Ufunuo kwa Yohana 15:1-8

  • Malaika saba wakiwa na mapigo saba (1-8)

    • Wimbo wa Musa na wa Mwanakondoo (3, 4)

15  Nami nikaona huko mbinguni ishara nyingine kubwa na ya ajabu sana, malaika saba+ wenye mapigo saba. Hayo ndiyo ya mwisho, kwa sababu kupitia hayo hasira ya Mungu inamalizika.+  Nami nikaona kitu kama bahari ya kioo+ iliyochanganyika na moto, na wale wanaomshinda+ yule mnyama wa mwituni na sanamu yake+ na ile namba ya jina lake+ walikuwa wamesimama kando ya ile bahari ya kioo, wakiwa wameshika vinubi vya Mungu.  Walikuwa wanaimba wimbo wa Musa+ mtumwa wa Mungu na wimbo wa Mwanakondoo,+ wakisema: “Matendo yako ni makuu na ya ajabu,+ Yehova* Mungu, Mweza-Yote.+ Njia zako ni za uadilifu na za kweli,+ Mfalme wa umilele.+  Ni nani ambaye kwa kweli hatakuogopa wewe, Yehova,* na kulitukuza jina lako, kwa kuwa wewe peke yako ni mshikamanifu?+ Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako,+ kwa sababu amri zako za uadilifu zimefunuliwa.”  Baada ya hayo nikaona, patakatifu pa hema la ushahidi+ pakifunguliwa mbinguni,+  na wale malaika saba wenye mapigo saba+ wakatokea katika patakatifu, wakiwa wamevaa kitani safi, kinachong’aa na wakiwa wamefunga mishipi ya dhahabu kifuani.  Mmoja wa wale viumbe hai wanne akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa hasira ya Mungu,+ anayeishi milele na milele.  Na patakatifu pakajaa moshi kwa sababu ya utukufu wa Mungu+ na kwa sababu ya nguvu zake, na hakuna yeyote aliyeweza kuingia patakatifu mpaka yale mapigo saba+ ya wale malaika saba yalipomalizika.

Maelezo ya Chini