Nahumu 2:1-13

  • Ninawi kuangamizwa (1-13)

    • “Malango ya mto yatafunguliwa” (6)

2  Yule anayetawanya amekuvamia.*+ Linda ngome. Linda njia. Jitayarisheni* na mkusanye nguvu zenu zote.   Kwa maana Yehova atarudisha fahari ya Yakobo,Pamoja na fahari ya Israeli,Kwa sababu waangamizaji wamewaangamiza;+Nao wameharibu machipukizi yao.   Ngao za wanaume wake hodari zimetiwa rangi nyekundu,Mashujaa wake wamevaa nguo nyekundu. Vyuma vya magari yake ya vita vinawakawaka kama motoKatika siku anayojitayarisha kwa ajili ya vita,Na mikuki ya miberoshi inapotikiswa.   Magari ya vita yanaendeshwa kwa kasi sana barabarani. Yanakimbia huku na huku katika viwanja vya mji. Yanang’aa kama mienge inayowaka na kumweka kama radi.   Atawaita maofisa wake. Watajikwaa wanaposonga mbele. Wanakimbilia haraka kwenye ukuta wake;Wanaweka kizuizi.   Malango ya mto yatafunguliwa,Na jumba la mfalme litayeyushwa.*   Imeamriwa:* Amefunuliwa,Amechukuliwa, na vijakazi wake wanalia kwa huzuni;Wanalia kama njiwa huku wakijipigapiga vifua.*   Katika siku zake zote jiji la Ninawi+ lilikuwa kama dimbwi la maji,Lakini sasa wanakimbia. “Simameni tuli! Simameni tuli!” Lakini hakuna yeyote anayegeuka nyuma.+   Poreni fedha, poreni dhahabu! Hazina zake haziishi. Zimejazwa kila aina ya vitu vyenye thamani. 10  Jiji liko tupu, liko ukiwa, na limeharibiwa kabisa!+ Mioyo yao inayeyuka kwa woga, magoti yao yanalegea, viuno vyao vinatetemeka;Nyuso zao zote zimebadilika rangi. 11  Liko wapi pango la simba,+ mahali ambapo wanasimba* wanakula,Mahali ambapo simba anatoka akimwongoza mtoto wake,Na hakuna yeyote wa kuwaogopesha? 12  Simba aliwararulia watoto wake mawindo ya kutosha,Akayakaba pumzi mawindo kwa ajili ya majike yake. Alijaza mawindo katika mapango yake,Makao yake akayajaza wanyama walioraruliwa. 13  “Tazama! Niko dhidi yako,” asema Yehova wa majeshi,+“Nitayateketeza kwa moto magari yake ya vita,+Na upanga utawachinja wanasimba wako.* Nitayaangamiza kabisa mawindo yako duniani,Na sauti ya wajumbe wako haitasikika tena.”+

Maelezo ya Chini

Yaani, Ninawi.
Tnn., “Imarisheni viuno.”
Au “litaporomoka.”
Au “Imeagizwa.”
Tnn., “mioyo.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “wanasimba wako wenye manyoya marefu shingoni.”