Kwa Waebrania 2:1-18

  • Kazia uangalifu zaidi kuliko ilivyo kawaida (1-4)

  • Vitu vyote vimetiishwa kwa Yesu (5-9)

  • Yesu na ndugu zake (10-18)

    • Wakili Mkuu wa wokovu wao (10)

    • Kuhani mkuu mwenye rehema (17)

2  Hiyo ndiyo sababu ni lazima tuyakazie uangalifu zaidi kuliko ilivyo kawaida mambo tuliyosikia,+ ili tusipeperushwe kamwe.+  Kwa maana ikiwa neno lililosemwa kupitia malaika+ lilikuwa hakika, na kila kosa na tendo la kutotii liliadhibiwa kupatana na haki,+  je, sisi tutaponyoka ikiwa tumepuuza wokovu huo mkuu?+ Kwa kuwa ulianza kusemwa kupitia Bwana wetu+ nasi tukathibitishiwa na wale waliomsikia,  huku Mungu akijiunga katika kutoa ushahidi kwa ishara na mambo ya ajabu* na matendo mbalimbali yenye nguvu+ na roho takatifu iliyotolewa kulingana na mapenzi yake.+  Kwa maana dunia inayokaliwa inayokuja,+ ambayo tunazungumza kuihusu hajaitiisha chini ya malaika.  Lakini mahali fulani shahidi mmoja alisema: “Mwanadamu ni nini hivi kwamba unamweka akilini, au mwana wa mtu hivi kwamba unamtunza?+  Ulimfanya awe mdogo kidogo kuliko malaika; ulimvika taji kwa utukufu na heshima, na kumweka juu ya kazi za mikono yako.  Ulivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.”+ Kwa kuvitiisha vitu vyote chini yake,+ Mungu hakuacha kitu chochote kisichotiishwa chini yake.+ Ingawa hivyo, bado hatuoni vitu vyote vikiwa vimetiishwa chini yake.+  Lakini tunamwona Yesu, aliyefanywa kuwa mdogo kidogo kuliko malaika,+ sasa amevikwa taji la utukufu na heshima kwa kupatwa na kifo,+ ili kwa fadhili zisizostahiliwa za Mungu aonje kifo kwa ajili ya kila mtu.+ 10  Kwa maana ilifaa kwamba yule ambaye kwa ajili yake na kupitia kwake vitu vyote vipo, katika kuleta wana wengi kwenye utukufu,+ alipaswa kumfanya Wakili Mkuu wa wokovu wao+ awe mkamilifu kupitia mateso.+ 11  Kwa maana yule anayetakasa na wale wanaotakaswa+ pia wote hutokana na mmoja,+ na kwa sababu hiyo yeye haoni aibu kuwaita ndugu,+ 12  kama anavyosema: “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kutaniko nitakusifu kwa wimbo.”+ 13  Na tena: “Nitamtegemea yeye.”+ Na tena: “Tazama! Mimi na watoto wadogo, ambao Yehova* alinipa.”+ 14  Basi, kwa kuwa “watoto wadogo” ni washiriki wa damu na mwili, vivyo hivyo yeye pia aliyashiriki mambo hayo,+ ili kupitia kifo chake amwangamize yule aliye na uwezo wa kusababisha kifo,+ yaani, Ibilisi,+ 15  na ili awaweke huru* wale wote waliokuwa chini ya utumwa katika maisha yao yote kwa kuogopa kifo.+ 16  Kwa maana kwa kweli yeye hawasaidii malaika, bali anasaidia uzao wa* Abrahamu.+ 17  Kwa hiyo alipaswa kuwa kama “ndugu” zake katika mambo yote,+ ili awe kuhani mkuu mwenye rehema na mwaminifu katika mambo yanayohusiana na Mungu, ili atoe dhabihu ya upatanisho*+ kwa ajili ya dhambi za watu.+ 18  Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteseka alipokuwa akijaribiwa,+ anaweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.+

Maelezo ya Chini

Au “miujiza.”
Au “awakomboe.”
Tnn., “mbegu ya.”
Au “atoe dhabihu ya kufunika dhambi; kufunika dhambi.”