Wimbo wa Sulemani 1:1-17

  • Wimbo wa nyimbo (1)

  • Msichana (2-7)

  • Mabinti wa Yerusalemu (8)

  • Mfalme (9-11)

    • “Tutakutengenezea mapambo ya dhahabu” (11)

  • Msichana (12-14)

    • ‘Mpenzi wangu ni kama mfuko wa manukato ya manemane’ (13)

  • Mchungaji (15)

    • “Wewe ni mrembo, mpenzi wangu”

  • Msichana (16, 17)

    • “Wewe ni mrembo, mpenzi wangu” (16)

1  Wimbo wa nyimbo,* ambao ni wa Sulemani:+   “Unibusu* kwa mabusu ya kinywa chako,Kwa maana maonyesho yako ya mapenzi ni bora kuliko divai.+   Manukato ya mafuta yako mbalimbali yanapendeza.+ Jina lako ni kama mafuta yaliyomiminwa yenye manukato.+ Ndiyo sababu wasichana wanakupenda.   Nichukue;* acha tukimbie. Mfalme amenileta katika vyumba vyake vya ndani! Na tufurahi na kukushangilia. Na tusifu* maonyesho yako ya mapenzi kuliko divai. Wana* haki ya kukupenda.   Mimi ni mweusi, lakini napendeza, enyi mabinti wa Yerusalemu,Kama mahema ya Kedari,+ kama vitambaa vya mahema+ ya Sulemani.   Msinikodolee macho kwa sababu mimi ni mweusi,Kwa sababu jua limenichoma. Wana wa mama yangu walinikasirikia;Walinifanya kuwa mlinzi wa mashamba ya mizabibu,Lakini sikulinda shamba langu mwenyewe la mizabibu.   Niambie, wewe ninayekupenda* sana,Mahali unapochunga mifugo yako,+Mahali unapoipumzisha wakati wa adhuhuri. Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela*Kati ya makundi ya wenzako?”   “Ikiwa hujui, ewe mwanamke mrembo kuliko wote,Nenda ufuate nyayo za mifugoNa uchunge wanambuzi wako karibu na mahema ya wachungaji.”   “Ewe mpenzi wangu, nakufananisha na farasi jike* kati ya magari ya Farao.+ 10  Mashavu yako yanavutia kwa mapambo,*Shingo yako kwa mikufu ya shanga. 11  Tutakutengenezea mapambo* ya dhahabuYaliyotiwa vifungo vya fedha.” 12  “Mfalme anapokuwa ameketi kwenye meza yake ya mviringo,Marashi* yangu+ hunukia. 13  Mpenzi wangu ni kama mfuko wa manemane unaonukia manukato+Unaokaa usiku kucha katikati ya matiti yangu. 14  Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya hina+Kati ya mashamba ya mizabibu ya En-gedi.”+ 15  “Tazama! Wewe ni mrembo, mpenzi wangu. Tazama! Wewe ni mrembo. Macho yako ni macho ya njiwa.”+ 16  “Tazama! Wewe ni mrembo,* mpenzi wangu, na unapendeza.+ Kitanda chetu kiko kati ya majani mabichi. 17  Maboriti ya nyumba yetu* ni mierezi,Mapau yetu ni miberoshi.

Maelezo ya Chini

Au “Wimbo ulio bora.”
Anayeongea ni msichana.
Tnn., “Nivute nikufuate.”
Au “tusimulie.”
Yaani, wale wasichana.
Tnn., “shela ya maombolezo.”
Au “ambaye nafsi yangu inakupenda.”
Au “farasi jike wangu.”
Au labda, “kati ya nywele zilizosukwa.”
Au “mapambo ya duara ya kichwani.”
Tnn., “Nardo.”
Au “una sura nzuri.”
Au “nyumba yetu kubwa.”