Wimbo wa Sulemani 8:1-14

  • Ndugu za msichana (5a)

    • ‘Ni nani huyu anayemwegemea mpenzi wake?’

  • Msichana (5b-7)

    • “Upendo una nguvu kama kifo” (6)

  • Ndugu za msichana (8, 9)

    • “Akiwa ukuta, . . . lakini akiwa mlango, . . .” (9)

  • Msichana (10-12)

    • “Mimi ni ukuta” (10)

  • Mchungaji (13)

    • ‘Acha nisikie sauti yako’

  • Msichana (14)

    • “Kimbia mbio kama swala”

8  “Laiti ungekuwa kama ndugu yangu,Aliyenyonya matiti ya mama yangu! Ningekukuta nje, ningekubusu.+ Na hakuna mtu angenidharau.   Ningekuongoza;Ningekuleta ndani ya nyumba ya mama yangu,+Aliyenifundisha. Ningekupa divai iliyotiwa vikolezo unywe,Maji matamu ya makomamanga.   Angenishika shingoni kwa mkono wake wa kushoto,Na mkono wake wa kulia ungenikumbatia.+   “Nawaapisha, enyi binti za Yerusalemu: Msijaribu kuamsha au kuchochea upendo ndani yangu mpaka utakapoamka wenyewe.”+   “Ni nani huyu anayekuja kutoka nyikani,Akiwa amemwegemea mpenzi wake?” “Chini ya mtofaa nilikuamsha. Hapo ndipo mama yako alipopata uchungu wa kukuzaa. Hapo ndipo mama yako alipokuzaa kwa uchungu.   Niweke kama muhuri juu ya moyo wako,Kama muhuri juu ya mkono wako,Kwa maana upendo una nguvu kama kifo,+Na kama Kaburi,* ujitoaji kamili haukubali kushindwa. Miale yake ni moto mkali, mwali wa Yah.*+   Maji yenye nguvu hayawezi kuuzima upendo,+Wala mito haiwezi kuufagilia mbali.+ Kama mtu angejaribu kuuza mali yote nyumbani mwake kwa ajili ya upendo,Mali hiyo ingedharauliwa* kabisa.”   “Tuna dada mdogo,+Ambaye hana matiti. Tutamfanyia nini dada yetuSiku atakapoposwa?”   “Akiwa ukuta,Tutajenga juu yake mnara wa fedha,Lakini akiwa mlango,Tutamziba kwa ubao mpana wa mwerezi.” 10  “Mimi ni ukuta,Na matiti yangu ni kama minara. Kwa hiyo machoni pake nimekuwaKama mtu anayepata amani. 11  Sulemani alikuwa na shamba la mizabibu+ kule Baal-hamoni. Aliwakabidhi watunzaji shamba hilo la mizabibu. Kila mmoja wao alikuwa akileta vipande elfu moja vya fedha kwa ajili ya matunda yake. 12  Nina shamba langu mwenyewe la mizabibu. Hivyo vipande elfu moja vya fedha ni vyako, Ee Sulemani,Na vipande mia mbili ni vya wale wanaotunza matunda ya shamba hilo.” 13  “Wewe unayekaa katika bustani,+Rafiki zako wanasikiliza sauti yako. Acha niisikie.”+ 14  “Kimbia, mpenzi wangu,Kimbia mbio kama swala+ Au paa dume mchangaJuu ya milima yenye viungo.”*

Maelezo ya Chini

Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Au labda, “Angedharauliwa.”
Au “vikolezo.”