Ufunuo kwa Yohana 8:1-13

  • Muhuri wa saba wafunguliwa (1-6)

  • Tarumbeta nne za kwanza zapigwa (7-12)

  • Ole tatu zatangazwa (13)

8  Alipofungua+ muhuri wa saba,+ kukawa na kimya mbinguni kwa karibu nusu saa.  Nami nikawaona wale malaika saba+ wanaosimama mbele za Mungu, nao wakapewa tarumbeta saba.  Malaika mwingine, akiwa ameshika chombo cha uvumba* cha dhahabu,+ akafika na kusimama kwenye madhabahu, naye akapewa kiasi kikubwa cha uvumba+ ili autoe pamoja na sala za watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu+ ambayo ilikuwa mbele ya kile kiti cha ufalme.  Moshi wa uvumba kutoka kwenye mkono wa huyo malaika ukapanda pamoja na sala+ za watakatifu mbele za Mungu.  Lakini mara moja malaika huyo akachukua kile chombo cha uvumba, akakijaza moto kutoka kwenye madhabahu na kukitupa duniani. Kukatokea ngurumo na sauti na radi+ na tetemeko la ardhi.  Na wale malaika saba wenye tarumbeta saba+ wakajitayarisha kuzipiga.  Malaika wa kwanza akaipiga tarumbeta yake. Kukawa na mvua ya mawe na moto uliochanganyika na damu, nao ukatupwa duniani;+ na theluthi moja ya dunia ikateketezwa, na theluthi moja ya miti ikateketezwa, na mimea yote mibichi ikateketezwa.+  Malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake. Na kitu fulani kama mlima mkubwa unaowaka moto kikatupwa ndani ya bahari.+ Na theluthi moja ya bahari ikawa damu;+  na theluthi moja ya viumbe hai* wa baharini wakafa,+ na theluthi moja ya meli zikaharibiwa. 10  Malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake. Na nyota kubwa inayowaka kama taa ikaanguka kutoka mbinguni, ikaanguka juu ya theluthi moja ya mito na juu ya chemchemi za maji.*+ 11  Jina la nyota hiyo ni Pakanga. Na theluthi moja ya maji ikageuka kuwa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kutokana na maji hayo, kwa sababu yaligeuka kuwa machungu.+ 12  Malaika wa nne akaipiga tarumbeta yake. Na theluthi moja ya jua ikapigwa,+ pia theluthi moja ya mwezi, na theluthi moja ya nyota, ili theluthi moja ya hizo itiwe giza+ na mchana usiwe na nuru kwa theluthi moja, na usiku vivyo hivyo. 13  Nami nikaona na kusikia tai akiruka katikati ya mbingu akisema kwa sauti kubwa: “Ole, ole, ole+ wao wanaokaa duniani kwa sababu ya milio mingine ya tarumbeta za wale malaika watatu walio karibu kuzipiga tarumbeta zao!”+

Maelezo ya Chini

Au “chetezo.”
Au “viumbe wenye nafsi.”
Au “mabubujiko ya maji.”