Kwa Waefeso 1:1-23

  • Salamu (1, 2)

  • Baraka za kiroho (3-7)

  • Kuvikusanya vitu vyote katika Kristo (8-14)

    • “Usimamizi” katika nyakati zilizowekwa (10)

    • Kutiwa muhuri kwa roho kama “rehani ya mapema” (13, 14)

  • Paulo amshukuru Mungu kwa sababu ya imani ya Waefeso na kusali kwa ajili yao (15-23)

1  Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu, kwa watakatifu walio huko Efeso+ na walio waaminifu katika muungano na Kristo Yesu:  Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.  Asifiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwa kuwa ametubariki kwa kila baraka ya kiroho katika mahali pa kimbingu katika muungano na Kristo,+  kama alivyotuchagua tuwe katika muungano naye* kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu, ili tuwe watakatifu na bila dosari+ mbele zake katika upendo.  Kwa maana alituagiza awali+ tufanywe kuwa wanawe mwenyewe+ kupitia Yesu Kristo, kulingana na mapenzi yake mema na kusudi lake,+  kwa sifa ya fadhili zake zisizostahiliwa+ zenye utukufu alizotupatia kwa fadhili kupitia mpendwa wake.+  Kupitia kwake tunaachiliwa huru kwa njia ya fidia kupitia damu ya huyo,+ ndiyo, msamaha wa makosa yetu,+ kulingana na utajiri wa fadhili zake zisizostahiliwa.  Alituzidishia fadhili zisizostahiliwa katika hekima yote na uelewaji,*  kwa kutujulisha siri takatifu+ ya mapenzi yake. Ni kulingana na mapenzi yake mema aliyokusudia mwenyewe 10  kwa ajili ya usimamizi* kwenye nyakati kamili zilizowekwa, kukusanya pamoja vitu vyote katika Kristo, vitu vilivyo mbinguni na vitu vilivyo duniani.+ Ndiyo, katika yeye 11  ambaye tuko katika muungano naye na tulihesabiwa kuwa warithi,+ kwa kuwa tuliagizwa awali kulingana na kusudi la yule anayetimiza mambo yote kama anavyoamua kulingana na mapenzi yake, 12  ili sisi tulio wa kwanza kumtumaini Kristo tutumikie kwa ajili ya sifa ya utukufu wake. 13  Lakini ninyi pia mlimtumaini baada ya kulisikia neno la kweli, habari njema kuhusu wokovu wenu. Baada ya kuamini, mlitiwa muhuri+ kupitia kwake kwa roho takatifu iliyoahidiwa, 14  ambayo ni rehani ya mapema* ya urithi wetu,+ kwa kusudi la kuachilia huru mali ya Mungu mwenyewe+ kupitia fidia,+ kwa sifa yake yenye utukufu. 15  Hiyo ndiyo sababu mimi pia, kwa kuwa nimesikia kuhusu imani mliyo nayo katika Bwana Yesu na upendo mnaowaonyesha watakatifu wote, 16  siachi kamwe kutoa shukrani kwa ajili yenu. Ninaendelea kuwataja katika sala zangu, 17  ili Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape roho ya hekima na ya ufunuo katika ujuzi sahihi kumhusu.+ 18  Ameyatia nuru macho ya moyo wenu, ili mjue tumaini alilowaitia, utajiri wenye utukufu ambao amewawekea watakatifu kuwa urithi,+ 19  na jinsi nguvu zake kutuelekea sisi waamini zilivyo kuu zaidi.+ Ni kulingana na utendaji wa uwezo wa nguvu zake, 20  ambao aliutumia kuhusiana na Kristo alipomfufua kutoka kwa wafu na kumketisha kwenye mkono wake wa kuume+ katika mahali pa kimbingu, 21  juu kuliko kila serikali na mamlaka na nguvu na utawala na kila jina linalotajwa,+ si katika mfumo huu wa mambo* tu, bali pia katika ule unaokuja. 22  Alivitiisha pia vitu vyote chini ya miguu yake+ na kumfanya kuwa kichwa juu ya vitu vyote kuhusiana na kutaniko,+ 23  ambalo ni mwili wake,+ ujazo wake anayejaza vitu vyote katika vyote.

Maelezo ya Chini

Yaani, pamoja na Kristo.
Au “akili nzuri.”
Au “kusimamia mambo.”
Au “malipo ya awali; uthibitisho (dhamana) wa kile kitakachokuja.”
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”