Wimbo wa Sulemani 2:1-17

  • Msichana (1)

    • “Mimi ni ua la zafarani”

  • Mchungaji (2)

    • ‘Mpenzi wangu ni kama yungiyungi’

  • Msichana (3-14)

    • ‘Msiamshe upendo mpaka utakapoamka wenyewe’ (7)

    • Maneno ya mchungaji (10b-14)

      • “Mrembo wangu, njoo twende zetu” (10b, 13)

  • Ndugu za msichana (15)

    • “Tukamatieni mbweha”

  • Msichana (16, 17)

    • “Mpenzi wangu ni wangu mimi, na mimi ni wake” (16)

2  “Mimi ni ua la zafarani tu la mwambao wa pwani,Yungiyungi la mabondeni.”+   “Kama yungiyungi katikati ya miibaNdivyo alivyo mpenzi wangu kati ya mabinti.”   “Kama mtofaa kati ya miti ya msituni,Ndivyo alivyo mpenzi wangu miongoni mwa wana. Natamani sana kukaa katika kivuli chake,Na tunda lake ni tamu kinywani mwangu.   Alinileta katika nyumba ya karamu,*Na bendera aliyoweka juu yangu ilikuwa upendo.   Niburudishe kwa keki za zabibu kavu;+Nilishe matofaa,Kwa maana naugua kwa mapenzi.   Amenishika shingoni kwa mkono wake wa kushoto,Na mkono wake wa kulia unanikumbatia.+   Nawaapisha, enyi mabinti wa Yerusalemu,Kwa swala+ na paa jike wa porini: Msijaribu kuamsha au kuchochea upendo ndani yangu mpaka utakapoamka wenyewe.+   Sauti ya mpenzi wangu! Tazama! Ndiye yule anakuja,Akipanda milima, akirukaruka juu ya vilima.   Mpenzi wangu ni kama swala, kama paa dume mchanga.+ Yule pale, amesimama nyuma ya ukuta wetu,Akichungulia madirishani,Akitazama kupitia viunzi vya madirisha. 10  Mpenzi wangu anaongea, ananiambia: ‘Inuka, mpenzi wangu,Mrembo wangu, njoo twende zetu. 11  Angalia, majira ya baridi* yamepita. Mvua zimekwisha na kwenda zake. 12  Maua yamechanua nchini,+Wakati wa kupunguza matawi umefika,+Na wimbo wa njiwa tetere unasikiwa katika nchi yetu.+ 13  Mtini unaivisha tini zake za mapema;+Mizabibu inachanua na kunukia manukato. Inuka, mpenzi wangu, njoo. Mrembo wangu, njoo twende zetu. 14  Ewe njiwa wangu, kwenye mapango ya miamba,+Kwenye mashimo ya mlimani,Acha nikuone na kusikia sauti yako,+Kwa maana sauti yako inavutia na umbo lako linapendeza.’”+ 15  “Tukamatieni mbweha,Mbweha wadogo wanaoharibu mashamba ya mizabibu,Kwa maana mashamba yetu ya mizabibu yamechanua.” 16  “Mpenzi wangu ni wangu mimi, na mimi ni wake.+ Anachunga kondoo+ kati ya mayungiyungi.+ 17  Mpaka upepo uanze kuvuma* na vivuli kukimbia,Rudi haraka, ewe mpenzi wangu,Kama swala+ au paa dume mchanga+ juu ya milima inayotutenganisha.*

Maelezo ya Chini

Tnn., “nyumba ya divai.”
Au “majira ya mvua.”
Tnn., “siku ianze kupumua.”
Au labda, “milima yenye nyufa.” Au “milima ya Betheri.”