Barua ya Yakobo 5:1-20

  • Onyo kwa matajiri (1-6)

  • Mungu huwabariki wanaovumilia kwa subira (7-11)

  • Acheni “ndiyo” yenu iwe ndiyo (12)

  • Sala ya imani ina nguvu (13-18)

  • Kumsaidia mtenda dhambi arudi (19, 20)

5  Haya basi, enyi matajiri, lieni na kupiga mayowe kwa sababu ya taabu zitakazowapata.+  Utajiri wenu umeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.*+  Dhahabu na fedha zenu zimeliwa na kutu, na kutu hiyo itakuwa ushahidi dhidi yenu nayo itakula miili yenu. Vitu mlivyoweka akiba vitakuwa kama moto katika siku za mwisho.+  Tazama! Mishahara ambayo hamjawalipa wafanyakazi waliovuna mashamba yenu, inaendelea kupaza kilio, na vilio vya kuomba msaada vya wavunaji vimefika masikioni mwa Yehova* wa majeshi.+  Ninyi mmeishi kwa anasa na kwa ajili ya kutosheleza tamaa zenu duniani. Mmeinonesha mioyo yenu katika siku ya machinjo.+  Mmemhukumu; mmemuua mwadilifu. Je, yeye hawapingi ninyi?  Basi, iweni na subira, akina ndugu, mpaka kuwapo kwa Bwana.+ Tazama! Mkulima huendelea kungojea matunda yenye thamani ya nchi, akiyasubiri mpaka mvua ya mapema na mvua ya baadaye inyeshe.+  Ninyi pia iweni na subira;+ imarisheni mioyo yenu, kwa sababu kuwapo kwa Bwana kumekaribia.+  Msinung’unikiane,* akina ndugu, ili msihukumiwe.+ Tazama! Mwamuzi amesimama mbele ya milango. 10  Akina ndugu, fuateni mfano wa manabii waliopatwa na uovu+ na kuonyesha subira+ na ambao walisema katika jina la Yehova.*+ 11  Tazama! Tunawaona wale ambao wamevumilia kuwa wenye furaha.*+ Mmesikia kuhusu uvumilivu wa Ayubu+ na mmeona matokeo ambayo Yehova* alileta,+ kwamba Yehova* ni mwenye upendo mwororo sana* na mwenye rehema.+ 12  Zaidi ya yote, akina ndugu, acheni kuapa kwa mbingu au kwa dunia au kwa kiapo kingine chochote. Bali acheni “Ndiyo” yenu iwe ndiyo, na “Siyo” yenu, siyo,+ ili msihukumiwe. 13  Je, kuna yeyote kati yenu aliye na matatizo? Na aendelee kusali.+ Je, kuna yeyote mwenye roho changamfu? Na aimbe zaburi.+ 14  Je, kuna yeyote aliye mgonjwa kati yenu? Na awaite wazee+ wa kutaniko, nao wasali kwa ajili yake, wakimpaka mafuta+ katika jina la Yehova.* 15  Na sala ya imani itamponya huyo mgonjwa,* na Yehova* atamwinua. Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa. 16  Kwa hiyo ungameni waziwazi dhambi zenu+ kwa mtu na mwenzake na kusali kwa ajili ya mtu na mwenzake, ili mponywe. Dua ya mtu mwadilifu ina nguvu nyingi.*+ 17  Eliya alikuwa mtu mwenye hisia kama zetu, na bado aliposali kwa bidii mvua isinyeshe, haikunyesha juu ya nchi kwa miaka mitatu na miezi sita.+ 18  Naye akasali tena, na mbingu ikatoa mvua na nchi ikazaa matunda.+ 19  Ndugu zangu, yeyote kati yenu akipotoshwa kutoka katika kweli na mwingine amrudishe, 20  jueni kwamba yeyote anayemrudisha mtenda dhambi kutoka kwenye kosa+ la njia yake atamwokoa* kutoka kwenye kifo naye atafunika dhambi nyingi.+

Maelezo ya Chini

Aina ya wadudu.
Au “Msizomeane; Msilalamikiane.”
Au “ni mwenye huruma sana.”
Au “wamebarikiwa.”
Au labda, “aliyechoka.”
Tnn., “ina nguvu nyingi inapofanya kazi.”
Au “ataokoa nafsi yake.”