Nehemia 10:1-39

  • Watu wakubali kuifuata Sheria (1-39)

    • “Hatutaipuuza nyumba ya Mungu wetu” (39)

10  Wale walioyathibitisha kwa kutia muhuri+ walikuwa: Gavana* Nehemia, mwana wa Hakalia, Na Sedekia,  Seraya, Azaria, Yeremia,  Pashuri, Amaria, Malkiya,  Hatushi, Shebania, Maluku,  Harimu,+ Meremothi, Obadia,  Danieli,+ Ginethoni, Baruku,  Meshulamu, Abiya, Miyamini,  Maazia, Bilgai, na Shemaya; hao ndio makuhani.  Pia Walawi: Yeshua mwana wa Azania, Binui wa wana wa Henadadi, Kadmieli,+ 10  na ndugu zao Shebania, Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani, 11  Mika, Rehobu, Hashabia, 12  Zakuri, Sherebia,+ Shebania, 13  Hodia, Bani, na Beninu. 14  Viongozi wa watu: Paroshi, Pahath-moabu,+ Elamu, Zatu, Bani, 15  Buni, Azgadi, Bebai, 16  Adoniya, Bigvai, Adini, 17  Ateri, Hezekia, Azuri, 18  Hodia, Hashumu, Besai, 19  Harifu, Anathothi, Nebai, 20  Magpiashi, Meshulamu, Heziri, 21  Meshezabeli, Sadoki, Yadua, 22  Pelatia, Hanani, Anaya, 23  Hoshea, Hanania, Hashubu, 24  Haloheshi, Pilha, Shobeki, 25  Rehumu, Hashabna, Maaseya, 26  Ahiya, Hanani, Anani, 27  Maluku, Harimu, na Baana. 28  Watu wengine wote—makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji, watumishi wa hekaluni,* kila mtu aliyejitenga na mataifa yaliyokuwa nchini ili afuate Sheria ya Mungu wa kweli,+ pamoja na wake zao, wana wao, na mabinti wao, kila mtu mwenye ujuzi na uelewaji* 29  wakajiunga na ndugu zao, wakuu wao, wakajifunga kwa kiapo na laana, kwamba watatembea katika Sheria ya Mungu wa kweli, iliyotolewa kupitia Musa mtumishi wa Mungu wa kweli, na kufuata kwa makini amri zote za Yehova Bwana wetu, hukumu zake, na masharti yake. 30  Hatutakubali mabinti wetu waolewe na watu wa mataifa yaliyo nchini, wala hatutakubali wana wetu wawaoe mabinti wao.+ 31  Ikiwa watu wa mataifa hayo wataleta bidhaa zao na kila aina ya nafaka ili watuuzie katika siku ya Sabato, hatutanunua chochote kutoka kwao siku ya Sabato+ au siku nyingine takatifu.+ Pia, mwaka wa saba+ hatutalima mashamba na tutayafuta madeni yote.+ 32  Pia, tukajiwekea wajibu kwamba kila mmoja wetu atoe sehemu ya tatu ya shekeli* kila mwaka kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya* Mungu wetu,+ 33  kwa ajili ya mkate wa tabaka,*+ toleo la nafaka la kila siku,+ dhabihu za kawaida za kuteketezwa za Sabato+ na miezi mipya,+ na kwa ajili ya sherehe rasmi,+ kwa ajili ya vitu vitakatifu, kwa ajili ya dhabihu za dhambi+ ili kufunika dhambi za Waisraeli, na kwa ajili ya kazi zote za nyumba ya Mungu wetu. 34  Pia, tukapiga kura ili kupanga wakati ambao kila ukoo* wa makuhani, Walawi, na watu wangeleta kuni kwenye nyumba ya Mungu wetu wakati uliowekwa, mwaka baada ya mwaka, ili kuwasha moto kwenye madhabahu ya Yehova Mungu wetu, kama ilivyoandikwa katika Sheria.+ 35  Pia tutaleta kwenye nyumba ya Yehova mazao ya kwanza yaliyokomaa ya nchi yetu na matunda ya kwanza yaliyoiva ya kila mti wa matunda, mwaka baada ya mwaka,+ 36  vilevile tutatoa wazaliwa wetu wa kwanza wa kiume na pia wa mifugo yetu—kama ilivyoandikwa katika Sheria+—wazaliwa wetu wa kwanza wa ng’ombe na wa kondoo. Tutawaleta kwenye nyumba ya Mungu wetu, kwa makuhani wanaohudumu kwenye nyumba ya Mungu wetu.+ 37  Pia, unga wetu wa kwanza ambao haujakobolewa,+ michango yetu, matunda ya mti wa kila aina,+ divai mpya, na mafuta,+ tutawapelekea makuhani kwenye maghala* ya nyumba ya Mungu wetu,+ pia tutawapa Walawi sehemu ya kumi ya mazao ya mashamba yetu,+ kwa maana Walawi ndio wanaokusanya sehemu za kumi za mazao katika miji yetu yote ya kilimo. 38  Na kuhani, mwana wa Haruni, anapaswa kuwa pamoja na Walawi wanapokusanya sehemu ya kumi; Walawi nao wanapaswa kuleta sehemu ya kumi ya ile sehemu ya kumi katika nyumba ya Mungu wetu,+ kwenye vyumba vya* ghala. 39  Kwa maana Waisraeli na Walawi wanapaswa kuleta mchango+ wa nafaka, divai mpya, na mafuta+ kwenye maghala,* ambamo mna vyombo vya mahali patakatifu, na pia walinzi wa malango, waimbaji, na makuhani wanaohudumu. Hatutaipuuza nyumba ya Mungu wetu.+

Maelezo ya Chini

Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Au labda, “wote wenye umri wa kutosha kuelewa.”
Shekeli moja ilikuwa na uzito wa gramu 11.4. Angalia Nyongeza B14.
Au “hekalu la.”
Yaani, mkate wa wonyesho.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “majumba ya kulia chakula.”
Au “majumba ya kulia chakula ya.”
Au “majumba ya kulia chakula.”