Ufunuo kwa Yohana 17:1-18

  • “Babiloni Mkuu” ahukumiwa (1-18)

    • Kahaba mkubwa aketi juu ya mnyama-mwitu mwenye rangi nyekundu (1-3)

    • Mnyama-mwitu ‘aliyekuwako, lakini hayuko, na bado yuko karibu kupanda kutoka katika shimo refu lisilo na mwisho’ (8)

    • Pembe kumi kupigana na Mwanakondoo (12-14)

    • Pembe kumi kumchukia kahaba (16, 17)

17  Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na mabakuli saba+ akaja na kuniambia: “Njoo, nitakuonyesha hukumu dhidi ya yule kahaba mkubwa anayekaa juu ya maji mengi,+  ambaye wafalme wa dunia walifanya uasherati* naye,+ na watu wanaokaa duniani walileweshwa kwa divai ya uasherati* wake.”+  Naye akanichukua katika nguvu za roho akanipeleka nyikani. Nami nikamwona mwanamke ameketi juu ya mnyama wa mwituni mwenye rangi nyekundu aliyejaa majina ya makufuru na aliyekuwa na vichwa saba na pembe kumi.  Yule mwanamke alikuwa amevaa nguo za rangi ya zambarau+ na nyekundu, naye alikuwa amepambwa kwa dhahabu na mawe ya thamani na lulu,+ na mkononi mwake alikuwa na kikombe cha dhahabu kilichojaa machukizo na mambo machafu ya uasherati* wake.  Alikuwa ameandikwa kwenye paji la uso wake jina la fumbo: “Babiloni Mkubwa, mama wa makahaba+ na wa machukizo ya dunia.”+  Nami nikaona kwamba yule mwanamke amelewa damu ya watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu.+ Basi, nilipomwona nilishangaa sana.  Ndipo yule malaika akaniambia: “Kwa nini ulishangaa? Nitakuambia fumbo la yule mwanamke+ na la yule mnyama wa mwituni anayembeba na aliye na vichwa saba na pembe kumi:+  Mnyama wa mwituni uliyemwona alikuwako, lakini hayuko, na bado yuko karibu kupanda kutoka katika shimo refu lisilo na mwisho,*+ naye ataenda kwenye uharibifu. Na watu wanaokaa duniani ambao majina yao hayajaandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha uzima+ tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu watashangaa watakapoona jinsi yule mnyama wa mwituni alivyokuwako, lakini hayuko, na bado atakuwapo.  “Hilo linahitaji akili yenye hekima: Vile vichwa saba+ vinamaanisha milima saba, ambapo yule mwanamke huketi juu yake. 10  Na kuna wafalme saba: Watano wameanguka, mmoja yuko, na yule mwingine bado hajafika; lakini atakapofika, lazima akae kwa muda mfupi. 11  Na yule mnyama wa mwituni aliyekuwako lakini hayuko,+ yeye pia ni mfalme wa nane, lakini anatokana na wale saba, naye anaenda zake kwenye uharibifu. 12  “Pembe kumi ulizoona zinamaanisha wafalme kumi ambao bado hawajapokea ufalme, lakini wanapokea mamlaka wakiwa wafalme kwa saa moja pamoja na yule mnyama wa mwituni. 13  Hao wana wazo moja, kwa hiyo wanampa yule mnyama wa mwituni nguvu na mamlaka yao. 14  Nao watapigana na Mwanakondoo,+ lakini kwa sababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme,+ Mwanakondoo atawashinda.+ Pia, wale walio pamoja naye walioitwa na waliochaguliwa na walio waaminifu watawashinda.”+ 15  Akaniambia: “Yale maji uliyoyaona, ambapo yule kahaba ameketi, yanamaanisha jamii za watu na umati na mataifa na lugha.+ 16  Na zile pembe kumi+ ulizoona, na yule mnyama wa mwituni,+ hao watamchukia yule kahaba+ na kumfanya kuwa ukiwa na uchi, nao watakula nyama yake na kumteketeza kabisa kwa moto.+ 17  Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao ili kutekeleza wazo lake,+ ndiyo, kutekeleza lile wazo lao moja kwa kumpa yule mnyama wa mwituni+ ufalme wao, mpaka maneno ya Mungu yatakapokwisha kutimizwa. 18  Na yule mwanamke+ uliyemwona anamaanisha lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wa dunia.”

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “abiso.” Angalia Kamusi.