Ufunuo kwa Yohana 3:1-22

  • Ujumbe kwa kutaniko la Sardisi (1-6), la Filadelfia (7-13), la Laodikia (14-22)

3  “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Sardi andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule aliye na zile roho saba za Mungu+ na zile nyota saba:+ ‘Ninayajua matendo yako, kwamba una jina* kuwa uko hai, lakini umekufa.+  Uwe macho,+ na uyatie nguvu mambo yanayobaki yaliyokuwa tayari kufa, kwa maana mimi sikuona kazi zako zikiwa zimefanywa kikamili* mbele za Mungu wangu.  Kwa hiyo, endelea kuzingatia* jinsi ulivyopokea na jinsi ulivyosikia, na uendelee kulishika, na utubu.+ Hakika usipoamka, nitakuja kama mwizi,+ nawe hutajua kamwe saa nitakayokuja juu yako.+  “‘Hata hivyo, una watu wachache* katika Sardi ambao hawakuyatia unajisi mavazi yao,+ nao watatembea pamoja nami wakiwa na mavazi meupe,+ kwa sababu wanastahili.  Kwa hiyo, yule atakayeshinda+ atavikwa mavazi meupe,+ na kwa vyovyote sitalifuta* jina lake kutoka katika kitabu cha uzima,+ bali nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu na mbele ya malaika zake.+  Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’  “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Filadelfia andika: Haya ndiyo mambo anayosema yule aliye mtakatifu,+ aliye wa kweli,+ aliye na ufunguo wa Daudi,+ anayefungua hivi kwamba hakuna yeyote atakayefunga na anayefunga hivi kwamba hakuna yeyote anayefungua:  ‘Ninayajua matendo yako—tazama! nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa,+ usioweza kufungwa na yeyote. Nami ninajua kwamba una nguvu kidogo, nawe ulilishika neno langu na hukulikana jina langu.  Tazama! Nitawafanya wale wa sinagogi la Shetani wanaosema ni Wayahudi ingawa sio,+ lakini wanasema uwongo—tazama! nitawafanya waje wainame* mbele ya miguu yako na kuwafanya wajue kwamba nimekupenda wewe. 10  Kwa sababu ulilishika neno kuhusu uvumilivu wangu,*+ mimi pia nitakulinda kutokana na ile saa ya jaribu+ itakayokuja juu ya dunia nzima inayokaliwa, ili kuwajaribu wale wanaokaa duniani. 11  Ninakuja upesi.+ Endelea kushika imara kile ulicho nacho, ili yeyote asilichukue taji lako.+ 12  “‘Yule atakayeshinda—nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, naye hataondoka humo kamwe, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu+ na jina la jiji la Mungu wangu, Yerusalemu Jipya+ linaloshuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu jipya.+ 13  Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’ 14  “Kwa malaika wa kutaniko lililo huko Laodikia+ andika: Haya ndiyo mambo anayosema Amina,+ shahidi+ mwaminifu na wa kweli,+ mwanzo wa uumbaji wa Mungu:+ 15  ‘Ninayajua matendo yako, kwamba wewe si baridi wala si moto. Laiti ungekuwa baridi au moto. 16  Basi kwa sababu wewe ni vuguvugu na si moto+ wala si baridi,+ nitakutapika kutoka kinywani mwangu. 17  Kwa sababu unasema, “Mimi ni tajiri,+ nimejipatia utajiri na sihitaji kitu chochote,” lakini hujui kwamba wewe ni mwenye taabu na wa kusikitikiwa na maskini na kipofu na uko uchi, 18  ninakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili uwe tajiri, na mavazi meupe ili uvae na kwamba aibu ya uchi wako isifunuliwe,+ na dawa ya macho ya kupaka katika macho yako+ ili uweze kuona.+ 19  “‘Wale wote ninaowapenda, mimi huwakaripia na kuwatia nidhamu.+ Basi uwe mwenye bidii na utubu.+ 20  Tazama! Nimesimama mlangoni na ninapiga hodi. Mtu yeyote akiisikia sauti yangu na kuufungua mlango, nitaingia ndani ya nyumba yake na kula mlo wa jioni pamoja naye, naye pamoja nami. 21  Yule atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kuketi pamoja nami kwenye kiti changu cha ufalme,+ kama vile nilivyoshinda na kuketi+ pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha ufalme. 22  Yule aliye na sikio na asikie yale ambayo roho inayaambia makutaniko.’”

Maelezo ya Chini

Au “unajulikana.”
Au “zimekamilika.”
Au “kukumbuka.”
Tnn., “majina machache.”
Au “sitaliondoa.”
Au “wasujudu.”
Au labda, “ulifuata mfano wangu wa uvumilivu.”