Kwa Tito 1:1-16

  • Salamu (1-4)

  • Tito aagizwa kuweka rasmi wazee huko Krete (5-9)

  • Wakaripie wale wanaoasi (10-16)

1  Paulo, mtumwa wa Mungu na mtume wa Yesu Kristo kulingana na imani ya waliochaguliwa wa Mungu, na ujuzi sahihi wa ile kweli ambayo inapatana na ujitoaji-kimungu*  na inayotegemea tumaini la uzima wa milele+ ambao Mungu, asiyeweza kusema uwongo,+ aliahidi zamani za kale;  lakini kwa wakati wake, alifanya neno lake lijulikane kupitia kazi ya kuhubiri ambayo nilikabidhiwa+ kulingana na amri ya Mwokozi wetu, Mungu;  kwa Tito, mwanangu halisi kulingana na imani tunayoshiriki: Na uwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Mwokozi wetu.  Nilikuacha Krete ili urekebishe mambo yaliyokuwa na kasoro* na kuweka rasmi wazee katika jiji moja baada ya lingine, kama nilivyokuagiza:  ikiwa kuna mwanamume asiye na shtaka, mume wa mke mmoja, mwenye watoto wanaoamini ambao hawana mashtaka ya kuwa wapotovu* au waasi.+  Mwangalizi ni msimamizi aliyechaguliwa na Mungu, hivyo hapaswi kuwa na shtaka, asiwe mshupavu,+ asiwe mwenye kukasirika upesi,+ asiwe mlevi, asiwe mkatili,* asiwe na pupa ya mapato yasiyo ya haki,  bali awe mkaribishaji wageni,*+ anayependa mema, mwenye utimamu wa akili,*+ mwadilifu, mshikamanifu,+ anayejidhibiti,+  anayefuata kikamili neno la uaminifu* katika ustadi wake wa kufundisha,+ ili aweze kutia moyo* kwa fundisho lenye manufaa*+ na pia kuwakaripia+ wale ambao hulipinga. 10  Kwa maana kuna watu wengi waasi, wanaoongea maneno yasiyo na faida, na wadanganyifu, hasa wale wanaoshikamana na tohara.+ 11  Lazima watu hao wanyamazishwe, kwa sababu wanaendelea kupotosha imani ya nyumba nzima nzima kwa kufundisha mambo ambayo hawapaswi, wakiwa na nia ya kupata mapato yasiyo ya haki. 12  Mmoja wao, nabii wao wenyewe, alisema: “Wakrete ni waongo sikuzote, wanyama hatari wa mwituni, walafi wasiofanya kazi.” 13  Ushahidi huu ni wa kweli. Kwa sababu hiyo endelea kuwakaripia kwa ukali ili wawe na imani yenye afya, 14  na wasisikilize hadithi za uwongo za Kiyahudi na amri za watu ambao wanaiacha kweli. 15  Vitu vyote ni safi kwa watu safi;+ lakini kwa watu waliochafuliwa na wasio na imani hakuna chochote kilicho safi, kwa kuwa akili na dhamiri zao zimechafuliwa.+ 16  Wao hutangaza hadharani kwamba wanamjua Mungu, lakini wanamkana kwa matendo yao,+ kwa sababu ni wenye kuchukiza, wasiotii, na wasiostahili kufanya kazi yoyote njema.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “upungufu.”
Au “watukutu.”
Au “asiwe mpiga watu.”
Au “anayefanya maamuzi mazuri; mwenye busara.”
Au “mkarimu.”
Au “ujumbe wenye kutegemeka.”
Au “kuhimiza.”
Au “lenye afya; lenye faida.”