Kwa Wagalatia 4:1-31

  • Si watumwa tena, bali ni wana (1-7)

  • Paulo awahangaikia Wagalatia (8-20)

  • Hagari na Sara: maagano mawili (21-31)

    • Yerusalemu lililo juu, mama yetu, liko huru (26)

4  Basi ninasema kwamba mrithi akiwa bado mtoto mdogo, hayuko tofauti na mtumwa, ingawa ndiye bwana wa vitu vyote,  bali yuko chini ya watunzaji na wasimamizi mpaka siku iliyopangwa mapema na baba yake.  Vivyo hivyo, sisi pia tulipokuwa watoto, tulikuwa watumwa wa mambo ya msingi ya ulimwengu.+  Lakini wakati kamili ulipofika, Mungu alimtuma Mwana wake, aliyezaliwa na mwanamke+ na pia alikuwa chini ya sheria,+  ili awaachilie huru kwa kuwanunua wale walio chini ya sheria,+ ili sisi tufanywe kuwa wana.+  Sasa kwa sababu ninyi ni wana, Mungu ametuma roho+ ya Mwana wake ndani ya mioyo yetu,+ nayo hupaza sauti: “Abba,* Baba!”+  Kwa hiyo, wewe si mtumwa tena bali ni mwana; na ikiwa ni mwana, basi wewe pia ni mrithi kupitia Mungu.+  Hata hivyo, wakati hamkumjua Mungu, mlikuwa watumwa wa miungu ya uwongo.*  Lakini sasa kwa kuwa mmemjua Mungu au, kwamba sasa Mungu amewajua ninyi, kwa nini mnarudi tena kwenye mambo ya msingi yaliyo dhaifu+ na yasiyo na maana na kutaka kuyatumikia tena?+ 10  Mnashika kwa uangalifu sana siku na miezi+ na majira na miaka. 11  Ninaogopa kwa ajili yenu, isiwe kwamba nimepoteza jitihada zangu kwenu. 12  Ninawaomba akina ndugu, iweni kama nilivyo, kwa sababu mimi pia nilikuwa kama mlivyo.+ Hamkunikosea. 13  Lakini mnajua ni kwa sababu ya ugonjwa wa kimwili kwamba nilipata nafasi yangu ya kwanza ya kuwatangazia habari njema. 14  Na ingawa hali yangu ya kimwili ilikuwa jaribu kwenu, hamkunitendea kwa dharau au kunichukia;* bali mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama Kristo Yesu. 15  Furaha mliyokuwa nayo iko wapi? Kwa maana ninawatolea ushahidi kwamba, kama ingewezekana, mngeyang’oa macho yenu na kunipa.+ 16  Hivyo basi, je, nimekuwa adui yenu kwa sababu ninawaambia ukweli? 17  Wanawatafuta kwa bidii ili muwafuate, bali si kwa kusudi zuri; wanataka kuwatenganisha nami, ili muwafuate wao kwa bidii. 18  Hata hivyo, ni vema sikuzote kwa mtu kuwatafuta ninyi kwa bidii kwa kusudi zuri bali si wakati tu ninapokuwa pamoja nanyi, 19  watoto wangu wadogo,+ ambao tena nina uchungu wa kuwazaa mpaka Kristo atakapofanyizwa* ndani yenu. 20  Ninatamani ningekuwa pamoja nanyi sasa hivi na kuzungumza kwa njia tofauti, kwa sababu ninawahangaikia ninyi. 21  Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, Je, hamsikii Sheria? 22  Kwa mfano, imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wawili, mmoja kupitia kijakazi+ na mwingine kupitia mwanamke aliye huru;+ 23  lakini yule wa kijakazi kwa kweli alizaliwa kupitia njia ya asili*+ na yule mwingine wa mwanamke aliye huru kupitia ahadi.+ 24  Mambo haya yanaweza kumaanisha tukio la mfano; kwa maana wanawake hawa wanamaanisha maagano mawili, moja kutoka Mlima Sinai,+ ambalo huzaa watoto kwa ajili ya utumwa na ambalo ni Hagari. 25  Basi Hagari anamaanisha Sinai,+ mlima ulio Arabia, naye analingana na Yerusalemu la leo, kwa maana liko katika utumwa pamoja na watoto wake. 26  Lakini Yerusalemu la juu liko huru, nalo ni mama yetu. 27  Kwa maana imeandikwa: “Furahi, wewe mwanamke tasa usiyezaa; piga vigelegele vya shangwe, wewe mwanamke usiye na uchungu wa kuzaa; kwa maana watoto wa mwanamke aliye ukiwa ni wengi kuliko wa yule aliye na mume.”+ 28  Basi, akina ndugu, ninyi ni watoto wa ahadi kama Isaka alivyokuwa.+ 29  Lakini kama ilivyokuwa wakati huo, yule aliyezaliwa kupitia njia ya asili* alianza kumtesa yule aliyezaliwa kupitia roho,+ ndivyo ilivyo pia sasa.+ 30  Hata hivyo, andiko linasema nini? “Mfukuze kijakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa kijakazi hatakuwa mrithi kamwe pamoja na mwana wa mwanamke aliye huru.”+ 31  Basi, akina ndugu, sisi si watoto wa kijakazi, bali wa yule mwanamke aliye huru.

Maelezo ya Chini

Neno la Kiebrania au Kiaramu linalomaanisha “Ee Baba!”
Tnn., “ ile ambayo kwa kweli si miungu.”
Au “kunitemea mate.”
Au “atakapoumbwa.”
Tnn., “kulingana na mwili.”
Tnn., “kulingana na mwili.”