Ruthu 4:1-22

  • Boazi awa mkombozi (1-12)

  • Boazi na Ruthu wamzaa Obedi (13-17)

  • Ukoo wa Daudi (18-22)

4  Sasa Boazi akapanda kwenda kwenye lango la jiji+ na kuketi hapo. Na tazama! yule mkombozi ambaye Boazi alimtaja+ alikuwa akipita. Basi Boazi akamwita: “Fulani wa fulani, njoo, keti hapa.” Akaja na kuketi.  Kisha Boazi akawaita wazee kumi wa jiji,+ akawaambia: “Ketini hapa.” Nao wakaketi.  Ndipo Boazi akamwambia mkombozi huyo:+ “Naomi aliyerudi kutoka katika mashamba ya Moabu+ hana budi kuuza shamba la ndugu yetu Elimeleki.+  Niliona nikufahamishe jambo hilo na kukwambia, ‘Linunue mbele ya wakaaji na wazee wa watu wangu.+ Ikiwa utalikomboa, likomboe. Lakini ikiwa hutalikomboa, niambie ili nijue, kwa maana una haki ya kulikomboa, mimi ni wa pili.’” Mtu huyo akasema: “Niko tayari kulikomboa.”+  Kisha Boazi akamwambia: “Siku utakapolinunua shamba hilo kutoka kwa Naomi, unapaswa kulinunua pia kutoka kwa Ruthu Mmoabu, mke wa mwanamume aliyekufa, ili kurudisha jina la mume wake aliyekufa katika urithi huo.”+  Basi mkombozi huyo akasema: “Siwezi kulikomboa kwa maana huenda nikaharibu urithi wangu mwenyewe. Likomboe kwa ajili yako mwenyewe ukitumia haki yangu ya kukomboa, kwa sababu siwezi kulikomboa.”  Ili kuhalalisha makubaliano yoyote, hii ndiyo desturi iliyofuatwa zamani katika Israeli kuhusu haki ya kukomboa na kubadilishana vitu: Mtu alipaswa kuvua kiatu chake+ na kumpa mwenzake, na huo ndio utaratibu uliofuatwa ili kuthibitisha* makubaliano katika Israeli.  Kwa hiyo mkombozi huyo alivua kiatu alipomwambia Boazi, “Linunue liwe lako.”  Kisha Boazi akawaambia wazee na watu wote waliokuwepo: “Ninyi ni mashahidi+ leo kwamba ninanunua kutoka kwa Naomi vitu vyote vilivyokuwa vya Elimeleki na vitu vyote vilivyokuwa vya Kilioni na Maloni. 10  Namchukua pia Ruthu Mmoabu, mke wa Maloni, awe mke wangu ili kurudisha jina la mwanamume huyo aliyekufa katika urithi wake,+ ili jina la mwanamume huyo aliyekufa lisifutiliwe mbali kutoka kati ya ndugu zake na kutoka katika lango la jiji lake. Ninyi ni mashahidi leo.”+ 11  Ndipo watu wote waliokuwa katika lango la jiji na wale wazee wakasema: “Sisi ni mashahidi! Yehova na ambariki mke anayekuja nyumbani mwako ili awe kama Raheli na Lea, ambao walijenga nyumba ya Israeli.+ Ufanikiwe katika Efratha+ na ujijengee jina zuri* katika Bethlehemu.+ 12  Nyumba yako na iwe kama nyumba ya Perezi,+ ambaye Tamari alimzalia Yuda, kupitia uzao ambao Yehova atakupa kutoka kwa mwanamke huyu kijana.”+ 13  Basi Boazi akamwoa Ruthu. Akalala naye, na Yehova akamwezesha kupata mimba na kuzaa mwana. 14  Halafu wanawake wakamwambia Naomi: “Yehova na asifiwe, ambaye hakukuacha bila mkombozi leo. Jina la mwana huyo na litangazwe katika Israeli! 15  Yeye* amekurudishia uhai wako* na atakutunza uzeeni, kwa sababu amezaliwa na binti mkwe wako anayekupenda+ na ambaye ni bora kwako kuliko wana saba.” 16  Naomi akamchukua mtoto huyo na kumbeba kifuani, naye akamtunza.* 17  Kisha wanawake majirani wakampa jina. Wakasema, “Naomi amezaa mwana,” nao wakamwita Obedi.+ Yeye ndiye baba ya Yese,+ aliyemzaa Daudi. 18  Basi huu ndio ukoo wa* Perezi:+ Perezi alimzaa Hezroni;+ 19  Hezroni akamzaa Ramu; Ramu akamzaa Aminadabu;+ 20  Aminadabu+ akamzaa Nashoni; Nashoni akamzaa Salmoni; 21  Salmoni akamzaa Boazi; Boazi akamzaa Obedi; 22  Obedi akamzaa Yese;+ na Yese akamzaa Daudi.+

Maelezo ya Chini

Au “kutoa ushuhuda wa.”
Tnn., “utangaze jina.”
Yaani, mjukuu wa Naomi.
Au “nafsi yako.”
Au “akawa mlezi wake.”
Tnn., “hivi ndivyo vizazi vya.”