Kwa Waroma 4:1-25

  • Abrahamu alitangazwa kuwa mwadilifu kupitia imani (1-12)

    • Abrahamu, baba ya wale walio na imani (11)

  • Kupokea ahadi kupitia imani (13-25)

4  Ikiwa ni hivyo, tutasema alipata faida gani Abrahamu, babu yetu kulingana na mwili?  Kwa mfano, ikiwa Abrahamu alitangazwa kuwa mwadilifu kwa sababu ya matendo, angekuwa na sababu ya kujisifu, lakini si mbele za Mungu.  Kwani andiko linasema nini? “Abrahamu alikuwa na imani katika Yehova,* na hilo likahesabiwa kwake kuwa uadilifu.”+  Basi kwa mtu anayefanya kazi, malipo yake hayahesabiwi kuwa fadhili zisizostahiliwa bali ni deni.  Kwa upande mwingine, mtu asiyefanya kazi bali anaweka imani katika Yule anayemtangaza kuwa mwadilifu mtu asiyemwogopa Mungu, imani yake inahesabiwa kuwa ni uadilifu.+  Kama vile Daudi pia anavyosema kuhusu furaha ya mtu ambaye Mungu humhesabu kuwa mwadilifu bila matendo:  “Wenye furaha ni wale ambao matendo yao ya kuasi sheria yamesamehewa na ambao dhambi zao zimefunikwa;*  mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova* hatahesabu dhambi yake kamwe.”+  Basi, je, furaha hiyo huja tu kwa watu waliotahiriwa au pia kwa watu wasiotahiriwa?+ Kwa maana tunasema: “Imani ya Abrahamu ilihesabiwa kwake kuwa uadilifu.”+ 10  Basi, ilihesabiwa kuwa uadilifu chini ya hali gani? Alipokuwa ametahiriwa au kabla ya kutahiriwa? Ni kabla ya kutahiriwa. 11  Naye alipokea ishara+—yaani, kutahiriwa—kuwa muhuri wa* uadilifu kwa imani aliyokuwa nayo alipokuwa katika hali yake ya kutotahiriwa, ili awe baba ya wale wote walio na imani+ ingawa hawajatahiriwa, kusudi wahesabiwe kuwa waadilifu; 12  na ili awe baba ya uzao uliotahiriwa, si kwa wale tu wanaoshikamana na kutahiriwa, bali pia kwa wale wanaotembea kwa utaratibu katika hatua za imani ambayo baba yetu Abrahamu+ alikuwa nayo katika hali ya kutotahiriwa. 13  Kwa maana Abrahamu au uzao wake* hawakupata ahadi kwamba atakuwa mrithi wa ulimwengu kupitia sheria,+ bali kupitia uadilifu kwa imani.+ 14  Kwa maana ikiwa wale wanaoshika sheria ni warithi, imani inakuwa isiyofaa kitu na ahadi imefutwa. 15  Kwa kweli Sheria hutokeza ghadhabu,+ lakini pasipo na sheria, hakuna kosa lolote.+ 16  Ndiyo sababu ni kupitia imani, ili iwe kulingana na fadhili zisizostahiliwa,+ kusudi ahadi iwe hakika kwa uzao wake* wote,+ si kwa wale tu wanaoshika Sheria, bali pia kwa wale wanaoshika imani ya Abrahamu, ambaye ni baba yetu sote.+ 17  (Kama tu ilivyoandikwa: “Nimekuweka uwe baba ya mataifa mengi.”)+ Hili lilikuwa machoni pa Mungu, ambaye Abrahamu alimwamini, anayewafanya wafu kuwa hai na kuyaita mambo yasiyokuwako kana kwamba yako.* 18  Ingawa hakukuwa na tumaini, lakini kwa kutegemea tumaini, alikuwa na imani kwamba angekuwa baba ya mataifa mengi kulingana na yale yaliyokuwa yamesemwa: “Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”*+ 19  Na ingawa imani yake haikudhoofika, alifikiria mwili wake mwenyewe, sasa ukiwa kama tayari umekufa (kwa kuwa alikuwa na umri wa karibu miaka 100),+ na pia hali ya kufa* ya tumbo la uzazi la Sara.+ 20  Lakini kwa sababu ya ahadi ya Mungu, yeye hakusitasita kwa kukosa imani; bali alikuwa mwenye nguvu kwa imani yake, akimpa Mungu utukufu 21  na akiwa na uhakika kamili kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kutimiza kile alichoahidi.+ 22  Kwa hiyo “ikahesabiwa kwake kuwa uadilifu.”+ 23  Hata hivyo, maneno “ilihesabiwa kwake” hayakuandikwa kwa ajili yake tu,+ 24  bali pia kwa ajili yetu ambao itahesabiwa, kwa sababu tunamwamini Yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu kutoka kwa wafu.+ 25  Alitolewa kwa ajili ya makosa yetu+ na kufufuliwa kwa ajili ya kututangaza sisi kuwa waadilifu.+

Maelezo ya Chini

Au “zimesamehewa.”
Au “dhamana ya; uhakikisho wa.”
Tnn., “mbegu yake.”
Tnn., “mbegu yake.”
Au labda, “anafanya vitu visivyokuwapo viwepo.”
Tnn., “mbegu yako.”
Au “hali ya kuwa tasa.”