Wimbo wa Sulemani 7:1-13

  • Mfalme (1-9a)

    • “Unapendeza sana, ewe msichana mpendwa” (6)

  • Msichana (9b-13)

    • “Mimi ni wa mpenzi wangu, naye ananitamani” (10)

7  “Miguu yako inapendeza kwelikweli katika viatu vyako,Ewe binti unayeheshimika! Umbo la mapaja yako ni kama mapambo,Kazi ya mikono ya fundi.   Kitovu chako ni bakuli la mviringo. Kisikose kamwe divai iliyotiwa vikolezo. Tumbo lako ni rundo la ngano,Lililozungukwa na mayungiyungi.   Matiti yako mawili ni kama paa wawili wachanga,Mapacha wa paa.+   Shingo yako+ ni kama mnara wa pembe ya tembo.+ Macho yako+ ni kama vidimbwi kule Heshboni,+Karibu na lango la Bath-rabimu. Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,Unaoelekea Damasko.   Kichwa chako kinakuvika taji kama Karmeli,+Na mashungi ya nywele zako*+ ni kama sufu ya zambarau.+ Mfalme ameduwazwa* na nywele zako ndefu.   Wewe ni mrembo kwelikweli, nawe unapendeza sana,Ewe msichana mpendwa, unazidi vyote vinavyopendeza!   Kimo chako ni kama cha mtende,Na matiti yako ni kama vishada vya tende.+   Nilisema, ‘Nitapanda juu ya mtendeNishike vitawi vyake vyenye tende.’ Matiti yako na yawe kama vishada vya mizabibu,Na pumzi yako inanukia kama matofaa,   Na kinywa chako* kama divai bora kabisa.” “Na ishuke taratibu kwa ajili ya mpenzi wangu,Itiririke taratibu juu ya midomo ya mpenzi wangu.* 10  Mimi ni wa mpenzi wangu,+Naye ananitamani. 11  Njoo, ewe mpenzi wangu,Twende mashambani;Twende tukapumzike kati ya mimea ya hina.+ 12  Tuamke mapema twende kwenye mashamba ya mizabibuTuone ikiwa mzabibu umechipuka,Ikiwa maua yamechanua,+Ikiwa mikomamanga imechanua.+ Huko nitakuonyesha upendo wangu.+ 13  Dudai+ hutoa harufu yake nzuri;Kwenye milango yetu kuna matunda bora ya kila aina.+ Mapya na pia ya zamani,Ewe mpenzi wangu, nimekuhifadhia.

Maelezo ya Chini

Au “ametekwa.”
Tnn., “kichwa chako.”
Tnn., “kaakaa lako.”
Tnn., “midomo ya wanaolala usingizi.”