Sefania 3:1-20

  • Yerusalemu, jiji lenye uasi na upotovu (1-7)

  • Kuhukumiwa na kurudishwa (8-20)

    • Wapewa lugha safi (9)

    • Wanyenyekevu na wapole wataokolewa (12)

    • Yehova atashangilia kwa sababu ya Sayuni (17)

3  Ole kwa jiji lenye uasi, lenye uchafu, lenye ukandamizaji!+  Halijatii sauti yoyote;+ halijakubali nidhamu yoyote.+ Halijamtumaini Yehova;+ halijamkaribia Mungu wake.+   Wakuu wake walio ndani yake ni simba wanaonguruma.+ Waamuzi wake ni mbwamwitu wakati wa usiku;Hawaachi hata mfupa mmoja wa kuguguna mpaka asubuhi.   Manabii wake ni wakaidi, wanaume wenye hila.+ Makuhani wake wanachafua kilicho kitakatifu;+Wanaitendea sheria kikatili.+   Yehova ni mwadilifu miongoni mwake;+ hatendi kosa lolote. Asubuhi baada ya asubuhi hutangaza hukumu zake,+Kama nuru ya mchana isivyokosa kuangaza. Lakini asiye mwadilifu haoni aibu hata kidogo.+   “Niliyaangamiza mataifa; minara yao ya pembeni iliachwa ukiwa. Niliharibu barabara zao, hivi kwamba hakuna yeyote aliyepita. Majiji yao yaliachwa magofu, bila mtu yeyote, bila mkaaji yeyote.+   Nikasema, ‘Hakika mtaniogopa na kukubali nidhamu,’*+ Ili makao yake yasiweze kuharibiwa+—Ni lazima nilifanye liwajibike* kwa sababu ya mambo hayo yote. Lakini walitamani hata zaidi kutenda kwa upotovu.+   ‘Kwa hiyo endeleeni kunitarajia,’*+ asema Yehova, ‘Mpaka siku nitakapoinuka ili kuchukua nyara,* Kwa maana uamuzi wangu wa hukumu ni kuyakusanya mataifa, kuzikusanya falme,Niwamwagie ghadhabu yangu, hasira yangu yote inayowaka;+Kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa bidii yangu.+   Kwa maana wakati huo nitabadili lugha ya mataifa iwe lugha safi,Ili wote waweze kuliitia jina la Yehova,Wamtumikie bega kwa bega.’*+ 10  Kutoka eneo la mito ya Ethiopia,Wale wanaonisihi, binti ya watu wangu waliotawanywa, wataniletea zawadi.+ 11  Siku hiyo hamtaaibishwaKwa sababu ya matendo yenu yote ya uasi mliyonitendea,+ Kwa maana wakati huo nitawaondoa kati yenu watu wenye kiburi wanaojigamba;Nanyi hamtakuwa tena na kiburi katika mlima wangu mtakatifu.+ 12  Nitawaruhusu watu wanyenyekevu na wapole wabaki miongoni mwenu,+Nao watapata kimbilio katika jina la Yehova. 13  Waisraeli watakaobaki+ hawatatenda mambo yasiyo ya uadilifu;+Hawatasema uwongo, wala hawatakuwa na ndimi za udanganyifu vinywani mwao;Watakula* na kulala, na hakuna yeyote atakayewaogopesha.”+ 14  Paza sauti kwa shangwe, Ee binti ya Sayuni! Paza sauti kwa ushindi, Ee Israeli!+ Shangilia na kufurahi kwa moyo wako wote, Ee binti ya Yerusalemu!+ 15  Yehova ameondoa hukumu ulizokabili.+ Amemfukuza adui yako.+ Mfalme wa Israeli, Yehova, yuko katikati yako.+ Hutaogopa msiba tena.+ 16  Siku hiyo jiji la Yerusalemu litaambiwa: “Usiogope, Ee Sayuni.+ Usilegeze mikono yako. 17  Yehova Mungu wako yuko katikati yako.+ Akiwa Mwenye nguvu, ataokoa. Atakushangilia kwa shangwe kubwa.+ Atakaa kimya* katika upendo wake. Atakushangilia kwa kelele za shangwe. 18  Nitawakusanya pamoja wale wanaohuzunika kwa sababu ya kukosa sherehe zako;+Hawakuwa pamoja nawe kwa sababu ya kubeba shutuma yake.+ 19  Tazama! Wakati huo nitawachukulia hatua wote wanaokukandamiza;+Nami nitamwokoa yule anayechechemea,+Nitawakusanya pamoja waliotawanyika.+ Nitawafanya kuwa kitu cha sifa na umaarufu*Katika kila nchi ambamo waliaibishwa. 20  Wakati huo nitawaleta ndani,Wakati nitakapowakusanya pamoja. Kwa maana nitawafanya kuwa kitu cha umaarufu* na sifa+ miongoni mwa mataifa yote duniani,Nitakapowakusanya mateka wenu mbele ya macho yenu,” asema Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “niliadhibu.”
Au “kurekebishwa.”
Au “kuningojea kwa subira.”
Au labda, “nitakapoinuka nikiwa shahidi.”
Au “wamwabudu kwa umoja.”
Au “Watajilisha malishoni.”
Au “Atanyamaza; Atatulia; Ataridhika.”
Tnn., “jina.”
Tnn., “jina.”