Ufunuo kwa Yohana 6:1-17

  • Mwanakondoo afungua mihuri ya kwanza sita (1-17)

    • Mshindi akiwa kwenye farasi mweupe (1, 2)

    • Aliyepanda farasi wa rangi ya moto aondoa amani (3, 4)

    • Aliyepanda farasi mweusi aleta njaa (5, 6)

    • Aliyepanda farasi wa kijivu anaitwa Kifo (7, 8)

    • Waliouawa, chini ya madhabahu (9-11)

    • Tetemeko kubwa la ardhi (12-17)

6  Naye Mwanakondoo+ alipofungua mmoja wa ile mihuri saba,+ nikaona, na kumsikia mmoja wa wale viumbe hai wanne+ akisema kwa sauti kama ya ngurumo: “Njoo!”  Nami nikaona, na tazama! farasi mweupe,+ na yule aliyeketi juu yake alikuwa na upinde; naye akapewa taji,+ naye akaenda akishinda na kukamilisha ushindi wake.+  Alipofungua muhuri wa pili, nikamsikia kiumbe hai wa pili+ akisema: “Njoo!”  Mwingine akatokea, farasi mwenye rangi ya moto, na yule aliyeketi juu yake akapewa ruhusa ya kuondoa amani duniani ili wauane, naye akapewa upanga mkubwa.+  Alipofungua muhuri wa tatu,+ nikamsikia kiumbe hai wa tatu+ akisema: “Njoo!” Nami nikaona, na tazama! farasi mweusi, na yule aliyeketi juu yake alikuwa na mizani mkononi mwake.  Nami nikasikia kitu kama sauti katikati ya wale viumbe hai wanne ikisema: “Kibaba* cha ngano kwa dinari*+ moja na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja; na usidhuru divai na mafuta ya zeituni.”+  Alipofungua muhuri wa nne, nikasikia sauti ya kiumbe hai wa nne+ akisema: “Njoo!”  Nami nikaona, na tazama! farasi wa rangi ya kijivu, na yule aliyeketi juu yake alikuwa na jina Kifo. Na Kaburi* lilikuwa likimfuata kwa ukaribu. Nao wakapewa mamlaka juu ya sehemu ya nne ya dunia, ili kuua kwa upanga mrefu na kwa upungufu wa chakula+ na kwa ugonjwa hatari na kwa wanyama wa mwituni wa dunia.+  Alipofungua muhuri wa tano, nikaona chini ya madhabahu+ nafsi*+ za wale waliouawa kwa sababu ya neno la Mungu na kwa sababu ya ushahidi waliokuwa wametoa.+ 10  Wakasema kwa sauti kubwa: “Bwana Mwenye Enzi Kuu, mtakatifu na wa kweli,+ utajizuia mpaka lini kuhukumu na kulipiza kisasi cha damu yetu juu ya wale wanaokaa duniani?”+ 11  Na kila mmoja wao akapewa kanzu nyeupe,+ nao wakaambiwa waendelee kupumzika kwa muda mfupi, mpaka idadi itimie ya watumwa wenzao na ndugu zao waliokuwa karibu kuuawa kama vile wao walivyouawa.+ 12  Nami nikaona alipofungua muhuri wa sita, na tetemeko kubwa la ardhi likatokea; na jua likawa jeusi kama gunia la manyoya,* na mwezi mzima ukawa kama damu,+ 13  na nyota za mbinguni zikaanguka duniani kama mtini unaotikiswa na upepo mkali unavyoangusha tini zake mbichi. 14  Na mbingu ikaondoka kama kitabu cha kukunjwa kinachokunjwa,+ na kila mlima na kila kisiwa vikaondolewa mahali pake.+ 15  Na wafalme wa dunia, maofisa wa cheo cha juu, viongozi wa kijeshi, matajiri, wenye nguvu, kila mtumwa, na kila mtu aliye huru wakajificha katika mapango na katika miamba ya milima.+ 16  Nao wanaendelea kuiambia milima na miamba: “Tuangukieni,+ mtufiche kutoka kwenye uso wa Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme+ na kutoka kwenye ghadhabu ya Mwanakondoo,+ 17  kwa sababu siku kuu ya ghadhabu yao imekuja,+ na ni nani anayeweza kusimama?”+

Maelezo ya Chini

Sarafu ya fedha ya Kiroma iliyolingana na mshahara wa siku moja. Angalia Nyongeza B14.
Au “Hadesi.” Angalia Kamusi.
Inaonekana ni uhai unaowakilishwa na damu yao iliyomwagwa kwenye madhabahu. Angalia Kamusi.
Huenda lililotengenezwa kwa manyoya ya mbuzi.