Kwa Waefeso 3:1-21

  • Siri takatifu ingetia ndani Watu wa Mataifa (1-13)

    • Watu wa Mataifa ni warithi wenzi pamoja na Kristo (6)

    • Kusudi la Mungu la milele (11)

  • Sala kwa ajili ya Waefeso ili wapate hekima (14-21)

3  Kwa sababu hii, mimi Paulo, mfungwa+ wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, watu wa mataifa—  ikiwa, kwa kweli, mmesikia kuhusu usimamizi+ wa fadhili zisizostahiliwa za Mungu ambao nilipewa kwa ajili yenu,  kwamba nilijulishwa siri takatifu kupitia ufunuo, kama vile nilivyoandika kwa ufupi hapo mwanzoni.  Basi mnaposoma jambo hili, mnaweza kuona jinsi ninavyoelewa siri takatifu+ ya Kristo.  Katika vizazi vingine wanadamu hawakujulishwa siri hii kama vile ambavyo sasa imefunuliwa kwa mitume wake watakatifu na manabii kupitia roho,+  yaani, kwamba watu wa mataifa, katika muungano na Kristo Yesu na kupitia habari njema, wawe warithi na viungo vya mwili uleule+ na washiriki wa ahadi pamoja nasi.  Mimi nilikuja kuwa mhudumu wa hilo kulingana na zawadi ya bure ya Mungu ya fadhili zisizostahiliwa nilizopewa kupitia utendaji wa nguvu zake.+  Mimi, niliye mdogo kuliko aliye mdogo zaidi kati ya watakatifu wote,+ nilipewa fadhili hizi zisizostahiliwa,+ ili niwatangazie mataifa habari njema kuhusu utajiri usiopimika wa Kristo  na kufanya kila mtu aone usimamizi wa siri takatifu+ ambayo imefichwa kwa vizazi na vizazi katika Mungu, aliyeumba vitu vyote. 10  Ilikuwa hivyo ili sasa, kupitia kutaniko,+ serikali na mamlaka zilizo mahali pa kimbingu zijulishwe hekima ya Mungu inayoonekana kwa njia nyingi sana.+ 11  Hii ni kulingana na kusudi la milele alilofanyiza kuhusiana na Kristo,+ Yesu Bwana wetu, 12  ambaye kupitia kwake tuna uhuru huu wa kusema na uhuru wa kukaribia+ tukiwa na uhakika kupitia imani yetu kwake. 13  Basi ninawaomba msife moyo kwa sababu ya dhiki zangu kwa ajili yenu, kwa maana zinamaanisha utukufu kwenu.+ 14  Kwa sababu hiyo ninampigia Baba magoti, 15  ambaye kila familia mbinguni na duniani hupata jina kutoka kwake. 16  Ninasali kwamba awawezeshe kulingana na wingi wa utukufu wake ili mfanywe kuwa na uwezo katika mtu mliye kwa ndani,+ mkiwa na nguvu kupitia roho yake, 17  na kupitia imani yenu muwe na Kristo akikaa katika mioyo yenu kwa upendo.+ Iweni na mizizi+ na kuimarishwa juu ya ule msingi,+ 18  ili pamoja na watakatifu wote mweze kufahamu kikamili upana na urefu na kimo na kina, 19  na kuujua upendo wa Kristo,+ unaozidi ujuzi, ili mjawe na ujazo wote ambao Mungu hutoa. 20  Basi kwa yule anayeweza, kulingana na nguvu zake zinazotenda ndani yetu,+ kufanya kwa wingi zaidi kupita mambo yote tunayoomba au tunayofikiri,+ 21  na awe na utukufu kupitia kutaniko na kupitia Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina.

Maelezo ya Chini