Sefania 2:1-15

  • Mtafuteni Yehova kabla ya siku yake ya hasira (1-3)

    • Tafuteni uadilifu na upole (3)

    • “Huenda mtafichwa” (3)

  • Mataifa jirani yahukumiwa (4-15)

2  Kusanyikeni pamoja, naam, jikusanyeni,+Ewe taifa lisiloona aibu.+   Kabla amri haijatekelezwa,Kabla siku hiyo haijapeperuka kama makapi,Kabla hasira inayowaka ya Yehova haijaja juu yenu,+Kabla siku ya hasira ya Yehova haijaja juu yenu,   Mtafuteni Yehova,+ ninyi nyote mlio wapole* wa dunia,Mnaoshika amri zake za uadilifu.* Utafuteni uadilifu, utafuteni upole.* Huenda* mtafichwa katika siku ya hasira ya Yehova.+   Kwa maana Gaza litakuwa jiji lililoachwa mahame;Na Ashkeloni litafanywa ukiwa.+ Waashdodi watafukuzwa kweupe kabisa wakati wa mchana,*Na Ekroni litang’olewa.+   “Ole kwa wale wanaokaa pwani, taifa la Wakerethi!+ Neno la Yehova liko dhidi yenu. Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti, nitakuangamiza,Hivi kwamba hakuna mkaaji atakayebaki.   Na eneo la pwani litakuwa eneo la malisho,Lenye visima kwa ajili ya wachungaji na mazizi ya mawe kwa ajili ya kondoo.   Litakuwa eneo la watu waliobaki wa nyumba ya Yuda;+Watalisha huko. Jioni watalala chini katika nyumba za Ashkeloni. Kwa maana Yehova Mungu wao atawaelekezea uangalifu,*Naye atawakusanya na kuwarudisha mateka wao.”+   “Nimesikia shutuma za Moabu+ na matusi ya Waamoni,+ Ambao wamewadhihaki watu wangu na kujigamba kwa vitisho dhidi ya eneo lao.+   Kwa hiyo, kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli,“Moabu itakuwa tu kama Sodoma,+Na Waamoni kama Gomora,+Mahali penye upupu, shimo la chumvi, na nchi iliyoachwa ukiwa milele.+ Watu wangu waliobaki watawapora,Na watu waliobaki wa taifa langu watamiliki nchi yao. 10  Hayo ndiyo watakayopata badala ya kiburi chao,+Kwa sababu waliwadhihaki na kujikweza dhidi ya watu wa Yehova wa majeshi. 11  Yehova atawaogopesha sana;* Kwa maana ataiharibu kabisa* miungu yote ya dunia,Na visiwa vyote vya mataifa vitamwinamia,*+Kila kisiwa kikiwa mahali pake. 12  Ninyi Waethiopia mtauawa pia kwa upanga wangu.+ 13  Ataunyoosha mkono wake kuelekea kaskazini na kuangamiza Ashuru,Naye atalifanya Ninawi liwe ukiwa,+ liwe kavu kama jangwa. 14  Mifugo italala ndani yake, kila aina ya wanyama wa mwituni.* Mwari na nungunungu watalala usiku kati ya nguzo zake zilizoanguka. Sauti itaimba dirishani. Kutakuwa na uharibifu kwenye kizingiti;Kwa maana atafunua mbao za mierezi zinazopamba kuta. 15  Hili ndilo jiji lenye kiburi lililokuwa likikaa kwa usalama,Lililokuwa likisema moyoni mwake, ‘Mimi ndiye, na hakuna mwingine yeyote.’ Jinsi ambavyo limekuwa kitu chenye kutisha,Mahali ambapo wanyama wa mwituni wanalala! Kila mtu anayepita karibu nalo atapiga mluzi na kutikisa ngumi yake.”+

Maelezo ya Chini

Au “wanyenyekevu.”
Tnn., “hukumu yake.”
Au “unyenyekevu.”
Au “Inaelekea.”
Au “adhuhuri.”
Au “atawatunza.”
Au “atawatisha.”
Au “ataidhoofisha.”
Au “vitamwabudu.”
Tnn., “kila mnyama wa mwituni katika taifa.”