Kwa Waebrania 3:1-19

  • Yesu ni mkuu kuliko Musa (1-6)

    • Vitu vyote vilitengenezwa na Mungu (4)

  • Onyo dhidi ya kukosa imani (7-19)

    • “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake” (7, 15)

3  Kwa hiyo, ndugu watakatifu, washiriki wa mwito* wa mbinguni,+ mfikirieni mtume na kuhani mkuu tunayemkubali*—Yesu.+  Alikuwa mwaminifu kwa Yule aliyemchagua,+ kama vile Musa alivyokuwa pia katika nyumba yote ya Mungu.+  Kwa maana huyo* anastahili utukufu zaidi+ kuliko Musa, kwa kuwa yule anayejenga nyumba ana heshima kuliko nyumba yenyewe.  Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yule aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.  Sasa Musa alikuwa mtumishi mwaminifu katika nyumba yote ya Huyo akiwa ushuhuda* wa mambo ambayo yangesemwa baadaye,  lakini Kristo alikuwa mwaminifu akiwa mwana+ juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba Yake,+ ikiwa kwa kweli tunashikilia imara uhuru wetu wa kusema na tumaini ambalo tunajisifia mpaka mwisho.  Kwa hiyo, kama vile roho takatifu inavyosema,+ “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,  msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama ule wakati wa kusababisha hasira kali, kama siku ile ya jaribu nyikani,+  ambayo mababu zenu waliniweka kwenye jaribu, na kunipima, ingawa waliona matendo yangu kwa miaka 40.+ 10  Ndiyo sababu nilichukizwa na kizazi hiki, nikasema: ‘Wao hupotoka sikuzote katika mioyo yao, nao hawazijui njia zangu.’ 11  Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu: ‘Hawataingia katika pumziko langu.’”+ 12  Jihadharini, akina ndugu, ili moyo mwovu unaokosa imani usisitawi ndani ya yeyote kati yenu kwa kujiondoa kwa Mungu aliye hai;+ 13  lakini endeleeni kutiana moyo kila siku, maadamu inaitwa “Leo,”+ ili yeyote kati yenu asifanywe kuwa mgumu kwa nguvu za udanganyifu za dhambi. 14  Kwa maana kwa kweli tunakuwa washiriki wa* Kristo ikiwa tu tunashikilia imara mpaka mwisho uhakika tuliokuwa nao mwanzoni.+ 15  Kama inavyosemwa, “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama ule wakati wa kusababisha hasira kali.”+ 16  Kwa maana ni nani waliosikia na bado wakamchochea kuwa na hasira kali? Kwa kweli, je, si wale wote waliotoka Misri chini ya Musa?+ 17  Zaidi ya hayo, Mungu alichukizwa na akina nani kwa miaka 40?+ Je, si wale waliotenda dhambi, ambao maiti zao zilianguka nyikani?+ 18  Naye aliapa kwa akina nani kwamba hawataingia katika pumziko lake? Je, si wale waliotenda kwa kutotii? 19  Kwa hiyo tunaona kwamba hawakuingia kwa sababu walikosa imani.+

Maelezo ya Chini

Au “mwaliko.”
Au “tunayemkiri.”
Yaani, Yesu.
Au “ushahidi.”
Au “tunakuwa na ushirika na.”