Kwa Waebrania 13:1-25

  • Himizo na salamu za kumalizia (1-25)

    • Msisahau kuwakaribisha wageni (2)

    • Ndoa na iheshimiwe (4)

    • Watiini wale wanaoongoza (7, 17)

    • Kutoa dhabihu ya sifa (15, 16)

13  Upendo wenu wa kindugu na uendelee.+  Msisahau kuwakaribisha wageni,*+ kwa maana kwa kufanya hivyo watu fulani bila kujua waliwakaribisha malaika.+  Wakumbukeni wale walio gerezani,*+ kana kwamba mmefungwa pamoja nao,+ na wale wanaoteswa, kwa kuwa ninyi pia mko katika mwili.*  Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kisiwe na unajisi,+ kwa maana Mungu atawahukumu waasherati* na wazinzi.+  Njia yenu ya maisha iwe bila upendo wa pesa,+ huku mkiridhika na vitu mlivyo navyo.*+ Kwa maana amesema: “Sitakuacha wala kukutupa kamwe.”+  Ili tuwe hodari na kusema: “Yehova* ni msaidizi wangu; sitaogopa. Mwanadamu atanifanya nini?”+  Wakumbukeni wale wanaoongoza kati yenu,+ ambao wamelisema neno la Mungu kwenu, nanyi mnapotafakari matokeo ya mwenendo wao, igeni imani yao.+  Yesu Kristo ni yuleyule jana, leo, na milele.  Msipotoshwe na mafundisho mbalimbali yaliyo mageni, kwa maana ni bora moyo uimarishwe kwa fadhili zisizostahiliwa, bali si kwa vyakula,* ambavyo haviwanufaishi wale wanaojishughulisha navyo.+ 10  Sisi tuna madhabahu ambayo wale wanaofanya utumishi mtakatifu katika hema hawana mamlaka ya kula kilicho juu yake.+ 11  Kwa maana miili ya wanyama ambao kuhani mkuu hupeleka damu yao ndani ya mahali patakatifu kama toleo la dhambi huteketezwa nje ya kambi.+ 12  Kwa hiyo, Yesu pia aliteseka nje ya lango la jiji+ ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.+ 13  Basi, acheni twende kwake nje ya kambi, tukiibeba shutuma aliyoibeba,+ 14  kwa maana hapa hatuna jiji linalodumu, bali tunatafuta kwa bidii lile litakalokuja.+ 15  Kupitia yeye sikuzote na tumtolee Mungu dhabihu ya sifa,+ yaani, tunda la midomo yetu+ ambalo hulitangaza jina lake hadharani.+ 16  Zaidi ya hayo, msisahau kutenda mema na kushiriki vitu vyenu pamoja na wengine,+ kwa maana Mungu hupendezwa na dhabihu kama hizo.+ 17  Watiini wale wanaoongoza kati yenu+ na mnyenyekee,+ kwa maana wanaendelea kuwalinda ninyi* kama wale watakaotoa hesabu,+ ili wafanye hivyo kwa shangwe na si kwa huzuni, kwa maana kufanya hivyo kungewadhuru ninyi. 18  Endeleeni kusali kwa ajili yetu, kwa maana tuna hakika kwamba tuna dhamiri nyoofu,* kwa kuwa tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.+ 19  Lakini hasa ninawahimiza ninyi msali kwamba nirudi kwenu haraka iwezekanavyo. 20  Basi Mungu wa amani, aliyemrudisha kutoka kwa wafu mchungaji mkuu+ wa kondoo, Bwana wetu Yesu, kwa damu ya agano linalodumu milele, 21  awape vifaa vyote vyema ili mfanye mapenzi yake, akitenda ndani yetu kupitia Yesu Kristo mambo yanayopendeza machoni pake, na awe na utukufu milele na milele. Amina. 22  Sasa ninawahimiza, akina ndugu, msikilize kwa subira neno hili la kutia moyo, kwa maana nimewaandikia barua fupi. 23  Ningependa kuwajulisha kwamba ndugu yetu Timotheo ameachiliwa huru. Akija hivi karibuni, nitakuja pamoja naye kuwaona. 24  Wapeni salamu zangu wote wanaoongoza kati yenu na watakatifu wote. Wale walio Italia+ wanawatumia salamu zao. 25  Fadhili zisizostahiliwa na ziwe pamoja nanyi nyote.

Maelezo ya Chini

Au “kuwaonyesha wageni fadhili; kuwa wakarimu.”
Tnn., “waliofungwa; walio katika vifungo.”
Au labda, “kana kwamba mnateseka pamoja nao.”
Angalia Kamusi, “Uasherati.”
Au “vya sasa.”
Yaani, sheria zinazohusu chakula.
Au “kuzilinda nafsi zenu.”
Tnn., “njema.”