anawajua.”
Yaani, Ninawi.
Au “pombe ya ngano.”
Au labda, “naye atapita katikati yake.”
Yaani, watu wa Yuda.
Yaani, Ashuru.
Au “sanamu za kuyeyushwa.”
Au “hekalu la.”