Ufunuo kwa Yohana 18:1-24

  • “Babiloni Mkubwa” aanguka (1-8)

    • “Tokeni kwake, watu wangu” (4)

  • Kuombolezea anguko la Babiloni (9-19)

  • Kushangilia mbinguni kwa sababu ya anguko la Babiloni (20)

  • Babiloni kutupwa baharini kama jiwe (21-24)

18  Baada ya hayo nikamwona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kubwa, na dunia ikatiwa nuru kwa utukufu wake.  Naye akasema kwa sauti yenye nguvu: “Ameanguka! Babiloni Mkubwa ameanguka,+ naye amekuwa makao ya roho waovu na mahali pa kuvizia pa kila roho mchafu* na kila ndege mchafu anayechukiwa!+  Kwa sababu ya divai ya hamu* ya uasherati* wake, mataifa yote yamenaswa,+ na wafalme wa dunia walifanya uasherati naye,+ na wafanyabiashara* wa dunia walikuwa matajiri kutokana na nguvu za anasa yake isiyo na aibu.”  Nami nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni kwake, watu wangu,+ ikiwa hamtaki kushiriki pamoja naye dhambi zake, na ikiwa hamtaki kupokea sehemu ya mapigo yake.+  Kwa maana dhambi zake zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni,+ naye Mungu amekumbuka matendo yake yasiyo ya haki.*+  Mlipeni kama alivyowatendea wengine,+ ndiyo, mlipeni mara mbili kwa yale aliyotenda;+ katika kikombe+ alichochanganya, mtilieni mchanganyiko mara mbili.+  Kwa kadiri alivyojitukuza na kuishi katika anasa isiyo na aibu, kwa kadiri hiyo mpeni mateso na maombolezo. Kwa maana anaendelea kusema moyoni mwake: ‘Ninaketi nikiwa malkia, mimi si mjane, nami sitaona maombolezo kamwe.’+  Hiyo ndiyo sababu mapigo yake yatakuja katika siku moja, kifo na kuomboleza na njaa kali, naye atateketezwa kabisa kwa moto,+ kwa sababu Yehova* Mungu, aliyemhukumu, ni mwenye nguvu.+  “Na wafalme wa dunia waliofanya uasherati* naye na kuishi naye katika anasa isiyo na aibu watalia na kujipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake watakapoona moshi unaotokana na kuteketea kwake. 10  Watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake na kusema: ‘Ole, ole, wewe jiji kubwa,+ Babiloni wewe jiji lenye nguvu, kwa sababu hukumu yako imefika katika saa moja!’ 11  “Pia, wafanyabiashara wa dunia wanalia na kuomboleza kwa sababu yake, kwa kuwa hakuna yeyote wa kununua tena bidhaa zao zilizojaa, 12  mizigo iliyojaa ya dhahabu, fedha, mawe ya thamani, lulu, kitani bora, vitambaa vya zambarau, hariri, na vitambaa vyekundu; na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao zenye manukato; na kila aina ya kitu kilichotengenezwa kwa pembe za tembo, na kwa mbao za thamani, shaba, chuma, na marumaru; 13  pia mdalasini, viungo vya Kihindi, uvumba, mafuta yenye marashi, ubani, divai, mafuta ya zeituni, unga laini, ngano, ng’ombe, kondoo, farasi, magari, watumwa, na uhai wa binadamu.* 14  Ndiyo, tunda zuri ulilotamani* limekuacha, na vitu vyote vitamu na vitu vyenye fahari vimetoweka kutoka kwako, navyo havitapatikana tena kamwe. 15  “Wafanyabiashara waliouza vitu hivyo, waliopata utajiri kutokana naye, watasimama mbali kwa sababu ya kuogopa kuteseka kwake nao watalia na kuomboleza, 16  wakisema: ‘Ole, ole, lile jiji kubwa lililovaa kitani bora, zambarau, na kitambaa chekundu, na lililopambwa sana kwa mapambo ya dhahabu, mawe ya thamani, na lulu,+ 17  kwa sababu katika saa moja mali nyingi hivyo zimeharibiwa!’ “Na kila kapteni wa meli na kila mtu anayesafiri baharini na mabaharia na wale wote ambao hupata riziki baharini walisimama mbali 18  na kusema kwa sauti kubwa huku wakitazama moshi uliotokana na kuteketezwa kwake: ‘Ni jiji gani lililo kama lile jiji kubwa?’ 19  Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao na kupaza kilio, wakilia na kuomboleza, wakisema: ‘Ole, ole, lile jiji kubwa, ambalo wale wote waliokuwa na meli baharini walikuwa matajiri kutokana na utajiri wake, kwa sababu katika saa moja ameharibiwa!’+ 20  “Furahini kwa sababu yake, enyi mbingu,+ pia ninyi watakatifu+ na mitume na manabii, kwa sababu Mungu ametangaza hukumu juu yake kwa ajili yenu!”+ 21  Na malaika mwenye nguvu akainua jiwe lililo kama jiwe kubwa la kusagia na kulitupa baharini, akisema: “Hivi ndivyo Babiloni lile jiji kubwa litakavyotupwa chini kwa kasi sana, naye hatapatikana tena.+ 22  Na sauti ya waimbaji ambao hufuatanisha sauti zao kwa kinubi, ya wanamuziki, ya wapiga-filimbi, na ya wapiga-tarumbeta haitasikiwa tena ndani yako. Na hakuna fundi anayefanya kazi yoyote atakayepatikana tena ndani yako, na hakuna sauti ya jiwe la kusagia itakayosikiwa tena ndani yako. 23  Hakuna nuru ya taa itakayoangaza tena ndani yako, na hakuna sauti ya bwana harusi na bibi harusi itakayosikiwa tena ndani yako; kwa kuwa wafanyabiashara wako walikuwa watu wenye vyeo vya juu duniani, kwa maana mataifa yote yalipotoshwa kwa mazoea yako ya kuwasiliana na roho.+ 24  Ndiyo, ndani yake ilipatikana damu ya manabii na ya watakatifu+ na ya wale wote ambao wameuawa duniani.”+

Maelezo ya Chini

Au labda, “pumzi chafu; maneno yaliyoongozwa na roho.”
Au “hasira.”
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “wafanyabiashara wanaosafiri.”
Au “uhalifu wake.”
Angalia Kamusi.
Au “nafsi za binadamu.”
Au “ambalo nafsi yako ililitamani.”