Kwa Waroma 5:1-21

  • Kupatanishwa na Mungu kupitia Kristo (1-11)

  • Kifo kupitia Adamu, uzima kupitia Kristo (12-21)

    • Dhambi na kifo vyaenea kwa wote (12)

    • Tendo moja la kutetewa (18)

5  Basi, kwa kuwa sasa tumetangazwa kuwa waadilifu kutokana na imani,+ na tufurahie amani* pamoja na Mungu kupitia Bwana wetu Yesu Kristo,+  ambaye kupitia kwake sisi pia tumepata fursa ya kuingia kwa imani katika fadhili hizi zisizostahiliwa ambamo sasa tunasimama;+ na tushangilie,* kwa kutegemea tumaini la utukufu wa Mungu.  Si hilo tu, bali na tushangilie* tukiwa katika dhiki,+ kwa kuwa tunajua kwamba dhiki hutokeza uvumilivu;+  nao uvumilivu, hali yenye kukubaliwa;+ nayo hali yenye kukubaliwa, tumaini,+  nalo tumaini halikatishi tamaa;+ kwa sababu upendo wa Mungu umemiminwa ndani ya mioyo yetu kupitia roho takatifu, ambayo tulipewa.+  Kwa maana, kwa kweli, tulipokuwa bado dhaifu,+ Kristo alikufa wakati uliowekwa kwa ajili ya watu wasiomwogopa Mungu.  Kwa maana ni vigumu kwa yeyote kufa kwa ajili ya mtu mwadilifu; hata hivyo labda mtu anaweza kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.  Lakini Mungu hupendekeza upendo wake kwetu kwa kuwa tulipokuwa bado watenda dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.+  Kwa kuwa sasa tumetangazwa kuwa waadilifu kwa damu yake,+ tutaokolewa hata zaidi kutokana na ghadhabu kupitia yeye.+ 10  Kwa maana, ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kupitia kifo cha Mwana wake,+ tutaokolewa hata zaidi kwa uhai wake, kwa kuwa sasa tumepatanishwa. 11  Si hilo tu, bali pia tunashangilia katika Mungu kupitia Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake sasa tumepokea upatanisho.+ 12  Hiyo ndiyo sababu, kama vile kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi,+ basi kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi+—. 13  Kwa maana dhambi ilikuwa katika ulimwengu kabla ya Sheria, lakini mtu yeyote hahesabiwi kuwa na dhambi ikiwa hakuna sheria.+ 14  Hata hivyo, kifo kilitawala kama mfalme tangu Adamu mpaka Musa, hata juu ya wale ambao hawakuwa wamefanya dhambi kama vile Adamu alivyofanya kosa, ambaye ni mfano wa yule aliyepaswa kuja.+ 15  Lakini zawadi si kama lile kosa. Kwa maana ikiwa kwa kosa la mtu mmoja wengi walikufa, fadhili zisizostahiliwa za Mungu na zawadi yake ya bure kupitia fadhili zisizostahiliwa za mtu mmoja,+ Yesu Kristo, zilizidi* hata zaidi kwa wengi!+ 16  Pia, ile zawadi ya bure si sawa na jinsi mambo yalivyotendeka kupitia mtu mmoja aliyefanya dhambi.+ Kwa maana hukumu baada ya kosa moja ilikuwa hatia,+ lakini zawadi baada ya makosa mengi ilikuwa tangazo la uadilifu.+ 17  Kwa maana ikiwa kwa kosa la mtu mmoja kifo kilitawala kama mfalme kupitia mtu huyo,+ wale wanaopokea wingi wa fadhili zisizostahiliwa na zawadi ya bure ya uadilifu+ watatawala hata zaidi wakiwa wafalme+ katika uzima kupitia mtu mmoja, Yesu Kristo!+ 18  Kwa hiyo basi, kama vile kupitia kosa moja matokeo kwa watu wa namna zote yalikuwa kuhukumiwa hatia,+ vivyo hivyo kupitia tendo moja la kutetewa matokeo kwa watu wa namna zote+ ni wao kutangazwa kuwa waadilifu kwa ajili ya uzima.+ 19  Kwa maana kama vile kupitia kutotii kwa mtu mmoja wengi walifanywa kuwa watenda dhambi,+ vivyo hivyo pia kupitia kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa kuwa waadilifu.+ 20  Basi Sheria ilikuja ili makosa yaongezeke.+ Lakini mahali ambapo dhambi ilizidi, fadhili zisizostahiliwa zilizidi hata zaidi. 21  Kwa kusudi gani? Ili kama vile dhambi ilivyotawala kama mfalme pamoja na kifo,+ vivyo hivyo pia fadhili zisizostahiliwa zitawale kama mfalme kupitia uadilifu na kuleta uzima wa milele kupitia Yesu Kristo Bwana wetu.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “tuna amani.”
Au labda, “tunashangilia.”
Au labda, “tunashangilia.”
Au “zilifurika.”