Waamuzi 7:1-25

  • Gideoni na wanaume 300 (1-8)

  • Jeshi la Gideoni lawashinda Wamidiani (9-25)

    • “Upanga wa Yehova na wa Gideoni!” (20)

    • Kambi ya Wamidiani yachanganyikiwa (21, 22)

7  Ndipo Yerubaali, yaani, Gideoni,+ na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaamka mapema na kupiga kambi karibu na Chemchemi ya Harodi, nayo kambi ya Wamidiani ilikuwa bondeni* upande wa kaskazini wa kambi yao karibu na kilima cha More.  Yehova akamwambia Gideoni, “Watu ulio nao ni wengi sana kwangu mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao.+ Waisraeli wasije wakajigamba mbele zangu wakisema, ‘Mkono wangu mwenyewe uliniokoa.’+  Sasa tafadhali, watangazie hivi watu wote: ‘Mtu yeyote anayeogopa na kutetemeka, arudi nyumbani.’”+ Basi Gideoni akawajaribu kwa maneno hayo. Ndipo watu 22,000 wakarudi nyumbani, wakabaki watu 10,000.  Lakini Yehova akamwambia hivi Gideoni: “Watu hawa bado ni wengi sana. Wapeleke kwenye maji ili niwajaribu kwa ajili yako. Mtu yeyote nitakayekuambia, ‘Huyu ataenda pamoja nawe,’ ataenda pamoja nawe, lakini yeyote nitakayekwambia, ‘Huyu hataenda pamoja nawe,’ basi hataenda.”  Basi Gideoni akawapeleka watu kwenye maji. Kisha Yehova akamwambia Gideoni, “Watenganishe watu wote wanaoramba maji kama mbwa anavyoramba na watu wanaopiga magoti kunywa maji.”  Wale waliochota maji kwa mikono yao na kuyaramba walikuwa wanaume 300. Lakini wengine wote walipiga magoti walipokunywa maji.  Sasa Yehova akamwambia hivi Gideoni: “Nitawatumia wanaume hawa 300 walioramba maji kuwaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mikononi mwako.+ Lakini waambie wengine wote warudi nyumbani.”  Kwa hiyo wakachukua vyakula na pembe* za wanaume hao Waisraeli, kisha Gideoni akawaambia wote warudi nyumbani, akabaki na wale 300 peke yao. Kambi ya Wamidiani ilikuwa upande wa chini bondeni.+  Usiku huo, Yehova akamwambia hivi: “Nenda uishambulie kambi, kwa maana nimeitia mikononi mwako.+ 10  Lakini ikiwa unaogopa kuishambulia, nenda kwanza kambini na Pura mtumishi wako. 11  Sikiliza wanayosema, nawe utapata ujasiri wa* kuwashambulia.” Ndipo yeye na Pura mtumishi wake wakashuka mpaka ukingoni mwa kambi hiyo ya kijeshi. 12  Wamidiani na Waamaleki na watu wote wa Mashariki+ walikuwa wamejaa bondeni nao walikuwa wengi kama nzige, na ngamia wao hawangeweza kuhesabiwa,+ walikuwa wengi kama chembe za mchanga kwenye ufuo wa bahari. 13  Gideoni alipofika, mtu fulani alikuwa akimsimulia mwenzake ndoto, akisema, “Katika ndoto niliona mkate wa shayiri wa mviringo ukivingirika hadi kwenye kambi ya Wamidiani. Ukalipiga hema kwa nguvu na kuliangusha.+ Naam, ukalipindua hema hilo, likaanguka chini.” 14  Basi mwenzake akasema, “Bila shaka huo ni upanga wa Gideoni+ mwana wa Yoashi, mwanamume Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na kambi yote mikononi mwake.”+ 15  Mara tu Gideoni alipomsikia akisimulia ndoto hiyo na kueleza maana yake,+ akainama chini na kuabudu. Kisha akarudi katika kambi ya Waisraeli na kusema, “Twendeni, kwa kuwa Yehova ameitia kambi ya Wamidiani mikononi mwenu.” 16  Basi akawagawa wale wanaume 300 katika vikosi vitatu na kuwapa wote pembe*+ na mitungi mikubwa mitupu yenye mienge. 17  Akawaambia, “Nitazameni na kufanya kama tu nitakavyofanya. Nitakapofika kwenye ukingo wa kambi, fanyeni kama nitakavyofanya. 18  Nitakapopiga pembe,* mimi na wote walio pamoja nami, ninyi pia zipigeni pembe* kuizunguka kambi yote na kupaza sauti, ‘Upanga wa Yehova na wa Gideoni!’” 19  Gideoni na wale wanaume 100 waliokuwa pamoja naye wakaja kwenye ukingo wa kambi mwanzoni mwa kesha la katikati ya usiku,* baada tu ya askari walinzi kuanza zamu. Wakazipiga zile pembe*+ na kuivunjavunja ile mitungi mikubwa waliyokuwa wamebeba mikononi mwao.+ 20  Ndipo vile vikosi vitatu vikapiga pembe* na kuivunjavunja ile mitungi mikubwa. Wakashika mienge kwa mikono ya kushoto na zile pembe kwa mikono ya kulia na kuzipiga, wakipaza sauti, “Upanga wa Yehova na wa Gideoni!” 21  Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka ile kambi, na jeshi lote likakimbia huku likipiga kelele.+ 22  Wanaume hao 300 wakaendelea kupiga pembe,* na Yehova akawafanya waanze kuuana wao kwa wao katika kambi yote;+ na jeshi likakimbia hadi Beth-shita, likafika Serera, hadi mpakani mwa Abel-mehola+ karibu na Tabathi. 23  Wanaume Waisraeli wakakusanywa kutoka katika kabila la Naftali, Asheri, na kabila lote la Manase,+ nao wakawafuatia Wamidiani. 24  Gideoni akatuma wajumbe katika eneo lote lenye milima la Efraimu, akisema, “Shukeni mkawashambulie Wamidiani, wazuieni wasivuke vijito vyote vya maji kufikia Beth-bara na pia Yordani.” Basi watu wote wa Efraimu wakakusanyika pamoja, nao wakawazuia kuvuka vijito vyote vya maji kufikia Beth-bara na Yordani. 25  Pia wakawakamata wale wakuu wawili wa Midiani, yaani, Orebu na Zeebu; wakamuua Orebu juu ya mwamba wa Orebu+ na kumuua Zeebu kwenye shinikizo la divai la Zeebu. Wakaendelea kuwafuatia Wamidiani,+ nao wakamletea Gideoni kichwa cha Orebu na cha Zeebu katika eneo la Yordani.

Maelezo ya Chini

Au “nchi tambarare ya chini.”
Au “tarumbeta.”
Tnn., “na mikono yako itakuwa na nguvu za.”
Au “tarumbeta.”
Au “tarumbeta.”
Au “tarumbeta.”
Kuanzia saa 4 hivi usiku hadi saa 8 usiku.
Au “tarumbeta.”
Au “tarumbeta.”
Au “tarumbeta.”