Kwa Wagalatia 5:1-26

  • Uhuru wa Kikristo (1-15)

  • Kutembea kwa roho (16-26)

5  Kristo alituweka huru ili tuwe na uhuru kama huo. Kwa hiyo, simameni imara,+ na msijiache mfungwe tena katika nira ya utumwa.+  Oneni! Mimi, Paulo, ninawaambia kwamba mkitahiriwa, Kristo hatakuwa na faida kwenu.+  Tena ninatoa ushahidi kwa kila mtu anayetahiriwa kwamba yuko chini ya wajibu wa kuitimiza Sheria yote.+  Mmetenganishwa na Kristo, ninyi mnaojaribu kutangazwa kuwa waadilifu kupitia sheria;+ mmeanguka kutoka kwenye fadhili zake zisizostahiliwa.  Kwa upande wetu, kupitia kwa roho tunasubiri kwa hamu uadilifu uliotumainiwa unaotokana na imani.  Kwa maana katika muungano na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutotahiriwa hakuna faida yoyote,+ bali imani inayotenda kupitia upendo ina faida.  Mlikuwa mnakimbia vema.+ Ni nani aliyewazuia kuendelea kuitii kweli?  Ushawishi wa namna hii hautoki kwa Yule anayewaita ninyi.  Chachu kidogo huchachisha donge zima.+ 10  Nina uhakika kwamba ninyi mlio katika muungano na Bwana+ hamtakuja kufikiria jambo tofauti; lakini yule anayewasababishia taabu,+ hata iwe ni nani, atapokea hukumu anayostahili. 11  Na mimi, akina ndugu, ikiwa bado ninahubiri kuhusu kutahiriwa, kwa nini bado ninateswa? Ikiwa ndivyo, kikwazo cha mti wa mateso*+ kimeondolewa. 12  Ningependa watu wanaojaribu kuwaangusha ninyi wajihasi wenyewe.* 13  Akina ndugu, mliitwa kwenye uhuru; lakini msiutumie uhuru huo kama nafasi ya kufuatilia tamaa za mwili,+ bali mtumikiane kupitia upendo.+ 14  Kwa maana Sheria nzima imetimizwa* katika amri hii moja: “Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”+ 15  Lakini, ikiwa mnaendelea kuumana na kuraruana,+ jihadharini ili msije mkaangamizana.+ 16  Lakini ninasema, Endeleeni kutembea kwa roho+ nanyi hamtatenda kwa tamaa za mwili hata kidogo.+ 17  Kwa maana mwili katika tamaa yake unapingana na roho, na roho inapingana na mwili; vitu hivyo vinapingana, hivi kwamba hamfanyi mambo mnayotaka kufanya.+ 18  Isitoshe, ikiwa mnaongozwa na roho, ninyi hamko chini ya sheria. 19  Sasa matendo ya mwili huonekana wazi, nayo ni uasherati,*+ uchafu, mwenendo mpotovu,*+ 20  ibada ya sanamu, kuwasiliana na roho,*+ chuki, mizozo, wivu, milipuko ya hasira, migogoro, migawanyiko, madhehebu, 21  husuda, ulevi,+ karamu zenye vurugu, * na mambo kama hayo.+ Ninawaonya mapema kuhusu mambo hayo, kama vile nilivyowaonya tayari, kwamba wale wanaozoea kufanya mambo hayo hawataurithi Ufalme wa Mungu.+ 22  Kwa upande mwingine, tunda la roho* ni upendo, shangwe, amani, subira,* fadhili, wema,+ imani, 23  upole, kujizuia.*+ Hakuna sheria dhidi ya mambo hayo. 24  Isitoshe, wale walio wa Kristo Yesu wametundika mwili mtini pamoja na mawazo na tamaa zake mbaya.+ 25  Ikiwa tunaishi kwa roho, na tuendelee pia kutembea kwa utaratibu kwa roho.+ 26  Tusiwe tukijisifu,+ tusichochee mashindano kati yetu,+ wala tusioneane wivu.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “wawe matowashi,” na hivyo wasistahili kufuata sheria ambayo walikuwa wakiitetea.
Au labda, “imejumlishwa.”
Neno la Kigiriki porneiʹa. Angalia Kamusi.
Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.
Au “uchawi.”
Au “karamu za kupindukia.”
Au “sifa zinazotokezwa na roho.”
Au “ustahimilivu.”
Au “kujidhibiti; kujiweza.”