Obadia 1:1-21

  • Kunyenyekezwa kwa taifa la Edomu lenye kiburi (1-9)

  • Taifa la Edomu lamtendea Yakobo ukatili (10-14)

  • Siku ya Yehova ya kuhukumu mataifa yote (15, 16)

  • Kurudishwa kwa nyumba ya Yakobo (17-21)

    • Edomu kuangamizwa na Yakobo (18)

    • Ufalme utakuwa wa Yehova (21)

 Maono ya Obadia:* Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi kuhusu Edomu:+ “Tumesikia habari kutoka kwa Yehova,Mjumbe ametumwa kati ya mataifa: ‘Inukeni, tujitayarishe kupigana na Edomu.’”+   “Tazama! Nimekufanya uwe mdogo sana kati ya mataifa;Unadharauliwa kabisa.+   Kimbelembele cha moyo wako kimekudanganya,+Wewe unayeishi katika mapango ya mwamba,Unayekaa juu, ukisema moyoni mwako,‘Ni nani atakayenishusha chini duniani?’   Hata ukijenga makao yako juu* kama tai,Au ukiweka kiota chako kati ya nyota,Nitakushusha chini kutoka huko,” asema Yehova.   “Ikiwa wezi wangekuvamia, ikiwa wanyang’anyi wangekuja usiku,Je, hawangeiba tu wanachotaka? Au ikiwa wavunaji wa zabibu wangekuja kwako,Je, hawangeacha zabibu chache? Lakini wewe utaangamizwa kabisa!+   Lo! Jinsi ambavyo Esau ametafutwa! Jinsi hazina zake zilizofichwa zilivyotafutwa!   Wamekufukuza hadi mpakani. Washirika wako wote* wamekudanganya. Watu walio na amani pamoja nawe wamekushinda. Wale wanaokula mkate pamoja nawe wataweka wavu chini yako,Lakini hutatambua.   Katika siku hiyo,” asema Yehova,“Je, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu+Na wenye utambuzi walio katika eneo lenye milima la Esau?   Na mashujaa wako wataogopa,+ Ee Temani,+Kwa kuwa kila mtu aliye katika eneo lenye milima la Esau atauawa kwa upanga.+ 10  Kwa sababu ya ukatili uliomtendea ndugu yako Yakobo,+Aibu itakufunika,+Nawe utaangamia milele.+ 11  Siku uliyosimama kando,Siku ambayo wageni walichukua jeshi lake na kulipeleka utekwani,+Wageni walipoingia katika lango lake na kugawana Yerusalemu kwa kura,+Ulitenda kama wao. 12  Hupaswi kucheka siku ambayo ndugu yako anapatwa na maafa,+Hupaswi kushangilia siku ambayo watu wa Yuda wanaangamia,+Nawe hupaswi kujigamba sana siku wanayotaabika. 13  Hupaswi kuingia katika lango la watu wangu siku wanayopatwa na msiba,+Hupaswi kuwacheka siku wanayopatwa na msiba,Nawe hupaswi kuchukua mali yao siku wanayopatwa na msiba.+ 14  Hupaswi kusimama kwenye makutano ya barabara ili kuwachinja watu wake wanaokimbia,+Nawe hupaswi kuwakabidhi waokokaji kwa maadui wao siku wanayopatwa na taabu.+ 15  Kwa maana siku ya Yehova ya kuhukumu mataifa yote inakaribia.+ Kama ulivyofanya, ndivyo utakavyofanyiwa.+ Utatendewa kama ulivyowatendea wengine. 16  Kwa maana kama mlivyokunywa divai kwenye mlima wangu mtakatifu,Ndivyo mataifa yote yatakavyoendelea kunywa hasira yangu kama divai.+ Yatakunywa na kumeza hasira yangu,Nayo yatatoweka kana kwamba hayajawahi kuwepo. 17  Lakini wale watakaookoka watakuwa juu ya Mlima Sayuni,+Nao utakuwa mtakatifu;+Na nyumba ya Yakobo itamiliki mali yao.+ 18  Nyumba ya Yakobo itakuwa moto,Nyumba ya Yosefu itakuwa mwali wa moto,Na nyumba ya Esau itakuwa kama majani makavu;Watayachoma moto na kuyateketeza,Na hakuna atakayeokoka katika nyumba ya Esau,+Kwa maana Yehova mwenyewe amesema. 19  Watamiliki Negebu na eneo lenye milima la Esau,+Shefela na nchi ya Wafilisti.+ Watamiliki shamba la Efraimu na shamba la Samaria,+Na Benjamini atamiliki Gileadi. 20  Waliohamishwa kutoka katika boma hili,*+Naam, Waisraeli, watamiliki nchi ya Wakanaani mpaka Sarefathi.+ Na waliohamishwa kutoka Yerusalemu, waliokuwa Sefaradi, watamiliki majiji ya Negebu.+ 21  Na waokoaji watapanda Mlima SayuniIli kuhukumu eneo lenye milima la Esau,+Na ufalme utakuwa wa Yehova.”+

Maelezo ya Chini

Maana yake “Mtumishi wa Yehova.”
Au labda, “ukiruka juu.”
Au “Wale wote waliofanya agano pamoja nawe.”
Au “ngome hii.”