Nehemia 1:1-11

  • Habari kutoka Yerusalemu (1-3)

  • Sala ya Nehemia (4-11)

1  Maneno ya Nehemia*+ mwana wa Hakalia: Sasa katika mwezi wa Kislevu,* mwaka wa 20, mimi nilikuwa katika ngome ya* Shushani.*+  Wakati huo Hanani,+ mmoja wa ndugu zangu, akaja pamoja na watu wengine kutoka Yuda, nami nikawauliza kuhusu Wayahudi waliobaki walioponyoka kutoka utekwani,+ na pia kuhusu Yerusalemu.  Wakanijibu: “Wale waliobaki na kuponyoka utekwani ambao wamebaki katika mkoa* ule wako katika hali mbaya sana na yenye kuaibisha.+ Kuta za Yerusalemu zimebomolewa,+ na malango yake yameteketezwa kwa moto.”+  Mara tu niliposikia maneno hayo, nikaketi chini na kuanza kulia na kuomboleza kwa siku nyingi, nami nikaendelea kufunga+ na kusali mbele za Mungu wa mbinguni.  Nikasema: “Ee Yehova, Mungu wa mbinguni, Mungu mkuu na mwenye kuogopesha, unayeshika agano lako na kuwatendea kwa upendo mshikamanifu wale wanaokupenda na kushika amri zako,+  tafadhali, tega sikio lako na ufungue macho yako ili usikilize sala ambayo mimi mtumishi wako ninakutolea leo, mchana na usiku,+ kuhusu watumishi wako Waisraeli, nikiungama dhambi ambazo watu wa Israeli wamekutendea. Tumetenda dhambi, mimi pamoja na nyumba ya baba yangu.+  Kwa hakika tumetenda mambo mapotovu dhidi yako+ kwa kuwa hatukushika amri, masharti, na sheria ulizompa* mtumishi wako Musa.+  “Tafadhali, kumbuka neno ulilomwamuru* Musa mtumishi wako, ukisema: ‘Msipotenda kwa uaminifu, nitawatawanya miongoni mwa mataifa.+  Lakini mkinirudia na kuzishika amri zangu na kuzitii, hata ingawa mtakuwa mmetawanyika mpaka kwenye mwisho wa mbingu, nitawakusanya+ na kuwaleta mahali ambapo nimepachagua ili jina langu likae hapo.’+ 10  Wao ni watumishi wako na watu wako, uliowakomboa kwa uwezo wako mkubwa na kwa mkono wako wenye nguvu.+ 11  Ee Yehova, tafadhali, tega sikio lako usikilize sala yangu mimi mtumishi wako na sala ya watumishi wako wanaofurahia kulihofu jina lako, na tafadhali, nipe mimi mtumishi wako mafanikio leo, ili mtu huyu anihurumie.”+ Basi mimi nilikuwa msimamizi wa vinywaji vya mfalme.+

Maelezo ya Chini

Maana yake “Yah Hufariji.”
Au “jumba la mfalme la.”
Au “Susa.”
Au “wilaya ya utawala.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu uliyomwagiza.”
Au “onyo ulilompa.”