Waamuzi 5:1-31

  • Wimbo wa ushindi wa Debora na Baraka (1-31)

    • Nyota zapigana na Sisera (20)

    • Mafuriko ya Mto Kishoni (21)

    • Wanaompenda Yehova wako kama jua (31)

5  Siku hiyo Debora+ pamoja na Baraka+ mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:+   “Kwa sababu ya nywele ndefu* katika Israeli,Kwa sababu ya watu kujitolea,+Msifuni Yehova!   Sikilizeni, enyi wafalme! Tegeni sikio, enyi watawala! Nitamwimbia Yehova. Nitamwimbia sifa* Yehova,+ Mungu wa Israeli.+   Yehova, ulipotoka Seiri,+Ulipopiga mwendo kutoka eneo la Edomu,Dunia ilitikisika, na mbingu zikamwaga maji,Naam, mawingu yakamwaga maji.   Milima iliyeyuka* mbele za uso wa Yehova,+Hata Sinai kutoka mbele za uso wa Yehova,+ Mungu wa Israeli.+   Katika siku za Shamgari+ mwana wa Anathi,Katika siku za Yaeli,+ barabara hazikuwa na watu;Wasafiri walipita vichochoroni.   Wanavijiji katika Israeli walitoweka;Walitoweka, mpaka mimi Debora+ nilipotokea,Mpaka nilipotokea kama mama katika Israeli.+   Walichagua miungu mipya;+Kisha kukawa na vita malangoni.+ Hakukuwa na ngao, wala mkuki,Kati ya wanaume 40,000 katika Israeli.   Moyo wangu uko pamoja na makamanda wa Israeli,+Waliojitolea na kwenda pamoja na watu.+ Msifuni Yehova! 10  Ninyi mnaopanda juu ya punda wa hudhurungi,Ninyi mnaoketi kwenye mazulia bora,Nanyi mnaotembea barabarani,Fikirieni mambo haya! 11  Sauti za wanaoteka maji zilisikika mahali pa kuteka maji;Walisimulia matendo ya uadilifu ya Yehova,Matendo ya uadilifu ya wanavijiji katika Israeli. Kisha watu wa Yehova wakashuka malangoni. 12  Amka, amka, Ee Debora!+ Amka, amka, imba wimbo!+ Inuka, Baraka!+ Wachukue mateka wako, Ee mwana wa Abinoamu! 13  Ndipo waliobaki wakashuka kwenda kwa watu mashuhuri;Watu wa Yehova wakashuka kuja kwangu ili kupigana na wanaume wenye nguvu. 14  Walitoka Efraimu, wale walio bondeni;*Wanakufuata, Ee Benjamini, kati ya watu wako. Kutoka Makiri+ makamanda walishuka,Na kutoka Zabuloni wale wanaobeba fimbo za wanaowaandikisha watu jeshini.* 15  Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora,Walikuwa pamoja naye kama Baraka+ alivyokuwa pamoja naye. Alipelekwa kwa miguu bondeni.*+ Kati ya vikundi vya Rubeni watu waliuchunguza sana moyo wao. 16  Kwa nini uliketi chini kama mnyama aliyelemewa na mizigo,*Ukiwasikiliza wakiwapigia kondoo zumari?+ Kwa kuwa watu walisitasita sana kati ya vikundi vya Rubeni. 17  Watu wa Gileadi walibaki ng’ambo ya Yordani;+Kabila la Dani, kwa nini mliendelea kukaa kwenye meli?+ Watu wa kabila la Asheri waliketi kizembe kando ya bahari,Na kuendelea kukaa bandarini.+ 18  Watu wa Zabuloni walihatarisha uhai wao* karibu wafe;Naftali pia,+ kwenye vilima vilivyo wazi.+ 19  Wafalme walikuja, wakapigana vita;Wafalme wa Kanaani wakapigana+Huko Taanaki, kando ya maji ya Megido.+ Hawakuchukua fedha kama nyara.+ 20  Kutoka mbinguni nyota zilipigana;Kutoka kwenye njia zake zilipigana na Sisera. 21  Mafuriko ya Kishoni yaliwafagilia* mbali,+Mafuriko ya* kale, mafuriko ya* Kishoni. Uliwakanyaga wenye nguvu, Ee nafsi* yangu. 22  Ndipo kwato za farasi zilipokanyaga kwa kishindoFarasi dume walipokimbia kwa kasi.+ 23  ‘Mlaani Merozi,’ akasema malaika wa Yehova,‘Naam, walaani wakaaji wake,Kwa sababu hawakuja kumsaidia Yehova,Kumsaidia Yehova pamoja na mashujaa.’ 24  Amebarikiwa sana Yaeli kati ya wanawake wote+Mke wa Heberi+ Mkeni;Naam, amebarikiwa kuliko wanawake wote wanaokaa katika mahema. 25  Aliomba maji; Yaeli akampa maziwa. Alimpa maziwa ya mgando* katika bakuli kubwa.+ 26  Alinyoosha mkono wake akachukua kigingi cha hema,Na kwa mkono wake wa kulia akachukua nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa,Akampasua na kumtoboa kichwa.+ 27  Alianguka katikati ya miguu yake; alianguka na kulala kimya;Alianguka katikati ya miguu yake akafa;Alipoangukia, hapo ndipo alipolala akiwa ameshindwa. 28  Kupitia dirishani mwanamke aliangalia nje,Mama ya Sisera alitazamakupitia viunzi vya dirisha,‘Mbona gari lake la vita limechelewa kuja? Mbona vishindo vya kwato za farasi wake vimechelewa sana?’+ 29  Wanawake wenye hekima zaidi nyumbani mwake walimjibu;Naam, yeye pia alisema tena na tena moyoni mwake, 30  ‘Bila shaka wanagawana nyara walizopata,Msichana mmoja, wasichana wawili, kwa kila shujaa,Nguo iliyotiwa rangi kwa ajili ya Sisera, nyara ya nguo iliyotiwa rangi,Vazi lililopambwa,* nguo iliyotiwa rangi, mavazi mawili yaliyopambwaKwa ajili ya shingo za waliochukua nyara.’ 31  Maadui wako wote na waangamie,+ Ee Yehova,Lakini wanaokupenda na wawe kama jua linalochomoza katika utukufu wake.” Na nchi ikawa na amani* kwa miaka 40.+

Maelezo ya Chini

Au “mashujaa waliokuwa na nywele ndefu.”
Au “Nitampigia muziki.”
Au labda, “ilitetemeka.”
Au “nchi tambarare ya chini.”
Au labda, “walio na vifaa vya mwandishi.”
Au “nchi tambarare ya chini.”
Au “Kwa nini uliketi kati ya mizigo miwili.”
Au “walidharau nafsi zao.“
Au “Kijito cha.”
Angalia Kamusi.
Au “kijito cha.”
Au “Kijito cha Kishoni kiliwafagilia.”
Au “alimpa mtindi.”
Yaani, “vazi lililotariziwa.”
Tnn., “ikapumzika.”