Wimbo wa Sulemani 4:1-16

4  “Tazama! Wewe ni mrembo, mpenzi wangu. Tazama! Wewe ni mrembo. Macho yako ni macho ya njiwa nyuma ya shela yako. Nywele zako ni kama kundi la mbuziWashukao chini kwenye milima ya Gileadi.+   Meno yako ni kama kundi la kondoo waliokatwa manyoya sasa hiviAmbao wametoka kuoshwa,Wote wamezaa mapacha,Na hakuna yeyote aliyepoteza watoto wake.   Midomo yako ni kama uzi mwekundu,Na maneno yako yanapendeza. Kama kipande cha komamangaNdivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya shela yako.   Shingo yako+ ni kama mnara wa Daudi,+Uliojengwa kwa safu za maweNa ngao elfu zimetundikwa juu yake,Ngao zote za mviringo za wanaume mashujaa.+   Matiti yako mawili ni kama paa wawili wachanga,Mapacha wa paa,+Wanaolisha kwenye mayungiyungi.”   “Mpaka upepo uanze kuvuma* na vivuli kukimbia,Nitakwenda zangu kwenye mlima wa manemaneNa kwenye kilima cha ubani.”+   “Wewe ni mrembo kabisa, mpenzi wangu,+Huna kasoro yoyote.   Njoo, bibi harusi wangu, tuondoke Lebanoni,Njoo tuondoke Lebanoni.+ Shuka kutoka kilele cha Amana,*Kutoka kilele cha Seniri, kilele cha Hermoni,+Kutoka kwenye mapango ya simba, kutoka kwenye milima ya chui.   Umeuteka moyo wangu,+ dada yangu, bibi harusi wangu,Umeuteka moyo wangu kwa kunitupia jicho mara moja tu,Kwa kidani kimoja cha mkufu wako. 10  Maonyesho yako ya upendo yanavutia kwelikweli,+ dada yangu, bibi harusi wangu! Maonyesho yako ya upendo ni bora zaidi kuliko divai,+Na manukato ya marashi yako yananukia kuliko kiungo chochote!+ 11  Midomo yako, bibi harusi wangu, inadondosha asali ya sega.+ Chini ya ulimi wako kuna asali na maziwa,+Na manukato ya mavazi yako ni kama manukato ya Lebanoni. 12  Dada yangu, bibi harusi wangu, ni kama bustani iliyofungwa,Bustani iliyofungwa, chemchemi iliyofunikwa kabisa. 13  Machipukizi* yako ni paradiso* ya makomamangaYenye matunda bora kabisa, mimea ya hina na ya nardo, 14  Nardo+ na zafarani, kane*+ na mdalasini,+Iliyo na miti ya kila aina ya ubani, manemane, na udi,+Pamoja na marashi yote yaliyo bora kabisa.+ 15  Wewe ni chemchemi ya bustani, kisima cha maji safi,Na vijito vinavyotiririka kutoka Lebanoni.+ 16  Amka, ewe upepo wa kaskazini;Ingia, ewe upepo wa kusini. Pumueni* kwenye bustani yangu. Manukato yake na yaenee.” “Mpenzi wangu na aje kwenye bustani yakeAle matunda yake yaliyo bora kabisa.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “siku ianze kupumua.”
Au “Milima iliyo ng’ambo ya milima ya Lebanoni.”
Au labda, “Ngozi.”
Au “bustani.”
Utete wenye harufu nzuri.
Au “Vumeni taratibu.”