Kwa Wafilipi 2:1-30

  • Unyenyekevu wa Kikristo (1-4)

  • Unyenyekevu wa Kristo na kupandishwa cheo (5-11)

  • Fanyieni kazi wokovu wenu wenyewe (12-18)

    • Kuangaza kama mianga (15)

  • Kumtuma Timotheo na Epafrodito (19-30)

2  Basi, ikiwa kuna jambo lolote la kutia moyo katika Kristo, ikiwa kuna faraja yoyote ya upendo, ikiwa kuna ushirika wowote wa kiroho,* ikiwa kuna upendo mwororo na huruma zozote,  fanyeni shangwe yangu ijae kwa kuwa na akili ileile na kuwa na upendo uleule, mkiwa mmeunganishwa kabisa,* mkiwa na wazo moja akilini.+  Msifanye jambo lolote kwa ugomvi+ au kwa kujisifu,+ bali kwa unyenyekevu* mwaone wengine kuwa bora kuliko ninyi,+  huku mkiangalia, si faida zenu wenyewe,+ bali pia faida za wengine.+  Iweni na mtazamo huu wa akili ambao pia Kristo Yesu alikuwa nao,+  ambaye, ingawa alikuwa katika umbo la Mungu,+ hakufikiria kufanya unyakuzi, yaani, kwamba yeye awe sawa na Mungu.+  Hapana, bali alijiondolea hali yake na kuchukua umbo la mtumwa+ na kuwa mwanadamu.*+  Zaidi ya hayo, alipokuja akiwa mwanadamu,* alijinyenyekeza na kuwa mtiifu mpaka kifo,+ ndiyo, kifo juu ya mti wa mateso.*+  Kwa sababu hiyo, Mungu alimpandisha kwenye cheo cha juu zaidi+ na kumpa kwa fadhili jina lililo juu kuliko kila jina lingine,+ 10  ili katika jina la Yesu kila goti lipigwe—la wale walio mbinguni na wale walio duniani na wale walio chini ya ardhi+ 11  na kila ulimi ukiri waziwazi kwamba Yesu Kristo ni Bwana+ kwa utukufu wa Mungu Baba. 12  Kwa hiyo, wapendwa wangu, kama vile ambavyo mmekuwa mkitii sikuzote, si wakati tu ninapokuwapo, bali kwa utayari zaidi sasa nisipokuwapo, endeleeni kuufanyia kazi wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka. 13  Kwa maana Mungu ndiye ambaye kwa mapenzi yake mema anawachochea, na kuwapa hamu na nguvu za kutenda. 14  Endeleeni kufanya mambo yote bila kunung’unika+ wala kubishana,+ 15  ili mje kuwa bila lawama wala hatia, watoto wa Mungu+ wasio na dosari katikati ya kizazi kilicho kombo na kilichopotoka,+ ambao kati yao mnaangaza kama mianga katika ulimwengu,+ 16  mkiendelea kulishika sana neno la uzima.+ Ndipo nitakuwa na sababu ya kushangilia katika siku ya Kristo, nikijua kwamba sikukimbia bure wala sikufanya kazi kwa bidii bure. 17  Hata hivyo, hata ikiwa ninamiminwa kama toleo la kinywaji+ juu ya dhabihu+ na utumishi mtakatifu* ambao imani yenu imewaongoza, ninafurahi na kushangilia pamoja nanyi nyote. 18  Vivyo hivyo, ninyi pia mnapaswa kufurahi na kushangilia pamoja nami. 19  Sasa ninatumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo+ kwenu upesi, ili nitiwe moyo nitakapopata habari kuwahusu ninyi. 20  Kwa maana sina mtu mwingine aliye na mwelekeo kama wake atakayejali kwa unyoofu mahangaiko yenu. 21  Kwa maana wengine wote wanatafuta faida zao wenyewe, si za Yesu Kristo. 22  Lakini ninyi mnajua jinsi alivyojithibitisha mwenyewe, kwamba kama mtoto+ na baba yake alitumikia pamoja nami katika kuendeleza habari njema. 23  Kwa hiyo, yeye ndiye ninayetumaini kumtuma mara tu nitakapoona jinsi mambo yangu yatakavyokuwa. 24  Kwa kweli, nina uhakika katika Bwana kwamba mimi mwenyewe pia nitakuja hivi karibuni.+ 25  Lakini sasa ninaona ni lazima nimtume kwenu Epafrodito, ndugu yangu na mfanyakazi mwenzangu na mwanajeshi mwenzangu, na mjumbe wenu na mtumishi wa kibinafsi kwa ajili ya uhitaji wangu,+ 26  kwa kuwa anatamani kuwaona ninyi nyote naye amehuzunika kwa sababu mlisikia alikuwa mgonjwa. 27  Kwa hakika, alikuwa mgonjwa karibu kufa; lakini Mungu alimhurumia. Kwa kweli, hakumhurumia yeye tu, bali mimi pia, ili nisipatwe na huzuni juu ya huzuni. 28  Kwa hiyo ninamtuma haraka bila kukawia, ili mtakapomwona, mshangilie tena, nami nipunguziwe wasiwasi. 29  Basi mkaribisheni kama ilivyo desturi katika Bwana kwa shangwe yote, nanyi mwendelee kuwaheshimu sana watu wa namna hiyo,+ 30  kwa kuwa alikaribia kufa kwa sababu ya kazi ya Kristo,* akihatarisha uhai wake,* ili ajazie kutokuwapo kwenu hapa kunitolea utumishi wa kibinafsi.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ushirika wowote wa roho.”
Au “mkiwa mmeunganishwa katika nafsi.”
Au “unyenyekevu wa akili.”
Tnn., “na kuwa kama wanadamu.”
Tnn., “alipopatikana katika umbo la mwanadamu.”
Angalia Kamusi.
Au “utumishi wa watu wote.”
Au labda, “kazi ya Bwana.”
Au “akiihatarisha nafsi yake.”