Nehemia 7:1-73

  • Malango ya jiji na walinzi wa malango (1-4)

  • Orodha ya watu waliorudi kutoka uhamishoni (5-69)

    • Watumishi wa hekaluni (46-56)

    • Wana wa watumishi wa Sulemani (57-60)

  • Michango kwa ajili ya kazi (70-73)

7  Mara tu ukuta ulipojengwa upya+ nikaweka milango;+ kisha walinzi wa malango,+ waimbaji,+ na Walawi+ wakawekwa rasmi.  Kisha nikamweka ndugu yangu Hanani+ asimamie Yerusalemu, pamoja na Hanania mkuu wa Ngome,+ kwa maana alikuwa mwanamume mwaminifu zaidi na alimwogopa Mungu wa kweli+ kuliko watu wengine wengi.  Basi nikawaambia: “Malango ya Yerusalemu yasifunguliwe mpaka mchana kabisa, na wanapolinda wanapaswa kufunga milango na kuweka makomeo. Kisha wapange wakaaji wa Yerusalemu wawe walinzi, kila mmoja katika kituo chake cha ulinzi alichogawiwa na kila mmoja mbele ya nyumba yake.”  Sasa jiji lilikuwa kubwa na pana, na watu walikuwa wachache,+ na nyumba hazikuwa zimejengwa upya.  Lakini Mungu wangu akaweka wazo moyoni mwangu niwakusanye wakuu, watawala wasaidizi, na watu ili waandikishwe kulingana na ukoo wao.+ Kisha nikapata kitabu cha orodha za koo za wale waliokuja mwanzoni, na kilikuwa na habari zifuatazo:  Hawa ndio watu wa mkoa* waliopanda kutoka utekwani huko uhamishoni, ambao Mfalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuwa amewapeleka uhamishoni+ na ambao baadaye walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye jiji lake,+  wale waliokuja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Misperethi, Bigvai, Nehumu, na Baana. Idadi ya wanaume Waisraeli ilitia ndani:+  wana wa Paroshi, 2,172;  wana wa Shefatia, 372; 10  wana wa Ara,+ 652; 11  wana wa Pahath-moabu,+ wa wana wa Yeshua na Yoabu,+ 2,818; 12  wana wa Elamu,+ 1,254; 13  wana wa Zatu, 845; 14  wana wa Zakai, 760; 15  wana wa Binui, 648; 16  wana wa Bebai, 628; 17  wana wa Azgadi, 2,322; 18  wana wa Adonikamu, 667; 19  wana wa Bigvai, 2,067; 20  wana wa Adini, 655; 21  wana wa Ateri, wa Hezekia, 98; 22  wana wa Hashumu, 328; 23  wana wa Besai, 324; 24  wana wa Harifu, 112; 25  wana wa Gibeoni,+ 95; 26  wanaume wa Bethlehemu na Netofa, 188; 27  wanaume wa Anathothi,+ 128; 28  wanaume wa Beth-azmavethi, 42; 29  wanaume wa Kiriath-yearimu,+ Kefira, na Beerothi,+ 743; 30  wanaume wa Rama na Geba,+ 621; 31  wanaume wa Mikmasi,+ 122; 32  wanaume wa Betheli+ na Ai,+ 123; 33  wanaume wa ile Nebo nyingine, 52; 34  wana wa Elamu mwingine, 1,254; 35  wana wa Harimu, 320; 36  wana wa Yeriko, 345; 37  wana wa Lodi, Hadidi, na Ono,+ 721; 38  wana wa Senaa, 3,930. 39  Makuhani:+ wana wa Yedaya wa nyumba ya Yeshua, 973; 40  wana wa Imeri, 1,052; 41  wana wa Pashuri,+ 1,247; 42  wana wa Harimu,+ 1,017. 43  Walawi:+ Wana wa Yeshua, wa nyumba ya Kadmieli,+ wa wana wa Hodeva, 74; 44  Waimbaji:+ wana wa Asafu,+ 148. 45  Walinzi wa malango:+ wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu,+ wana wa Hatita, wana wa Shobai, 138. 46  Watumishi wa hekaluni:*+ Wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi, 47  wana wa Kerosi, wana wa Sia, wana wa Padoni, 48  wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Salmai, 49  wana wa Hanani, wana wa Gideli, wana wa Gahari, 50  wana wa Reaya, wana wa Resini, wana wa Nekoda, 51  wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea, 52  wana wa Besai, wana wa Meunimu, wana wa Nefushesimu, 53  wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri, 54  wana wa Baslithi, wana wa Mehida, wana wa Harsha, 55  wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema, 56  wana wa Nezia, wana wa Hatifa. 57  Wana wa watumishi wa Sulemani:+ wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Perida, 58  wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli, 59  wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-hazebaimu, wana wa Amoni. 60  Watumishi wote wa hekaluni*+ na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392. 61  Na hawa ndio waliopanda kutoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni, na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kama ukoo wao* na asili yao ilikuwa ya Waisraeli:+ 62  wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, 642. 63  Na kutoka kwa makuhani: wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai,+ aliyemwoa mmoja kati ya mabinti wa Barzilai Mgileadi na kuitwa kwa jina lao. 64  Hao walichunguza kumbukumbu zao ili wathibitishe ukoo wao, lakini hawakupata majina ya koo zao, kwa hiyo hawakustahili kuwa makuhani.*+ 65  Gavana*+ akawaambia kwamba hawapaswi kula vitu vitakatifu kabisa+ mpaka apatikane kuhani ambaye angechunguza Urimu na Thumimu.+ 66  Kutaniko lote lilikuwa na jumla ya watu 42,360,+ 67  mbali na watumwa wao wa kiume na wa kike,+ ambao walikuwa 7,337; walikuwa pia na waimbaji 245 wa kiume na wa kike.+ 68  Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245, 69  ngamia 435, na punda 6,720. 70  Baadhi ya viongozi wa koo* walitoa mchango kwa ajili ya kazi.+ Gavana* alitoa kwa ajili ya hazina drakma 1,000 za dhahabu,* mabakuli 50, na kanzu 530 za makuhani.+ 71  Na baadhi ya viongozi wa koo* walitoa kwa ajili ya hazina ya kazi drakma 20,000 za dhahabu na mina 2,200 za fedha.* 72  Na wale watu wengine walitoa drakma 20,000 za dhahabu, mina 2,000 za fedha, na kanzu 67 za makuhani. 73  Na makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji,+ baadhi ya watu, watumishi wa hekaluni,* na Waisraeli wengine wote wakaanza kuishi katika majiji yao.+ Kufikia mwezi wa saba,+ Waisraeli wote* walikuwa wakiishi katika majiji yao.+

Maelezo ya Chini

Au “wilaya ya utawala.”
Au “Wanethini.” Tnn., “Waliotolewa.”
Au “Wanethini wote.” Tnn., “Wote Waliotolewa.”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Au “hawakustahili utumishi wa kikuhani kwa sababu hawakuwa safi.”
Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.
Kwa kawaida ilikuwa sawa na dariki ya dhahabu ya Uajemi yenye uzito wa gramu 8.4. Si drakma inayotajwa katika Maandiko ya Kigiriki. Angalia Nyongeza B14.
Au “Tirshatha,” cheo cha Kiajemi cha gavana wa mkoa.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Mina inayotajwa katika Maandiko ya Kiebrania ilikuwa na uzito wa gramu 570. Angalia Nyongeza B14.
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Tnn., “Israeli yote.”