Ruthu 3:1-18

  • Naomi ampa Ruthu maagizo (1-4)

  • Ruthu na Boazi kwenye uwanja wa kupuria nafaka (5-15)

  • Ruthu arudi kwa Naomi (16-18)

3  Basi Naomi mama mkwe wake akamwambia: “Binti yangu, je, si vema nikutafutie makao*+ ili mambo yakuendee vyema?  Boazi, ambaye ulifanya kazi na wasichana wake, je, yeye si mtu wetu wa ukoo?+ Usiku wa leo anapepeta shayiri kwenye uwanja wa kupuria.  Basi oga na ujipake mafuta yenye marashi; kisha uvae vizuri na kwenda kwenye uwanja wa kupuria. Hakikisha hakuoni hadi atakapomaliza kula na kunywa.  Atakapolala, angalia mahali ambapo atalala; kisha uende ufunue miguu yake na ulale hapo. Atakwambia jambo unalopaswa kufanya.”  Basi Ruthu akasema: “Yote unayoniambia nitafanya.”  Kwa hiyo, akaenda kwenye uwanja wa kupuria na kufanya yote aliyoambiwa na mama mkwe wake.  Basi Boazi akala, akanywa, na kuchangamka moyoni. Kisha akaenda kulala mwisho wa rundo la nafaka. Kisha Ruthu akaja kimyakimya, akamfunua miguu, na kulala hapo.  Katikati ya usiku, mwanamume huyo alianza kutetemeka, akaketi na kumwona mwanamke amelala miguuni pake.  Akamuuliza: “Wewe ni nani?” Akajibu: “Mimi ni Ruthu, kijakazi wako. Nifunike mimi kijakazi wako kwa vazi lako,* kwa maana wewe ni mkombozi.”+ 10  Basi Boazi akasema: “Yehova na akubariki, binti yangu. Wakati huu, umetenda kwa upendo mshikamanifu zaidi kuliko mwanzoni,+ kwa kuwa hukuwafuata wale vijana, matajiri au maskini. 11  Na sasa binti yangu, usiogope. Nitakufanyia kila jambo utakalosema,+ kwa maana kila mtu jijini* anajua kwamba wewe ni mwanamke bora. 12  Ni kweli kwamba mimi ni mkombozi,+ lakini kuna mkombozi ambaye ni mtu wa karibu zaidi wa ukoo kuliko mimi.+ 13  Kaa hapa usiku wa leo, na ikiwa atakukomboa asubuhi, ni sawa! Na akukomboe.+ Lakini ikiwa hataki kukukomboa, kwa hakika kama Yehova anavyoishi, mimi mwenyewe nitakukomboa. Lala hapa mpaka asubuhi.” 14  Basi akalala miguuni pake mpaka asubuhi, kisha akaamka kabla ya mapambazuko wakati ambapo ni vigumu kumtambua yeyote. Boazi akasema: “Isijulikane kwamba mwanamke alikuja kwenye uwanja wa kupuria.” 15  Naye akaendelea kusema: “Kilete kitambaa ulichojifunika ukitandaze.” Basi Ruthu akakitandaza, naye Boazi akampimia vipimo sita* vya shayiri na kumtwika, kisha Boazi akaenda jijini. 16  Ruthu akaenda kwa mama mkwe wake, ambaye alimuuliza: “Mambo yaliendaje,* binti yangu?” Akamwambia yote ambayo mwanamume huyo alimtendea. 17  Tena akasema: “Alinipa vipimo hivi sita vya shayiri na kuniambia, ‘Usiende kwa mama mkwe wako mikono mitupu.’” 18  Basi Naomi akamwambia: “Kaa hapa binti yangu, mpaka utakapojua jinsi itakavyokuwa, kwa maana mwanamume huyo hatapumzika mpaka atakapotimiza jambo hilo leo.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “mahali pa kumpumzika.”
Au “pindo la vazi lako.”
Tnn., “katika lango lote la watu wangu.”
Labda vipimo sita vya sea, au karibu kilogramu 20. Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “Wewe ni nani?”