Waamuzi 13:1-25

  • Malaika amtembelea Manoa na mke wake (1-23)

  • Samsoni azaliwa (24, 25)

13  Waisraeli wakaanza tena kutenda maovu machoni pa Yehova,+ na Yehova akawatia mikononi mwa Wafilisti+ kwa miaka 40.  Basi, kulikuwa na mtu mmoja huko Sora+ wa kabila la Dani+ aliyeitwa Manoa.+ Mke wake alikuwa tasa.+  Siku moja malaika wa Yehova akamtokea mwanamke huyo na kumwambia, “Wewe ni tasa na huna mtoto. Lakini utapata mimba na kuzaa mwana.+  Kwa hiyo, uwe mwangalifu usinywe divai wala chochote chenye kileo,+ na usile kitu chochote kisicho safi.+  Tazama! Utapata mimba na kuzaa mwana; na hakuna wembe utakaogusa kichwa chake+ kwa sababu mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu kuzaliwa,* naye atawaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wafilisti.”+  Ndipo mwanamke huyo akaenda na kumwambia hivi mume wake: “Mtu fulani wa Mungu wa kweli alinijia, na alikuwa kama malaika wa Mungu wa kweli, naye alikuwa mwenye kuogopesha sana. Sikumuuliza alikotoka, wala hakuniambia jina lake.+  Lakini aliniambia, ‘Tazama! Utapata mimba na kuzaa mwana. Basi usinywe divai wala chochote chenye kileo, wala usile kitu chochote kisicho safi, kwa sababu mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu kuzaliwa* mpaka kufa kwake.’”  Manoa akamsihi Yehova akisema, “Nakuomba Yehova. Tafadhali, tunaomba yule mtu wa Mungu wa kweli uliyekuwa umemtuma hivi punde arudi ili atufundishe jinsi ya kumlea mtoto atakayezaliwa.”  Basi Mungu wa kweli akamsikiliza Manoa, na yule malaika wa Mungu wa kweli akamjia tena huyo mwanamke alipokuwa ameketi shambani; lakini Manoa mume wake hakuwepo. 10  Mwanamke huyo akakimbia haraka na kumwambia mume wake, “Yule mtu aliyenijia siku ile amenitokea tena.”+ 11  Kwa hiyo Manoa akaondoka na kufuatana na mke wake. Akaja kwa mtu huyo na kumuuliza, “Ni wewe uliyezungumza na mke wangu?” naye akajibu: “Ni mimi.” 12  Ndipo Manoa akasema, “Maneno yako na yatimie! Mtoto huyo ataishi maisha ya aina gani, naye atafanya kazi gani?”+ 13  Basi malaika wa Yehova akamwambia hivi Manoa: “Mke wako na ajiepushe na kila kitu nilichomtajia.+ 14  Asile kitu chochote kinachotokana na mzabibu, asinywe divai wala chochote chenye kileo,+ na asile kitu chochote kisicho safi.+ Anapaswa kuzingatia mambo yote niliyomwagiza.” 15  Sasa Manoa akamwambia malaika wa Yehova, “Tafadhali kaa kidogo, tukuandalie mwanambuzi.”+ 16  Lakini malaika wa Yehova akamwambia Manoa, “Hata nikikaa, sitakula chakula chenu; lakini ukipenda unaweza kukitoa kwa Yehova kuwa dhabihu ya kuteketezwa.” Manoa hakujua kwamba mtu huyo alikuwa malaika wa Yehova. 17  Kisha Manoa akamuuliza malaika wa Yehova, “Unaitwa nani,+ ili neno lako litakapotimia tukuheshimu?” 18  Hata hivyo, malaika wa Yehova akamwambia: “Kwa nini unataka kujua jina langu, wakati jina lenyewe ni la ajabu?” 19  Basi Manoa akachukua mwanambuzi na toleo la nafaka, akamtolea Yehova juu ya mwamba. Naye akafanya jambo la kushangaza huku Manoa na mke wake wakitazama. 20  Mwali wa moto ulipokuwa ukipaa kuelekea mbinguni, malaika wa Yehova akapaa katika huo mwali uliotoka katika madhabahu huku Manoa na mke wake wakitazama. Basi wakaanguka chini kifudifudi. 21  Malaika wa Yehova hakumtokea tena Manoa na mke wake. Ndipo Manoa akatambua kwamba huyo alikuwa malaika wa Yehova.+ 22  Kisha Manoa akamwambia hivi mke wake: “Hakika tutakufa, kwa sababu tumemwona Mungu.”+ 23  Lakini mke wake akamwambia, “Kama Yehova angetaka kutuua, hangekubali dhabihu ya kuteketezwa+ na toleo la nafaka kutoka mikononi mwetu, naye hangetuonyesha mambo haya yote, wala hangetuambia mambo haya yote.” 24  Baadaye mwanamke huyo akazaa mwana na kumpa jina Samsoni;+ na mvulana huyo akazidi kukua, na Yehova akaendelea kumbariki. 25  Baada ya muda roho ya Yehova ikaanza kumchochea+ huko Mahane-dani+ kati ya Sora na Eshtaoli.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kutoka tumboni.”
Tnn., “kutoka tumboni.”