Kwa Waroma 10:1-21

  • Jinsi ya kufikia uadilifu wa Mungu (1-15)

    • Tangazo la hadharani (10)

    • Kumwitia Yehova humaanisha wokovu (13)

    • Miguu ya wahubiri inapendeza (15)

  • Habari njema yakataliwa (16-21)

10  Akina ndugu, nia njema ya moyo wangu na dua yangu kwa Mungu kwa ajili yao, kwa kweli, ni kwa ajili ya wokovu wao.+  Kwa maana ninawatolea ushahidi kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu,+ lakini si kulingana na ujuzi sahihi.  Kwa sababu ya kutojua uadilifu wa Mungu+ bali wakijaribu kujiwekea uadilifu wao wenyewe,+ hawakujitiisha kwa uadilifu wa Mungu.+  Kwa maana Kristo ndiye mwisho wa Sheria,+ ili kila mtu aliye na imani* awe na uadilifu.+  Kwa kuwa Musa anaandika hivi kuhusu uadilifu kupitia Sheria: “Mtu anayefanya mambo hayo ataishi kupitia mambo hayo.”+  Lakini uadilifu unaotokana na imani husema: “Usiseme moyoni mwako,+ ‘Ni nani atakayepanda juu mbinguni?’+ yaani, kumleta Kristo chini,  au, ‘Ni nani atakayeshuka katika shimo?’*+ yaani, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu.”  Lakini linasema nini? “Neno hilo liko karibu nawe, katika kinywa chako na katika moyo wako mwenyewe”;+ yaani, “neno” la imani, ambalo sisi tunahubiri.  Kwa maana ukitangaza waziwazi kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana,+ na kuwa na imani moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokolewa. 10  Kwa sababu kwa moyo mtu huwa na imani ili apate uadilifu, lakini kwa kinywa mtu hufanya tangazo la hadharani+ ili apate wokovu. 11  Kwa kuwa andiko linasema: “Yeyote anayemwamini hatakata tamaa.”+ 12  Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Mgiriki.+ Kuna Bwana yuleyule juu ya wote, aliye tajiri* kwa wote wanaomwitia. 13  Kwa maana “kila mtu anayeliitia jina la Yehova* ataokolewa.”+ 14  Hata hivyo, watawezaje kumwitia ikiwa hawajamwamini? Nao watamwaminije yule ambaye hawajamsikia? Nao watasikiaje bila mtu wa kuhubiri? 15  Nao watahubirije isipokuwa wawe wametumwa?+ Kama ilivyoandikwa: “Jinsi inavyopendeza miguu ya wale wanaotangaza habari njema ya mambo mema!”+ 16  Hata hivyo, si wote waliotii habari njema. Kwa maana Isaya anasema: “Yehova,* ni nani ambaye ameamini jambo alilosikia kutoka kwetu?”*+ 17  Kwa hiyo imani hufuata jambo lililosikiwa.+ Nalo jambo lililosikiwa ni kupitia neno kumhusu Kristo. 18  Lakini ninauliza, je, walikosa kusikia? Kwa kweli, “sauti yao ilifika katika dunia yote, na ujumbe wao ulifika mpaka kwenye miisho ya dunia inayokaliwa.”+ 19  Lakini ninauliza, je, kweli Israeli walikosa kujua?+ Kwanza Musa anasema: “Nitawachochea muwe na wivu kupitia lile ambalo si taifa; nitawachochea muwe na hasira kali kupitia taifa lenye ujinga.”+ 20  Lakini Isaya anakuwa na ujasiri sana na kusema: “Wale ambao hawakuwa wakinitafuta walinipata;+ wale ambao hawakuwa wakiuliza juu yangu walinijua.”+ 21  Lakini anasema kuhusiana na Israeli: “Mchana kutwa nimewanyooshea mikono yangu watu wasiotii na wakaidi.”+

Maelezo ya Chini

Au “anayeonyesha imani.”
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “mkarimu.”
Au “ujumbe wetu.”