Ufunuo kwa Yohana 2:1-29

  • Ujumbe kwa kutaniko la Efeso (1-7), la Smirna (8-11), la Pergamamu (12-17), la Thiatira (18-29)

2  “Kwa malaika+ wa kutaniko lililo huko Efeso+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule anayeshika zile nyota saba kwenye mkono wake wa kuume, na kutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu:+  ‘Ninayajua matendo yako, na kazi yako ya jasho na uvumilivu, na kwamba huwavumilii watu wabaya, nawe unawajaribu wale wanaosema kwamba wao ni mitume,+ lakini wao sio, nawe uliwagundua kuwa waongo.  Wewe pia unaonyesha uvumilivu, na umestahimili kwa ajili ya jina langu+ nawe hujachoka.+  Hata hivyo, nina jambo hili dhidi yako, kwamba umeacha upendo uliokuwa nao mwanzoni.  “‘Kwa hiyo kumbuka pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, nawe utubu+ na kufanya matendo uliyofanya mwanzoni. Usipofanya hivyo, nitakuja kwako, nami nitakiondoa kinara chako cha taa+ kutoka mahali pake, usipotubu.+  Hata hivyo, ninakusifu kwa jambo hili: kwamba unachukia matendo ya madhehebu ya Nikolao,+ ambayo mimi pia ninayachukia.  Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko:+ Yule atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kula matunda ya ule mti wa uzima,+ ulio katika paradiso ya Mungu.’  “Na kwa malaika wa kutaniko lililo huko Smirna andika: Haya ndiyo mambo anayosema, ‘wa Kwanza na wa Mwisho,’+ aliyekufa na akawa hai tena:+  ‘Ninajua dhiki na umaskini wako—lakini wewe ni tajiri+—na kufuru la wale wanaojiita Wayahudi na kwa kweli sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.+ 10  Usiogope mateso yatakayokupata hivi karibuni.+ Tazama! Ibilisi ataendelea kuwatupa gerezani baadhi yenu ili mjaribiwe kwa ukamili, nanyi mtapata dhiki kwa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufikia kifo, nami nitakupa taji la uzima.+ 11  Yule aliye na sikio na asikie+ yale ambayo roho inayaambia makutaniko: Yule atakayeshinda,+ kifo cha pili hakitamdhuru hata kidogo.’+ 12  “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Pergamamu andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule aliye na ule upanga mkali, mrefu na wenye makali pande mbili:+ 13  ‘Ninajua mahali unapokaa, yaani, mahali kilipo kiti cha ufalme cha Shetani; lakini bado unaendelea kulishika imara jina langu,+ nawe hukukana imani yako kwangu+ hata katika siku za Antipa, shahidi wangu mwaminifu+ aliyeuawa+ kando yenu, mahali anapokaa Shetani. 14  “‘Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako, kwamba unao hapo wale wanaofuata fundisho la Balaamu,+ aliyemfundisha Balaki+ kuweka kikwazo mbele ya wana wa Israeli, ili wale vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na kufanya uasherati.*+ 15  Vivyo hivyo, pia una wale wanaofuata fundisho la madhehebu ya Nikolao.+ 16  Basi tubu. Usipofanya hivyo, ninakuja kwako upesi, nami nitapigana nao kwa ule upanga mrefu wa kinywa changu.+ 17  “‘Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko:+ Yule atakayeshinda+ nitampa baadhi ya mana iliyofichwa,+ nami nitampa jiwe dogo jeupe, na kwenye jiwe hilo, jina jipya limeandikwa ambalo hakuna yeyote anayelijua ila yule anayelipokea.’ 18  “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Thiatira+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto+ na ambaye miguu yake ni kama shaba safi:+ 19  ‘Ninayajua matendo yako, na upendo wako na imani na huduma na uvumilivu wako, na kwamba matendo yako ya hivi karibuni yanazidi yale uliyofanya mwanzoni. 20  “‘Hata hivyo, nina jambo hili dhidi yako, kwamba unamvumilia yule mwanamke Yezebeli,+ anayejiita nabii, naye anafundisha na kuwapotosha watumwa wangu wafanye uasherati*+ na kula vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu. 21  Nami nilimpa muda wa kutubu, lakini hataki kutubu uasherati* wake. 22  Tazama! niko karibu kumtupa katika kitanda cha ugonjwa, na kuwatupa katika dhiki kuu wale wanaofanya uzinzi pamoja naye, ikiwa hawatatubu matendo yake. 23  Nami nitawaua watoto wake kwa ugonjwa hatari, hivi kwamba makutaniko yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mawazo ya ndani kabisa* na mioyo, nami nitampa kila mmoja wenu kulingana na matendo yake.+ 24  “‘Hata hivyo, ninawaambia wale wengine kati yenu walio huko Thiatira, wote wasiofuata fundisho hili, wale ambao hawakujua yale yanayoitwa “mambo mazito ya Shetani”:+ Mimi siwaongezei mzigo mwingine wowote. 25  Hata hivyo, shikeni imara lile mlilo nalo mpaka nitakapokuja.+ 26  Na yule atakayeshinda na kushika matendo yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,+ 27  kama vile nilivyopokea kutoka kwa Baba yangu, naye atawachunga watu kwa fimbo ya chuma+ hivi kwamba watavunjwa vipandevipande kama vyombo vya udongo. 28  Nami nitampa nyota ya asubuhi.+ 29  Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Au “hisia za ndani kabisa.” Tnn., “figo.”