Kwa Wafilipi 1:1-30

  • Salamu (1, 2)

  • Shukrani kwa Mungu; Sala ya Paulo (3-11)

  • Habari njema yasonga mbele licha ya matatizo (12-20)

  • Kuishi ni Kristo, kifo ni faida (21-26)

  • Jiendesheni kwa njia inayostahili habari njema (27-30)

1  Paulo na Timotheo, watumwa wa Kristo Yesu, kwa watakatifu wote katika muungano na Kristo Yesu walio huko Filipi,+ pamoja na waangalizi na watumishi wa huduma:+  Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.  Sikuzote ninamshukuru Mungu wangu ninapowakumbuka ninyi  katika dua zangu zote kwa ajili yenu nyote. Ninatoa kila dua kwa shangwe,+  kwa sababu ya mchango ambao mmeutoa kwa ajili ya* habari njema tangu siku ya kwanza mpaka sasa.  Kwa maana nina uhakika kuhusu jambo hili, kwamba yule aliyeanzisha kazi njema ndani yenu ataikamilisha+ kufikia siku ya Kristo Yesu.+  Ni sawa kwangu kufikiri hivyo kuwahusu ninyi nyote, kwa sababu mko katika moyo wangu, ninyi mlio washiriki pamoja nami katika fadhili zisizostahiliwa katika vifungo vyangu vya gereza+ na katika kuitetea na kuithibitisha kisheria habari njema.+  Kwa maana Mungu ni shahidi wangu kuhusu jinsi ninavyotamani kuwaona ninyi nyote kwa upendo mwororo kama alio nao Kristo Yesu.  Na hili ndilo ninaloendelea kusali, kwamba upendo wenu uwe mwingi zaidi na zaidi+ pamoja na ujuzi sahihi+ na utambuzi kamili;+ 10  kwamba mhakikishe mambo muhimu zaidi,+ ili muwe bila kasoro na msiwe mkiwakwaza wengine+ mpaka siku ya Kristo; 11  na kwamba mjazwe tunda la uadilifu, ambalo ni kupitia Yesu Kristo,+ kwa utukufu na sifa kwa Mungu. 12  Basi ninataka mjue, akina ndugu, kwamba hali yangu kwa kweli imesaidia kuendeleza habari njema, 13  hivi kwamba vifungo vyangu vya gereza+ kwa ajili ya Kristo vimejulikana wazi+ kati ya Walinzi wote wa Mfalme na watu wengine wote. 14  Sasa akina ndugu wengi katika Bwana wamekuwa na uhakika kwa sababu ya vifungo vyangu vya gereza, nao wanaonyesha uhodari mwingi wa kulisema neno la Mungu bila woga. 15  Ni kweli, wengine wanamhubiri Kristo kwa wivu na kushindana, lakini wengine kwa nia njema. 16  Hao wa mwisho wanamtangaza Kristo kutokana na upendo, kwa maana wanajua kwamba nimechaguliwa ili kuitetea habari njema;+ 17  lakini wale wa kwanza hufanya hivyo kutokana na ugomvi, si kwa kusudi safi, kwa maana wanataka kunisababishia dhiki katika vifungo vyangu vya gereza. 18  Matokeo ni nini? Ni kwamba katika kila njia, iwe ni kwa unafiki au ni kwa ukweli, Kristo anatangazwa, nami ninashangilia kuhusu jambo hilo. Kwa kweli, nitaendelea pia kushangilia, 19  kwa maana ninajua hilo litanisaidia kupata wokovu kupitia dua yenu+ na kwa msaada wa roho ya Yesu Kristo.+ 20  Hilo linapatana na tarajio langu lenye hamu na tumaini kwamba sitaona aibu kwa njia yoyote, bali kwamba kwa uhuru wote wa kusema, sasa Kristo, kama sikuzote hapo mwanzoni, atatukuzwa kupitia mwili wangu, iwe ni kupitia uzima au kupitia kifo.+ 21  Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo+ na kifo ni faida.+ 22  Basi ikiwa nitaendelea kuishi katika mwili, hilo ni tunda la kazi yangu; hata hivyo, mimi sisemi kile nitakachochagua. 23  Ninakabiliwa na mambo haya mawili, kwa maana ninatamani kufunguliwa na kuwa pamoja na Kristo,+ ambako, kwa hakika, ni bora zaidi.+ 24  Hata hivyo, ni muhimu zaidi kwangu kubaki katika mwili kwa ajili yenu. 25  Basi, nikiwa na uhakika wa jambo hili, ninajua nitabaki na kuendelea pamoja nanyi nyote ili msonge mbele na muwe na shangwe katika imani, 26  ili kwa sababu yangu furaha yenu ifurike katika Kristo Yesu nitakapokuwa tena pamoja nanyi. 27  Ila tu jiendesheni* kwa njia inayostahili habari njema kumhusu Kristo,+ ili kama nitakuja kuwaona au nisipokuja, nisikie kuwahusu na nisikie kwamba mnasimama imara katika roho moja, kwa nafsi moja,*+ mkijitahidi pamoja kwa ajili ya imani ya habari njema, 28  bila kuogopeshwa kamwe na wapinzani wenu. Jambo hili ni uthibitisho wa uharibifu+ kwao, lakini wa wokovu kwenu;+ na hili linatoka kwa Mungu. 29  Kwa maana mlipewa pendeleo kwa ajili ya Kristo, si muwe tu na imani katika yeye, bali pia mteseke kwa ajili yake.+ 30  Kwa maana mna pambano kama lile mliloona nikikabili,+ ambalo mnasikia kwamba bado ninakabili.

Maelezo ya Chini

Au “kwa sababu mmeshiriki kuendeleza.”
Au “jiendesheni kama raia.”
Au “kwa nia moja.”