Kwa Waroma 9:1-33

  • Paulo awahuzunikia Israeli wa kimwili (1-5)

  • Uzao wa kweli wa Abrahamu (6-13)

  • Mungu akichagua haiwezekani kumpinga (14-26)

    • Vyombo vya ghadhabu na vya rehema (22, 23)

  • Ni mabaki tu watakaookolewa (27-29)

  • Israeli wajikwaa (30-33)

9  Ninasema kweli katika Kristo; sisemi uwongo, kama dhamiri yangu inavyonitolea ushahidi katika roho takatifu,  kwamba nina huzuni kubwa na maumivu yasiyoisha moyoni mwangu.  Kwa maana ningetamani mimi mwenyewe nitenganishwe na Kristo, niwe aliyelaaniwa kwa ajili ya ndugu zangu, watu wangu wa ukoo kulingana na mwili,  ambao ni Waisraeli. Wao ndio waliofanywa kuwa wana+ na kupewa utukufu na maagano+ na Sheria+ na utumishi mtakatifu+ na ahadi.+  Wao ni uzao wa mababu,+ na Kristo alitoka kwao kulingana na mwili.+ Mungu, aliye juu ya wote, asifiwe milele. Amina.  Hata hivyo, si kwamba neno la Mungu limeshindwa. Kwa maana si wote wanaotokana na Israeli ni “Israeli” kihalisi.+  Wala si wote walio watoto kwa sababu wao ni uzao wa* Abrahamu;+ badala yake, “Ule utakaoitwa uzao wako* utapitia kwa Isaka.”+  Yaani, watoto katika mwili si watoto wa Mungu kihalisi,+ lakini watoto kupitia ahadi+ ndio wanaohesabiwa kuwa uzao.*  Kwa maana neno la ahadi lilisema hivi: “Nitakuja wakati huuhuu, na Sara atakuwa na mwana.”+ 10  Lakini si wakati huo tu, bali pia Rebeka alipopata mimba ya mapacha kupitia yule mwanamume mmoja, Isaka babu yetu;+ 11  kwa maana walipokuwa bado hawajazaliwa wala kufanya jambo lolote jema au baya, ili kusudi la Mungu kuhusu kuchagua liendelee kutegemea, si matendo, bali Yule ambaye huita, 12  Rebeka aliambiwa: “Mkubwa atakuwa mtumwa wa mdogo.”+ 13  Kama ilivyoandikwa: “Nilimpenda Yakobo, lakini nikamchukia Esau.”+ 14  Basi, tuseme nini? Je, Mungu ana ukosefu wa haki? La hasha!+ 15  Kwa maana anamwambia Musa: “Nitamwonyesha rehema yeyote ninayetaka kumwonyesha rehema, nami nitamhurumia yeyote ninayetaka kumhurumia.”+ 16  Hivyo basi, haitegemei jinsi mtu anavyotamani au jitihada zake,* bali inategemea Mungu, aliye na rehema.+ 17  Kwa maana andiko linamwambia Farao: “Kwa sababu hii nimekuacha ubaki: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”+ 18  Hivyo basi, yeye humwonyesha rehema yeyote anayetaka, lakini yeye humwacha yeyote anayetaka awe mkaidi.+ 19  Kwa hiyo utaniuliza: “Kwa nini bado analaumu? Kwa maana ni nani ambaye amepinga mapenzi yake?” 20  Lakini ewe mwanadamu wewe ni nani hata uthubutu kumjibu Mungu?+ Je, kitu kilichofinyangwa kitamwambia yule aliyekifinyanga: “Kwa nini ulinitengeneza hivi?”+ 21  Kwani, je, mfinyanzi hana mamlaka juu ya udongo+ kufanya kutokana na donge lilelile chombo kimoja kwa matumizi yenye kuheshimika, na kingine kwa matumizi yasiyo ya kuheshimika? 22  Inakuwaje basi, ikiwa Mungu, ingawa alikuwa na nia ya kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha nguvu zake, alivumilia kwa subira nyingi vyombo vya ghadhabu vilivyo tayari kwa ajili ya uharibifu? 23  Na ikiwa hilo lilifanywa ili ajulishe utajiri wa utukufu wake kwa vyombo vya rehema,+ alivyotayarisha awali kwa ajili ya utukufu, 24  yaani, sisi, ambao alituita si kutoka kati ya Wayahudi peke yao bali pia kutoka kati ya mataifa,+ kuna ubaya gani? 25  Ni kama anavyosema pia katika Hosea: “Wale ambao si watu wangu+ nitawaita ‘watu wangu,’ na mwanamke ambaye hakupendwa, nitamwita ‘mpendwa’;+ 26  na mahali ambapo waliambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ hapo wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’”+ 27  Isitoshe, Isaya anapaza sauti kuhusu Israeli: “Ijapokuwa idadi ya wana wa Israeli huenda ikawa kama chembe za mchanga wa bahari, ni watu wachache tu waliobaki watakaookolewa.+ 28  Kwa maana Yehova* atatoza hesabu duniani, na kuimaliza na kuifupisha.”*+ 29  Pia, kama Isaya alivyotabiri: “Kama Yehova* wa majeshi hangetuachia uzao,* tungekuwa kama Sodoma, na tungefanana na Gomora.”+ 30  Basi, tuseme nini? Kwamba watu wa mataifa, ingawa hawakuwa wakiufuatilia uadilifu,+ waliufikia uadilifu, uadilifu unaotokana na imani;+ 31  lakini Israeli, ingawa walikuwa wakiifuatilia sheria ya uadilifu, hawakuifikia sheria. 32  Kwa sababu gani? Kwa sababu waliifuatilia, si kwa imani, bali kama kwa matendo. Walijikwaa kwenye “jiwe la kukwaza”;+ 33  kama ilivyoandikwa: “Tazama! Ninaweka katika Sayuni jiwe+ la kukwaza na mwamba wa kuangusha, lakini yeye anayemwamini hatakata tamaa.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mbegu ya.”
Tnn., “mbegu yako.”
Tnn., “mbegu.”
Tnn., “yule anayetaka wala yule anayekimbia.”
Au “kuifanya haraka.”
Tnn., “mbegu.”