Kwa Wagalatia 1:1-24

  • Salamu (1-5)

  • Hakuna habari njema nyingine (6-9)

  • Habari njema aliyohubiri Paulo inatoka kwa Mungu (10-12)

  • Jinsi Paulo alivyogeuka na kazi yake ya mwanzoni (13-24)

1  Paulo, mtume, si kutokana na wanadamu wala kupitia mwanadamu, bali kupitia Yesu Kristo+ na Mungu Baba,+ aliyemfufua kutoka kwa wafu,  na ndugu wote walio pamoja nami, kwa makutaniko ya Galatia:  Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.  Alijitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu+ ili atuokoe kutoka katika mfumo huu mwovu wa mambo,*+ kulingana na mapenzi ya Mungu na Baba yetu,+  na awe na utukufu milele na milele. Amina.  Ninashangaa kwamba mnageuzwa* upesi kutoka kwa Yule aliyewaita kwa fadhili zisizostahiliwa za Kristo nanyi mnaenda kwenye habari njema ya aina nyingine.+  Si kwamba kuna habari njema nyingine; lakini kuna watu fulani wanaowataabisha ninyi+ na kutaka kupotosha habari njema kuhusu Kristo.  Hata hivyo, ikiwa sisi au malaika kutoka mbinguni tungewatangazia kuwa habari njema jambo tofauti na habari njema tuliyowatangazia, mtu huyo na alaaniwe.  Kama tulivyosema awali, sasa ninasema tena, Yeyote anayewatangazia kuwa habari njema jambo tofauti na lile mlilopokea, na alaaniwe. 10  Kwa kweli, je, sasa ninajaribu kuwashawishi wanadamu au Mungu? Au je, ninajaribu kuwapendeza wanadamu? Kama bado ningekuwa ninawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo. 11  Akina ndugu, ningependa mjue kwamba habari njema niliyowatangazia haitokani na wanadamu;+ 12  kwa kuwa sikuipokea kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa, bali ilikuwa kupitia ufunuo wa Yesu Kristo. 13  Bila shaka, mlisikia kuhusu mwenendo wangu wa zamani katika dini ya Kiyahudi,+ kwamba niliendelea kulitesa sana* kutaniko la Mungu na kuliangamiza;+ 14  nami nilikuwa nikifanya maendeleo makubwa katika dini ya Kiyahudi kuliko watu wengi wa umri wangu katika taifa langu, kwa maana nilikuwa na bidii zaidi kwa ajili ya mapokeo ya baba zangu.+ 15  Lakini Mungu, aliyenitenga tangu tumbo la uzazi la mama yangu na kuniita kupitia fadhili zake zisizostahiliwa,+ alipoona vema 16  kumfunua Mwana wake kupitia kwangu, ili niyatangazie mataifa habari njema kumhusu,+ sikushauriana papo hapo na mwanadamu yeyote;* 17  wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilienda Arabia, kisha nikarudi Damasko.+ 18  Miaka mitatu baadaye, nilipanda kwenda Yerusalemu+ kumtembelea Kefa,*+ nami nikakaa pamoja naye siku 15. 19  Lakini sikuwaona wale mitume wengine, isipokuwa Yakobo+ ndugu ya Bwana. 20  Basi kuhusu mambo ninayowaandikia, ninawahakikishia mbele za Mungu kwamba sisemi uwongo. 21  Baada ya hapo nikaenda katika maeneo ya Siria na Kilikia.+ 22  Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makutaniko ya Yudea yaliyokuwa katika muungano na Kristo. 23  Walikuwa tu wakisikia: “Yule mtu ambaye alitutesa+ hapo zamani sasa anatangaza habari njema kuhusu imani ambayo hapo zamani aliiangamiza.”+ 24  Basi wakaanza kumtukuza Mungu kwa sababu yangu.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Au “mnaondolewa.”
Tnn., “mpaka hatua inayozidi mno.”
Tnn., “na mwili na damu.”
Pia anaitwa Petro.