Ufunuo kwa Yohana 12:1-17

  • Mwanamke, mtoto wa kiume, na joka (1-6)

  • Mikaeli apigana na yule joka (7-12)

    • Joka atupwa duniani (9)

    • Ibilisi anajua kwamba ana kipindi kifupi (12)

  • Joka amtesa mwanamke (13-17)

12  Kisha ishara kubwa ikaonekana mbinguni: Mwanamke+ aliyepambwa* jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake palikuwa na taji la nyota 12,  naye alikuwa na mimba. Na alikuwa akilia akiwa katika maumivu na uchungu wa kuzaa.  Ishara nyingine ikaonekana mbinguni. Tazama! Joka mkubwa wa rangi ya moto,+ mwenye vichwa saba na pembe kumi na mataji saba* juu ya vichwa vyake;  na mkia wake unakokota theluthi moja ya nyota+ za mbinguni, naye akazitupa chini duniani.+ Na huyo joka akaendelea kusimama mbele ya yule mwanamke+ aliyekuwa karibu kuzaa, ili atakapozaa, ammeze mtoto wake.  Na yule mwanamke akazaa mwana,+ wa kiume, atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.+ Na mtoto wake akanyakuliwa* mpaka kwa Mungu na kwenye kiti chake cha ufalme.  Na yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotayarishwa na Mungu, na hapo watamlisha kwa siku 1,260.+  Na vita vikatokea ghafla mbinguni: Mikaeli*+ na malaika zake wakapigana na yule joka, naye joka na malaika zake wakapigana nao  lakini hawakushinda,* wala mahali hapakupatikana tena mbinguni kwa ajili yao.  Basi yule joka mkubwa+ akatupwa chini, yule nyoka wa zamani,+ anayeitwa Ibilisi+ na Shetani,+ anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa;+ akatupwa chini duniani,+ na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye. 10  Nikasikia sauti kubwa mbinguni ikisema: “Sasa kumekuwa na wokovu+ na nguvu na Ufalme wa Mungu wetu+ na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu ametupwa chini, anayewashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu!+ 11  Nao wakamshinda+ kwa sababu ya damu ya Mwanakondoo+ na kwa sababu ya neno lao la kutoa ushahidi,+ nao hawakupenda nafsi zao*+ hata walipokabili kifo. 12  Kwa sababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa ndani yake! Ole wa dunia na wa bahari,+ kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.”+ 13  Sasa yule joka alipoona kwamba ametupwa chini duniani,+ alimtesa yule mwanamke+ aliyezaa mtoto wa kiume. 14  Lakini yule mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa,+ ili aruke kwenda nyikani mahali pake, ambapo atalishwa kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati*+ mbali na uso wa yule nyoka.+ 15  Naye nyoka akatapika maji kama mto kutoka katika kinywa chake nyuma ya yule mwanamke, ili kumzamisha katika mto huo. 16  Lakini dunia ikaja kumsaidia mwanamke, nayo dunia ikafungua kinywa chake na kuumeza mto ambao yule joka aliutapika kutoka katika kinywa chake. 17  Basi yule joka akawa na ghadhabu kumwelekea yule mwanamke, naye akaenda zake kupigana na wale waliobaki wa uzao wake,*+ wanaoshika amri za Mungu na walio na kazi ya kutoa ushahidi kumhusu Yesu.+

Maelezo ya Chini

Au “aliyevikwa.”
Au “tepe saba za kichwani za kifalme.”
Au “akachukuliwa.”
Maana yake “Ni Nani Aliye Kama Mungu?”
Au labda, “lakini alishindwa [yaani, joka].”
Au “uhai wao.” Angalia Kamusi.
Yaani, nyakati tatu na nusu.
Tnn., “mbegu yake.”