Kwa Tito 3:1-15

  • Kujitiisha kwa njia inayofaa (1-3)

  • Uwe tayari kufanya matendo mema (4-8)

  • Epuka mabishano ya kipumbavu na madhehebu (9-11)

  • Maagizo ya kibinafsi na salamu (12-15)

3  Endelea kuwakumbusha wajitiishe na kuzitii serikali na mamlaka,+ wawe tayari kwa ajili ya kila kazi njema,  wasiseme vibaya kumhusu yeyote, wasiwe wagomvi, bali wawe na usawaziko,+ wakionyesha upole wote kwa watu wote.+  Kwa maana hata sisi wakati mmoja tulikuwa watu wasio na akili, wasiotii, waliopotoshwa, watumwa wa tamaa na anasa mbalimbali, tukiendeleza ubaya na wivu, tukiwa wenye kuchukiza, na kuchukiana.  Hata hivyo, fadhili za Mwokozi wetu, Mungu,+ na upendo wake kwa wanadamu ulipofunuliwa,  (si kwa sababu ya matendo yoyote ya uadilifu tuliyokuwa tumefanya,+ bali kwa sababu ya rehema yake),+ alituokoa kupitia kuoshwa kulikotuleta kwenye uzima,+ na kwa kutufanya wapya kupitia roho takatifu.+  Aliimimina roho hii kwa wingi* juu yetu kupitia Yesu Kristo Mwokozi wetu,+  ili baada ya kutangazwa kuwa waadilifu kupitia fadhili zake zisizostahiliwa,+ sisi tuwe warithi+ kulingana na tumaini la uzima wa milele.+  Maneno haya ni yenye kutegemeka, na ninataka uendelee kuyakazia mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu waendelee kukaza fikira zao katika kudumisha matendo mema. Mambo haya ni mema na yanawanufaisha watu.  Lakini epuka mabishano ya kipumbavu na kubishana kuhusu ukoo na mizozo na mapambano kuhusu Sheria, kwa maana mambo hayo hayana faida na ni ya ubatili.+ 10  Kuhusu mtu anayeendeleza madhehebu,+ mwepukeni+ baada ya kumwonya* mara ya kwanza na ya pili,+ 11  kwa kuwa mtu kama huyo ameiacha njia na anafanya dhambi, naye amejihukumu. 12  Nitakapomtuma Artema au Tikiko+ kwako, jitahidi kuja Nikopoli unione, kwa maana nimeamua kukaa huko majira ya baridi kali. 13  Jitahidi kabisa kuwapa Zena, aliye na ujuzi wa Sheria, na Apolo vitu wanavyohitaji ili wasikose kitu chochote kwa ajili ya safari yao.+ 14  Lakini acha watu wetu pia wajifunze kuendelea kufanya matendo mema ili wasaidie kunapokuwa na uhitaji wa dharura,+ ili wasikose kuzaa matunda.*+ 15  Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wape salamu zangu wale wanaotupenda katika imani. Fadhili zisizostahiliwa za Mungu na ziwe pamoja nanyi nyote.

Maelezo ya Chini

Au “kwa ukarimu.”
Au “kumkemea.”
Au “kupata matokeo mazuri.”