Ufunuo kwa Yohana 13:1-18

  • Mnyama-mwitu mwenye vichwa saba atoka baharini (1-10)

  • Mnyama-mwitu mwenye pembe mbili atoka duniani (11-13)

  • Sanamu ya mnyama-mwitu mwenye vichwa saba (14, 15)

  • Alama na namba ya mnyama-mwitu (16-18)

13  Naye* akasimama tuli juu ya mchanga wa bahari. Nami nikamwona mnyama wa mwituni+ akipanda kutoka baharini,+ naye alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, na mataji kumi* juu ya pembe zake, lakini juu ya vichwa vyake majina yenye makufuru.  Basi yule mnyama wa mwituni niliyemwona alikuwa kama chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu, na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Na yule joka+ akampa huyo mnyama nguvu zake na kile kiti chake cha ufalme na mamlaka kubwa.+  Nikaona kimoja kati ya vichwa vyake kikiwa kimejeruhiwa vibaya lakini jeraha hilo la kifo lilipona,+ na dunia yote ikamfuata kwa mshangao yule mnyama wa mwituni.  Nao wakamwabudu yule joka kwa sababu alimpa mamlaka yule mnyama wa mwituni, nao wakamwabudu mnyama wa mwituni kwa maneno haya: “Ni nani aliye kama huyu mnyama wa mwituni, na ni nani anayeweza kupigana naye?”  Akapewa kinywa kinachosema mambo makuu na makufuru, akapewa pia mamlaka ya kutenda kwa miezi 42.+  Naye akafungua kinywa chake kwa kumkufuru+ Mungu ili kulikufuru jina lake na makao yake, na hata wale wanaokaa mbinguni.+  Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watakatifu na kuwashinda,+ na akapewa mamlaka juu ya kila kabila na watu na lugha na taifa.  Na wale wote wanaokaa duniani watamwabudu. Tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu, hakuna jina la hata mmoja wao lililoandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha uzima+ cha Mwanakondoo aliyechinjwa.+  Ikiwa yeyote ana sikio, na asikie.+ 10  Ikiwa yeyote amekusudiwa kwenda utekwani, ataenda utekwani. Ikiwa yeyote ataua* kwa upanga, naye lazima auawe kwa upanga.+ Hapa ndipo watakatifu+ wanahitaji uvumilivu+ na imani.+ 11  Kisha nikamwona mnyama mwingine wa mwituni akipanda kutoka katika dunia, naye alikuwa na pembe mbili kama mwanakondoo, lakini akaanza kuzungumza kama joka.+ 12  Anatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza wa mwituni+ aliye machoni pake. Naye huifanya dunia na wale wanaokaa duniani wamwabudu yule mnyama wa kwanza wa mwituni, ambaye jeraha lake la kifo lilipona.+ 13  Naye hufanya ishara kubwa, hata hufanya moto ushuke kutoka mbinguni mpaka duniani machoni pa wanadamu. 14  Naye huwapotosha wale wanaokaa duniani, kwa sababu ya ishara alizoruhusiwa kufanya machoni pa yule mnyama wa mwituni, huku akiwaambia wale wanaokaa duniani watengeneze sanamu+ ya yule mnyama wa mwituni aliyekuwa na pigo la upanga lakini bado akabaki hai.+ 15  Naye akaruhusiwa kuipa pumzi* ile sanamu ya mnyama wa mwituni, ili ile sanamu ya mnyama wa mwituni iweze kusema na pia kufanya wale wote wanaokataa kuiabudu ile sanamu ya mnyama wa mwituni wauawe. 16  Anawalazimisha watu wote—wadogo kwa wakubwa, matajiri kwa maskini, walio huru kwa watumwa—ili wote watiwe alama kwenye mkono wao wa kulia au kwenye paji la uso wao,+ 17  na ili yeyote asiweze kununua au kuuza isipokuwa mtu aliye na ile alama, jina+ la yule mnyama wa mwituni au namba ya jina lake.+ 18  Hapa ndipo hekima inapohitajiwa: Yule aliye na ufahamu na afanye hesabu ya namba ya yule mnyama wa mwituni, kwa maana ni namba ya mwanadamu, na namba yake ni 666.+

Maelezo ya Chini

Yaani, yule joka.
Au “tepe kumi za kichwani za kifalme.”
Au labda, “Ikiwa yeyote atalazimika kuuawa.”
Au “roho.”